Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Sijui radio producer wa wapi huyu..ebu fuatilieni nyendo zake...ohhh mara wabunge dodoma wanatembea na machangu doa (katika post zake za majuzi) akijiita mwandishi wa habari za uchunguzi...? Oh mara hana kazi ana tafuta kazi ya uandishi wa habari.... Wewe itabidi uwekwe mahali pengine si hapa..... Sikatai unayo yasema lakini kuwa na base kwa kitu unachotaka kusema.... Sasa hapa breaking news ni nini wewe unaejiita journalist?
 
Jaman mbavu sina mimi, yaani watu wameshakata tamaa ya maisha hivi unakubali uponyaji kwa mizizi huku mkiwa mmesubiliana hadi watu mamia! si angeamuru wapone kwa Neno tu sasa hadi wanakufa!
Upupu mwingine bana!:hand::hand::hand:
Imani juu ya jambo ndiyo msingi hata yule mama aliyevuja damu miaka kumi na mbili Imani ilimsukuma kuwa ukishika vazi la Bwana Yesu basi utapona na kweli alifanya hivyo,je hapo ungekuwa wewe si ungemcheka kwa kuchagua kushika vazi na si Imani juu ya uponjaji,Sifa na Utukufu ni kwa Mungu tu kwa huduma anayoifanya huyu babu
 


Uelewa wako wa biblia ni mdogo sana.....nenda kasome vizuri miujiza ya Yesu na utaona masharti aliyokuwa akiwapa watu. Usiwe unakurupuka.
 
Jaman mbavu sina mimi, yaani watu wameshakata tamaa ya maisha hivi unakubali uponyaji kwa mizizi huku mkiwa mmesubiliana hadi watu mamia! si angeamuru wapone kwa Neno tu sasa hadi wanakufa!
Upupu mwingine bana!:hand::hand::hand:

Neno ndio hilo alilooteshwa babu hata akapangiwa kiwango ili kila aaminiye apate uponyaji bila matatizo.
 
Jaman mbavu sina mimi, yaani watu wameshakata tamaa ya maisha hivi unakubali uponyaji kwa mizizi huku mkiwa mmesubiliana hadi watu mamia! si angeamuru wapone kwa Neno tu sasa hadi wanakufa!
Upupu mwingine bana!:hand::hand::hand:

na nani aliumba mizizi ya loliondo? mungu aliumba vitu vinavyoonekana na visivyoonekana ilia mwanadamu akavitumie! na je dawa za mahospitalini nazo niaje?? tuziache na kushika neno???
 
Jaman mbavu sina mimi, yaani watu wameshakata tamaa ya maisha hivi unakubali uponyaji kwa mizizi huku mkiwa mmesubiliana hadi watu mamia! si angeamuru wapone kwa Neno tu sasa hadi wanakufa!
Upupu mwingine bana!:hand::hand::hand:

Hivi ungekuwepo enzi za Yesu alipokuwa duniani, ukamwona anatema mate chini kisha akafinyanga, tope lililotokea akampaka kipofu kisha akamwambia akanawe kwenye birika la Siloam, kisha jamaa akapona upofu wake, si ungesema Yesu ni mganga wa kienyeji au mchawi?

Achana na fikra za wamisheni wakoloni wafanya biashara waliofundisha na kuonyesha kuwa Mungu hawezi kuzungumza kupitia tamaduni zetu na hivyo kila chetu tulicho nacho ni dhambi...wakaua ngoma zetu na dawa zetu za asili ili wauze aspirini na santuri.
 

Mkuu umeshindwa kufika loliondo au umesharudi?
 
Wenye kupona wataendelea kupona, wenye ubishi wataendelea kubisha, lakini kama kweli Mungu nimjuaye ndiye aliyemtuma kuifanya kazi hiyo ataifanya hadi utimilifu wake. Kama Mungu anasingiziwa, anajua kujitetea na hakika atamuaibisha yeyote alitajaye bure Jina lake. Inapofikia mahali mtu anasema Mungu kamtuma, tunashauriwa kuzijaribu kila roho, maana Roho wa Mungu hajigombanishi mwenyewe, pakiwepo mzaha utafumuliwa. Dhambi zote mtu anaweza kusamehewa, lakini anayemkashifu Roho Mtakatifu kamwe hasameheki. Hayo ni maelezo ya moja kwa moja kutoka kinywani mwa YESU KRISTO.
 
What do you expect from Juju Nation? Watu wanapoteza muda wao na mapesa chungu nzima eti kwenda kupata tiba ya ajabu! Bado tuna safari ndefu sana ili kuondokana na imani kama hizi.
 
Hii issue ya babu wa monduli inachanganya kiukweli. Kwa sababu hakuna ajuae hii huduma imetoka kwa mungu,mganga wa kienyeji au shetani mwenyewe.


Why.Babu anasema alioteshwa akiwa amelala usiku akaonywesha mti ambao utasaidia kuwatibia watu.halafu akaambiwa itabidi watu wakufuate huku huku ndio utawapa dawa ya maji ambayo imechanganywa na kipande cha mti huo,na huo mti mtu mwingine akitaka kwenda kuutumia hautafanya kazi.

Hapa ndio suala hili linaponishangaza. Mungu ni mwema sana kwa nini kama ak=mekuja kuwaponya watu wake asiachie mti huu yeyote atkeutumia apone? mpaka uende kwa babu tu ndie awe na umiliki nao,hapa kidogo pana utyata
 
waweza kuuita upupu ila mkuu usicheke, watu walishapata shida sana kwa magonjwa so inawezekana kwa imani na huyo mganga wakapona!
 
Kuna baadhi ya mambo Mungu huweka masharti kwa watu wake hilo halina ubishi
yupo ADAM aliambiwa asilie tunda la kati kati hata yule mke wa Rutu alipoambiwa asigeuke nyuma atakuwa kichuguuu wote hawa walipovunja masharti wote tunafahamu kilichotokea!!!
Au kwa vile wale walilkuwa ni watu weupe ila masharti aliyopewa huyu Mzee unaanza kuhoji?Mbona huoji kwanini Adam alikatazwa kula tunda lakati kati?
 

Ni wapi ambpo Yesu alienda kuombea wagonjwa akawaacha wakafa?? Waliokufa walikuwa mbali si hospitalini kwa Yesu! usilaumu akili finyu tu yakwako haijapimwa! Anayepima akili ya Mtu ni Mungu tu! jionee aibu pliz!
 

Soma kuna replay ya blue color, Wewe bana Mungu hana masharti yaletayo madhara! Tuseme leo Mungu amekasirika sana anaweka masharti hadi wengine wanakufa huku ameamua kuwaokoa??
 
Hongera kwa kupanuka kiakili!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…