Mambo ya Mapenzi ambayo nimejifunza late katika maisha ambayo kijana wa sasa unatakiwa ujifunze mapema

Mambo ya Mapenzi ambayo nimejifunza late katika maisha ambayo kijana wa sasa unatakiwa ujifunze mapema

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241209_123912_Google.jpg


Moja,mtongoze mwanamke lakini usimuonyeshe bila yeye huwezi pata mwanamke mwingine,kadri utakavyo zidi kumfuatilia sana basi tambua ndio jinsi atakavyo kaa mbali na wewe na kukusumbua sana

Mbili,hata umpe mwanamke wako hela nyingi kiasi gani,au uisugue mbususu kiasi gani au usimamie kucha kiasi gani haita mzuia yeye kukuacha,akiamua kukuacha atakuacha tu

Tatu,mjali mpenzi wako au mke wako lakini usijisahau nawe kujiwekea kipaumbele,jithamini nawe pia,usikose vitu vizur au mambo mazuri kwasababu ya kujinyima ili mwanamke wako afurahi

Nne,jitahidi kumridhisha mwanamke kitandani kwa kadri ya uwezo wako,lakini usiharibu afya yako ya uzazi kwa kutumia sijui mkongo na aina nyingine za viagra,mwisho wa siku ukawa mtegemezi wa mambo hayo

Tano,mhudumie mwanamke kwa mapenzi yako na kwa utashi wako,lakini kamwe usidhani kwa kufanya hivyo ndio sababu ya kutoachwa,jua tu kwamba hizo ni huduma tu na si agano au kinga ya kutoachwa,ili ukiachwa usipate msongo wa mawazo kuwa umemgharamia sana

Sita,mpende mwanamke unavyo mpenda lakini usipoteze uanaume wako,kuwa na msimamo,ukisema mbele tembea na iwe hivyo,na ukisema nyuma geuka na iwe hivyo,wanawake wanapenda kuongozwa na sio kuwa na mwanaume ambaye hajui nafasi yake

Saba,kumfuatilia sana mwanamke na kumchunguza ni dalili kwamba una udhaifu mkubwa juu yake au dhaifu kiasi kwamba hujiamini kama anaweza kuwa wako peke yako,hivyo unataka kumlinda kitu ambacho hauta kiweza kamwe

Nane,kuwa na mwanamke au mkeo lakini usimfanye yeye ndio kila kitu chako,kwa maana furaha yako isitegemee uwepo wake maishani mwako,ili siku akiondoka uweze kuendelea na maisha kama kawaida,katika ulimwengu wa mapenzi moyo umeficha mengi

Tisa,kama ambavyo maisha ni kupanda na kushuka,basi hata mapenzi nayo yapo hivyo,leo utalia na kesho utafurahi,mzungumko uko hivyo,kwahiyo wakati wa kufurahi furahi na wakati wa kulia we lia,maisha ndio yalivyo

Kumi,hakuna mjanja katika mapenzi,kwakuwa hujapata misukosuko sasa basi usiwaone wengine ni wajinga,trust me siku yako inakuja na utaelewa hiki ninachosema

Mwisho,Mapenzi hayana mwenyewe ndio maana kila mtu anaumizwa kwa namna moja au nyingine,iwe tajir au maskini wote wamewahi kuumizwa na wanaendelea kuumizwa

Natamani mwanangu wa kiume wa kwanza ayajuaye haya mapema,au Mungu anipe umri mrefu ili ifikie kipindi tuyazungumze haya man to man

Ni hayo tu!
 
Kushoto upande wa dereva nikisubiri comment za MABAUNSA na WAJUVI wa mapenzi , mtoa mada jiandae kukupopolewa😆🙌🏻
Kupopolewa ndio sehemu ya kujifunza,halafu hii ni experience ambayo nimejifunza baadhi kwa kupitia haya na mengine kujifunza kwa wengine

Kwahiyo ni uzoefu wangu na maono yangu na si lazima wengine wayakubali
 
Wakati mwingine unadhani ukiwa nice guy ndio mambo yanaenda vizur lkn kumbe ni kinyume na hali halisi
Mkuu hawa viumbe hawataki upole na ndio mama kwenye muda wote , kuna muda wanatafuta ugomvi ili waone majibu yako. Hii lengo wajue ni mwanume kamili au lah
Kuna wakati wanaitaji commanding voice and decision sio kucheka cheka.

Kuishi na hawa viumbe ni uwe na msimamo, ukiwa legelege unatakimbiwa maana hata ile sense of security and leadership kwako anaona haiwezi kuipata
 
Mkuu hawa viumbe hawataki upole na ndio mama kwenye muda wote , kuna muda wanatafuta ugomvi ili waone majibu yako. Hii lengo wajue ni mwanume kamili au lah
Kuna wakati wanaitaji commanding voice and decision sio kucheka cheka.

Kuishi na hawa viumbe ni uwe na msimamo, ukiwa legelege unatakimbiwa maana hata ile sense of security and leadership kwako anaona haiwezi kuipata
Sahihi sana mkuu, me tangu niijue hii principle maisha yangu yamekua na furaha sana, kuna demu nashangaa miaka nenda rudi yupo tuu hataki kuniacha

Anajua me niko tayar kuachana muda wowote 😀😀😀
 
Mkuu hawa viumbe hawataki upole na ndio mama kwenye muda wote , kuna muda wanatafuta ugomvi ili waone majibu yako. Hii lengo wajue ni mwanume kamili au lah
Kuna wakati wanaitaji commanding voice and decision sio kucheka cheka.

Kuishi na hawa viumbe ni uwe na msimamo, ukiwa legelege unatakimbiwa maana hata ile sense of security and leadership kwako anaona haiwezi kuipata
Ni sahihi kabisa boss wangu,nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja
 
Do experience inahadithwa na kuirisishwa au mpka new commer nae aingie ulingoni ajionee mwenyew
Experience inarithishwa boss,walau vijana watajua abc za mapenzi,hata kuumizwa kunapungua kwakuwa wanajua tayar nini cha kuchafanya na kipi kiepukwe mapema

Tutapunguza huku kupigana na kuchinjana
 
Back
Top Bottom