Mambo ya msingi anayohitaji kila mwanadamu

Mambo ya msingi anayohitaji kila mwanadamu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Maisha ya mwanadamu yanahitaji vitu vikuu vinne:-​
  • Chakula​
  • Sehemu ya kulala​
  • Afya njema​
  • Mavazi​
Chakula
Mwanadamu lazima ahakikishe, miaka yote anapata chakula stahiki, iwe bei imepanda au kushuka, na hii ataitimiza kwa kujiwekea miradi mbali mbali ya kibiashara, kilimo, na ufugaji. Ili kufanikisha hili, ni muhimu kupunguza anasa zinazofuja kipato chako.

Sehemu ya kulala (makazi)
Ni vizuri uwe na sehemu yako ya kulala; uwe una kazi ama huna kazi. Hakikisha unapata sehemu nzuri ya kupumzisha mwili wako. Na hii utafanikisha baada ya kuacha vitu vya anasa anasa.

Afya njema
Afya ndio kila kitu, vitu vya anasa ndivyo chanzo namba moja vya kuangamiza afya ya mwili. Mwili ukilegea, kutimiza malengo mengine ni vigumu; muda mwingi utakuwa unautumia kwenda gereji (hospitali). Hili utafanikisha utakapoachana na vitu vya anasa anasa.

Mavazi
Mavazi ni hitaji pia la muhimu kwa binadamu, na hili utafanikiwa baada ya kupunguza au kuacha vitu vya anasa.

Kwa uchambuzi huu; tumia pesa yako kwa mambo ya maana, achana na starehe, kwa sababu mwisho wake huwa ni mbaya.​
 
Ukiona mawazo ya namna hii yanakujia, kuna issues mbili kwako;

1. Uchumi umeyumba, inabidi ujibane ili uendane na maisha.

2. Umri umekata, unaona kila unapoingia hu-fit na marina mengine.
 
Ukiona mawazo ya namna hii yanakujia, kuna issues mbili kwako;
1. Uchumi umeyumba, inabidi ujibane ili uendane na maisha.
2. Umri umekata, unaona kila unapoingia hu-fit na marina mengine.
Kama ulishajiwekea misingi imara, hata ukilala masaa 12 pesa inaingia tu; kunakuwa hakuna shida
 
Ukiona mawazo ya namna hii yanakujia, kuna issues mbili kwako;
1. Uchumi umeyumba, inabidi ujibane ili uendane na maisha.
2. Umri umekata, unaona kila unapoingia hu-fit na marina mengine.
Umeneno mkuu,
Kabla sijaishiwa vibaya sana,nilikuwa nashindwa kuacha tabia mbaya mbili;knunua nyapu na kucheza kamari.Nilipihika sana na hapo akili ilinikaa nikagundua kumbe zile ni tabia mbaya!

Somo la maisha halifundishwi,unalielewa bila kufundishwa!
 
Haziwezi kubaki, kwa sababu mahitaji ya muhimu ni mengi mno
Maandiko hayakatazi mkristo kunywa pombe, divai wala kinywaji chochote chenye kileo ndani. Maana maandiko mengine huzungumzia kileo kwa kuhalalisha matumizi yake. Mhubiri 9:7 inaamuru, “ kunywa kileo na moyo mkunjufu.” Zaburi 104:14-15 inaeleza Mungu hutoa divai “ inayofurahisha mioyo ya wanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia juu ya kunywa divai kutoka kwa shamba lako kama alama ya baraka za Mungu. Isaya 55;11 inapongeza “ naam, njoo ununue divai na maziwa…”
 
Mahitaji makubwa kwangu mimi ni

1. SELF ESTEEM

2.LOVE AND BELONGNESS

yote haya ukiwa nayo ya juu uliyotaja yatakuja th
 
Umeneno mkuu,
Kabla sijaishiwa vibaya sana,nilikuwa nashindwa kuacha tabia mbaya mbili;knunua nyapu na kucheza kamari.Nilipihika sana na hapo akili ilinikaa nikagundua kumbe zile ni tabia mbaya!

Somo la maisha halifundishwi,unalielewa bila kufundishwa!
Na uzuri MUNGU anakupitisha uko ili akili ikuee na hata kuacha uko milele ktk anasaa
 
Back
Top Bottom