Mambo ya Nyakati: Mbatia, Prof Lipumba, Maalim Seif na Mrema watarejea CCM kabla ya Uchaguzi Mkuu. CHADEMA itabaki kwa mzee Mtei

Siku hizi kuna utumbo unazunguka nchi sana na unatia kinyaa na kichefuchefuuuu sana ..kila mwasisi au mwenyekiti wa chama flani ni Afisa usalama wa nchi analinda nchi kupitia upinzani...Mambo ya kumezeshana sumu sana huko CCM ...tuseme Kila kiongoz wa chama cha upinzani ni afisa usalama...Kuna wengine hawatumikii tena idara hiyo walijitoa full .
 
Vipi CHADEMA bado ina moral authority ya kuongoza upinzani baada ya kununuliwa na Lowassa waliyetumia miaka minne wakimtangaza kuwa ni fisadi, list of shame, hasafishiki?
Kwakuwa umesema ww ni sawa CDM ilinunuliwa na Lowasa. Je fedha hizo alizitowa wapi?? Jibu unalo.

Wanaohangaika kuua/kuumiza upinzani ndiyo wasaliti wakubwa wa maendeleo ktk nchi yetu. Sina haja ya kufafanua hili ila mjiulize kama sio uwepo wa haya makampuni tofauti za simu tungekua tunachati kama tufanyavyo hivi sasa??

Vivyo hivyo ktk sekta ya usafirishaji abiria/mizigo kama sio uwepo wa makampuni mbali mbali kwa wingi haya mafanikio unayoyaona hivi sasa yangekuwepo??

Ushindani ni muhimu sana ktk maendeleo ya nchi yeyote ile. Hebu fikiria mashuleni au vyuoni kama kusingekuwepo na mitihani kungekuaje?? Kiongozi Mkuu wa nchi badala ya kuumiza kichwa juu ya uwepo wa upinzani basi angehakikkisha unaimarika na kuwa bora zaidi kama kweli anaitakia mema nchi yetu.

Nakuhakikishia endapo upinzani utakufa ktk kipindi hiki cha awamu ya tano hakika ataiacha nchi kwenye giza nene ambalo hata yeye mwenyewe atadondosha chozi. Yaani unaikuta nchi ikiwa na vyama vingi na watu wanaheshimiana bila kujali itikadi za vyama vyao halafu ktk uongozi wako unavivuruga kisha kuwakosanisha watu na ww eti unajisifu ni kingozi bora??
 
Pesa ilitoka kule CHADEMA walikotwambia kaiba na akawapa mgao wakapiga kimya toka siku hiyo wakakoma kumwita fisadi wakampa na kijiti kabisa agombee ili aendelee kuwapa mgao akifanikiwa kushinda.
Mimi sifurahii vyama pinzani kufa mimi ninachosema Mbatia asilaumiwe wacha naye ale maana wapinzani wote ni wachumia tumbo kula wale wengine akila yeye kwanini iwe nongwa
 
Pesa ilitoka kule CHADEMA walikotwambia kaiba na akawapa mgao wakapiga kimya toka siku hiyo wakakoma kumwita fisadi wakampa na kijiti kabisa agombee ili aendelee kuwapa mgao akifanikiwa kushinda

Wakafuta na list of shame kwenye website ya chadema
 
Itapendeza sana hao wakienda CCM kwani Dunia itaelewa ni nini Chadema inasema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
So what ? baada ya kuwa wamejiunga CCM?

Bara la Afrika litaendelea kuwa masikini kwa muda mtefu Sana ,hii inatokana na raia wake wengi kuwa wajinga. Kwa mfano kuhama kwa Hawa jamaa kutaisaidiaje nchi?
Je madeni ya taifa yatapungua?
Watumishi wataongezewa mishahara?
Umasikini wa Watanzania utapungua?
Uchumi utapanda?

Kuwa mshabiki wa watu wengine bila kuangalia hatima ya maisha yako na taifa kwa ujumla huo ni ujuha . Huku ni kukubali kutumiwa na watu wengine kwa manufaa yao binafsi.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meku mbona umefura sana...... Siasa ni sayansi na yakupasa upambane na hali yako!
 
Kwa kweli kumtaja Mzee Mrema na Cheyo umewaonea sana kwenye siasa za karne hii . Hawa wazee wamejichokea wanahesabu siku zao za kuishi hapa duniani. Hizo heka heka za kuhama vyama sidhani hata kama zipo kwenye mawazo yao.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
 

Hao wazee walisharejea tangu walipoasisi vile vyama vyao... Wapo kimkakati tu majukumu yao makuu ni kuwarubuni wadanganyika
 
John the Baptist naona huo ndo ukomo was akili zako. Kama Bashite vile!
 
Kwa hesabu za ACT kwa sasa zikifanikiwa bas 2025,Chama kikuu Cha Upinzani Zanzibar kitakuwa ACT ikiwa turufu ya Asset ikitumika vyema.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walijitoaje bwashee?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…