Mambo yakuzingatia unapotafuta forex mentor (mwalimu wa forex)

Mnaongea kana kwamba mnamshambulia Ontario vile
Ila ata yeye Ontario anakuambia "mtu yoyote akikuletea elimu ya forex usikatae ila training ambayo ya kumlipa lazma akuonesha trading zake" kwa maana hyo Ontario lazma atakua anaonesha live trading zake

Mtoa Uzi miaka minne huu mchongo unaujua sema ila ukanyut kimya kmya kama jmo ubinafs ndio unatumaliza Africa hasa apa Tanzania
 
ingia YouTube ,andika dar forex mkt, utapata watu wanazungumza nakukuelekeza hii kitu, kwa kiswahili, kisha Fanya maamuzi. samahanii timu.............. mi sio kama naipinga, ila tunafafanua ukwelii

Naona unasaka views kwa udi na uvumba mkuu [emoji23][emoji23]. HUPATI NG'OO
 
Mimi Binafsi sija Qualify kua Mentor wa hii biashara katika miaka hio minne, Ni miaka hii miwili ndo nimeanza kuonja mafanikio ya hii biashara

Mkuu miaka minne mingi sana aisee mkuu Ontario kachukua miezi mitano akatufungulia milango ya baraka je kwanini ww miaka yote minne umekula peke ako mkuu??
 
Narudia nikiyaona mafanikio ntawasaidia kwa sasa bado kaka uyo mnaemsema kafanikiwa sawa
 
Miaka miwili profitably, kwangu naona bado maaan msingi wa biashara hii sio tukuweza kutengeneza pesa kwa kipindi kifupi bali kuweza kutengeneza kwa kipindi kirefu bila kuzipoteza
 
Hivi kizungu km hakipandi unaweza fanya hii biashara kweli
Hii sio biashara ya waswahili aisee...
Kama Lugha ya Malkia haipandi vizuri na Elimu yako ya kuunga unga au umeishia darasa la saba, hii kitu kutoboza inaweza kuwa ni bahati nasibu.
 
Ukweli mmoja mkubwa ni huu...
Japokuwa hii biashara imekuwepo duniani muda mrefu na hata hapa Tanzania imekuwa ikifanyika kwa miaka mingi sana japokuwa kwa uchache mno, Lakini ni ONTARIO ndio amekuja kutufumbua macho na kutuzibua maskio watanzania tulio wengi kujaribu kuingia kwenye hii biashara.

To be honest, sikuwahi kushiriki mafunzo popote na wala sijawahi kuingia kwenye hii biashara, lakini ufahamu wa hii biashara niliinza kuupata kupitia mada za ONTARIO humu ndani JF na naweza kukiri wazi kuwa ONTARIO ndio mentor pekee wa kwanza wa kitaanzania aliyeweza kuwavutia watanzania wengi kujaribu kuingia kwenye hii biashara.
Yule jamaa anaweza na anajua aisee.
 
Sio wa kwanza tanzania.... sema wa kwanza JF....

Mi nina mwaka wa 8 naifanya hii inshu... ilianza physical now ni digital......

Welcome.

Sent from "La -Vista"
 
Unaposema umependa paragraph ya mwisho, unamaana zingine hukupenda?
Unao uhakika kwamba hizo sifa zingine jamaa zako unao waamini wanazo? Au kila uzi unavamia kubwabwaja kama zumbukuku ku comment husivyovijua.
Sasa nakwambia hivi pesa haina upepo, ni akili na discipline. Hakuna pesa rahisi kwenye forex babujii!
 
Shukran sana BORA wewe unasema ukweli hasa hiyo namba 4, Sio hao wanaodanganya watu ETI "TAJIRIKA NA FOREX TRADING" utapeli huo,,,, kwa ukweli na kwa mazingira yetu hapa TZ sio rahisi kumpata mentor mwenye sifa hizo
Asante mkuu, comment yako iko biyee kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…