Mambo yaliyokuwa yanakuudhi nyumbani ulipokuwa mdogo...

 
Unamsindikiza rafiki yako wa mtaa wa saba huko huko unakutana na mzee halafu anapita bila kukuongelesha hapo ndo unageuka saladin anakukuta nyumbani unajisomea licha ya kuwa yeye alikuwa kwenye pikpik.

Mbavu zinaniumaa ujue[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]eti saladini
 
 
Kuamshwa asubuhi tukateke maji nilikua sipendii..
 
Utakua mkorofi wewe, hahahhah
 
1-Mimi nilikuwa sipendi kumwagilia bustani maana bustaniyetu ilikuwa karibu na barabarani sasa wasichana niliokuwa nasoma nao wananiangalia wananichekaaaa

2-Kitu kingine mzee alikuwa hapendi uende kanisani bila kuchomekea,sasa kama unalazimishwa kufungwa mkanda.Nilikuwa kama mti vile kwa jinsi nilivyokakamaa

3-Kuna siku nikatoka shule sikumkuta mama home ila nikakuta chakula mezani mapaja 2 ya kuku na wali nikajua leo maza kanitunuku msosi mzuri nikapiga yale mapaja yote na wali nikabakiza kidogo,bwana eeeh hamadi nasikia sauti ya mama inasema karibu ingieni ndani,maza kaja na wageni nakile chakula kumbe ndio alikuwa amewaandaalia,nikajiongeza nikaenda kulala kwa shangazi yangu mtaa mwingine nilirudishwa baada ya siku moja maana nilijua kifuatacho ITV ni nini
 
 
niletee kitunguuu-- unaleta
niletee nyanya-- unaleta
niletee kisu-- unaleta
niletee maji-- unaleta
hujakaa sawa
niletee mwiko-- unaleta
hujapumzika unasikia
hebu niletee chumvi
hadi hicho chakula kiive umeshatembea zaidi ya km 10 kufata vitu tu.
Eheeee yaan sipendii hiii kitu,mi utoto wangu jamani halaf nilikuwa naonaga sipo huru kabisa
 
Mi mama ana tabia hiyo mpaka sasa hivi anapenda kutambulisha jamanii sijui wanasikia rahaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…