Mambo yanayonikasirisha Kanisani

Mambo yanayonikasirisha Kanisani

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2016
Posts
14,311
Reaction score
36,056
Wasalaam wana JF,

Kesho jamii nzima ya kikristo au sisi wakatoliki tunaanza kwaresma siku 40 za kufunga na kufanya ibada nyingi.

Pamoja na zoezi hilo, naomba niorodheshe mambo yanayonikera kanisani kama yafuatayo:

1. Kwaya kuimba nyimbo ambazo waumini hawazijui. Yaani wanaimba wenyewe tu mavitu ambayo hatuelewi na hatushiriki;

2. Wingi wa matangazo, makanisa yanakua kama platforms za matangazo, yanapoteza muda na kurefusha ibada;

3. Urefu wa mahubiri, mapadre wanaongea sana, waongee kwa kiasi ujumbe utafika tu;

4. Sadaka za kushtukiza, watu wapewe taarifa mapema watatoa tu; na

5. Kushindwa kufuata ratiba za ibada. Hii ni mikoani zaidi, unakaa zaidi ya nusu saa ibada haijatoka tofauti na ilivyoandikwa kwenye time table.

Nawatakia kwaresma njema.
 
Mfano misa inaanza saa tatu mpaka saa tano ndiyo ratiba yakawaida sasa unakuta kuna ugeni labda wa padri au wale wanafunzi mashemasi matangazo marefu wanaunganisha na wale mabwana
Stori zinakuwa haziishi me huwa naondoka
Ikifika saa tano na dk10 tu

Siku moja mlinzi ananirudisha mzozo wake haukuwa mdogo mlinzi mmoja alikuwa na busara kidogo alielewa hoja yangu
 
Bora wewe, mimi kinachoniuzi ni kutopata nafasi/kutoruhusiwa kumuuliza maswali/ kumkosoa padri juu ya anacho hubiri.
Kanisa katoliki kila siku ya ijumaa saa kumi jioni ni siku ya mafundisho juu ya yale amabyo yanakutatiza. Unaweza kuuliza swali lolote utakalo tatizo wengi hua hamshiriki hichi kipindi. Ibadani sio sehemu ya kuuliza bali kufafanuliwa na kufundishwa neno kadri ya Litrujia

PS. Mimi kikwazo changu ni kwenda kutoa sadaka mbele ya kanisa au kupokea Eucharist mbele ya kanisa halafu ukirudi macho ya waumini ambao wengi ni wanawake wakuangalia mwanzo mwisho. Kwakweli hili ni kikwazo Kwangu
 
Mfano misa inaanza saa tatu mpaka saa tano ndiyo ratiba yakawaida sasa unakuta kuna ugeni labda wa padri au wale wanafunzi mashemasi matangazo marefu wanaunganisha na wale mabwana
Stori zinakuwa haziishi me huwa naondoka
Ikifika saa tano na dk10 tu

Siku moja mlinzi ananirudisha mzozo wake haukuwa mdogo mlinzi mmoja alikuwa na busara kidogo alielewa hoja yangu
Kimsingi ratiba lazima iheshimiwe. Dunia imebadilika
 
Ratiba za makanisa mengi zinaboa sana..hasa haya makanisa taasisi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kanisa katoliki kila siku ya ijumaa ni siku ya mafundisho juu ya yale amabyo yanakutatiza. Unaweza kuuliza swali lolote utakalo tatizo wengi hua hamshiriki hichi kipindi. Ibadani sio sehemu ya kuuliza bali kufafanuliwa na kufundishwa neno kadri ya Litrujia

PS. Mimi kikwazo changu ni kwenda kutoa sadaka mbele ya kanisa au kupokea Eucharist mbele ya kanisa halafu ukirudi macho ya waumini ambao wengi ni wanawake wakuangalia mwanzo mwisho. Kwakweli hili ni kikwazo Kwangu
Kama na swali kuhusiana na hubiri la siku hiyo napataje chance?

#MaendeleoHayanaChama
 
Wengine hizo ibada na makanisa yalishatushindaga mapema sana[emoji23][emoji18].

Just imagine huruhusiwi kukosoa wala kuhoji, na ukiuliza swali kwa muhubiri kama hana jibu sahh ataishia kukupa majibu ya vitisho na kukatisha tamaa.

Sadaka nyingi ambazo ni nje ya mafundisho ya biblia,
Mambo mengi hayana mantiki kabisa, ni bora nikalale bar na walevi wenye hekima kulko kanisani kwenye walevi wa upumbavu
1646160556206.jpg
 
Wasalaam wana JF,

Kesho jamii nzima ya kikristo au sisi wakatoliki tunaanza kwaresma siku 40 za kufunga na kufanya ibada nyingi.

Pamoja na zoezi hilo, naomba niorodheshe mambo yanayonikera kanisani kama yafuatayo:

1. Kwaya kuimba nyimbo ambazo waumini hawazijui. Yaani wanaimba wenyewe tu mavitu ambayo hatuelewi na hatushiriki;
2. Uwingi wa matangazo, makanisa yanakua kama platforms za matangazo, yanapoteza muda na kurefusha ibada;
3. Urefu wa mahubiri, mapadre wanaongea sana, waongee kwa kiasi ujumbe utafika tu;
4. Sadaka za kushtukiza, watu wapewe taarifa mapema watatoa tu; na
5.kushindwa kufuata ratiba za ibada. Hii ni mikoani zaidi, unakaa zaidi ya nusu saa ibada haijatoka tofauti na ilivyoandikwa kwenye time table.

Nawatakia kwaresma njema.
Napenda muda wa kutoa sadaka, muda huo macho yangu huwa kwa warembo na namna walivyopendeza
 
Back
Top Bottom