Siri ya sifuri
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 2,335
- 1,967
Salaam wakuu;
Wahenga walisema"Kuhangaika bure sio sawa na kukaa bure,tena wakasema tembea uyaone.
Naam, leo nilikuwa na vijisent vyangu vilivyotosha kwa nauli ya kwenda mahala fulani na kunirudisha nilipotoka, huyoo kwenye daladala za kigamboni kutokea Tandika safari ikaanza,Daresalaam nzuri bwana asikwambie mtu kitu!
Kwasisi ambao tunatokea mikoani tunapotembea ndani ya jiji ndio kwanza tunajihisi tupo duniani!
lakini kama kawaida vizuri navyo havikosi kasoro,nilipofika kigamboni kwa namna jiji linavyopendeza na kuvutia nikaona bora nivuke kuliko kurudi Tandika kwa njia niliokujia ili niendelee kushangaashangaa na kupunguza ushamba! Ilishakuwa usiku na giza lilishatanda.
Mara pap! Moyo ukaanza kudunda, taratiiibu na kwatahadhari nikaelekea kudandia Panton (ferry)sio yale makubwa, mv magogoni niliyoyazoea, kuna mengine mawili madogo madogo na lile nililopanda lilishajaa watu kwenye viti vyote lakini bado kuna umati wa watu wengine wanatiririka kulipanda hilohilo!tukajaa top, chombo kikang'oa nanga.
Roho mkononi lakini kama watalii vile! Hofu yangu ikarudi tena pale tulipokaribia kufika kwenye upande wa pili, kabla lile pantoni halijapaki vizuri darajani abiria wale waliosimama wakaanza kusukumana kusogea mbele na wale tuliokaa tukaanza kusimama,sasa wote tukawa kwenye hekaheka kila mmoja anataka kuwahi kushuka yeye, mbaya zaidi yule baharia anaesimamia abiria bado hajaruhusu watu washuke kwasababu Pantoni halijakaa sawa darajani.
Ni hatari,hatari sana. Lakini kama ilivyo ada kwa mamlaka zinazohusika kukaa kimya mpaka maafa yatokee,kama hali itaendelea vile basi tujiandae kwa vilio.
(Tenda wema uondoke,malipo kwa Mungu)
Wahenga walisema"Kuhangaika bure sio sawa na kukaa bure,tena wakasema tembea uyaone.
Naam, leo nilikuwa na vijisent vyangu vilivyotosha kwa nauli ya kwenda mahala fulani na kunirudisha nilipotoka, huyoo kwenye daladala za kigamboni kutokea Tandika safari ikaanza,Daresalaam nzuri bwana asikwambie mtu kitu!
Kwasisi ambao tunatokea mikoani tunapotembea ndani ya jiji ndio kwanza tunajihisi tupo duniani!
lakini kama kawaida vizuri navyo havikosi kasoro,nilipofika kigamboni kwa namna jiji linavyopendeza na kuvutia nikaona bora nivuke kuliko kurudi Tandika kwa njia niliokujia ili niendelee kushangaashangaa na kupunguza ushamba! Ilishakuwa usiku na giza lilishatanda.
Mara pap! Moyo ukaanza kudunda, taratiiibu na kwatahadhari nikaelekea kudandia Panton (ferry)sio yale makubwa, mv magogoni niliyoyazoea, kuna mengine mawili madogo madogo na lile nililopanda lilishajaa watu kwenye viti vyote lakini bado kuna umati wa watu wengine wanatiririka kulipanda hilohilo!tukajaa top, chombo kikang'oa nanga.
Roho mkononi lakini kama watalii vile! Hofu yangu ikarudi tena pale tulipokaribia kufika kwenye upande wa pili, kabla lile pantoni halijapaki vizuri darajani abiria wale waliosimama wakaanza kusukumana kusogea mbele na wale tuliokaa tukaanza kusimama,sasa wote tukawa kwenye hekaheka kila mmoja anataka kuwahi kushuka yeye, mbaya zaidi yule baharia anaesimamia abiria bado hajaruhusu watu washuke kwasababu Pantoni halijakaa sawa darajani.
Ni hatari,hatari sana. Lakini kama ilivyo ada kwa mamlaka zinazohusika kukaa kimya mpaka maafa yatokee,kama hali itaendelea vile basi tujiandae kwa vilio.
(Tenda wema uondoke,malipo kwa Mungu)