May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,311
- 9,027
Siku chache zilizopita nimetumia muda mwingi barabarani nikitumia usafiri wa Mabasi yanayofanya safari kati ya Dar Es Salaama na Arusha.
Hakika kuna mengi nimeshuhudia yanayokera mpaka unajiuliza ziko wapi Mamlaka zinazotakiwa kusimamia na kutoa miongozo, ina mana hawaoni haya?
Kati ya mambo niliyoyaona na kukerwa nayo ni pamoja na aina ya maudhui yanayooneshwa kwenye TV screen zilizopo kwenye Mabasi haya.
Hebu Mamlaka iwakumbushe hawa Watoa huduma/Wamiliki kuwa wanawajibika kuwahudumia Watu wenye imani tofauti tofauti badala ya Watu kulazimika kuangalia na kusikiliza nyimbo za kuabudu zisizomuhusu na zilizoegemea upande mmoja tu wa imani, na sanasana ni ya mmiliki wa chombo.
Au la basi Kampuni husika ziweke wazi kuwa wao ni wa Mrengo wa Imani fulani na wanahitaji Abiria wa Imani hiyo tu...au walau basi wacheze maudhui hayo kwa uchache sana, Nyimbo moja au mbili sio mbaya.
Kama hiyo haitoshi nikakutana na kiroja kwenye moja ya Kampuni ambapo Muhudumu anafanya maombi ya kuombea safari...tatizo ni lile lile la kulazimishana Watu kutumia zaidi ya dakika 5 au 6 kusikiliza kero zisizokuhusu. Yaani kwa kuwa tu Muhudumu yeye ni Muumini wa kwa Wazee wa upako basi ataangusha maombi hapo bila kujali kuwa anachokifanya ni kero tu kwa Abiria wengine.
Ifike mahali kuwe na muongozo wa Mtu kusema maneno machache tu yanayotosha kubeba uzito...kwa mfano "Mungu ibariki Safari yetu" au "Mungu tuongoze kwenye hii Safari yetu" n.k badala ya kukera Watu na sala zao ndefu ambazo kama kuna Abiria wa Kihindi ndani ya Basi nyie mmemtenga kwa hizo sala zenu.
Kero nyingine kubwa ni maudhui ya Video za Muziki na Movie...Huwa najiuliza hawa Watu wanatumia vigezo gani kuchagua haya Maudhui, au wao hunufaika na nini kwa hayo Maudhui wanayoonesha kwenye Vyombo vyao hivyo vya usafiri?.
Mara kadhaa utakuta kuna Watoto wengi tu ndani ya Gari na matokeo yake kile wanchodhani kinatuburudisha huishia kuwa Kero kwa Wazazi walioongozana na Watoto wao ndani ya Basi, Hivi mbona zipo nyimbo nyingi tu zisizohusisha watu wanaoshikana shikana au wakiwa wamevaa chupi tu n.k..kwa mfano walicheza Wimbo wa Msanii Mbosso ambapo anashikana shikana na Mwanamke, baadae wakacheza wimbo wa Julio Iglicious ambapo Watu wananyonyana ndimi na nyingine kadhaa.
Nilimshuhudia Mama au Dada yake aliyekuwa amempakata Mtoto wa miaka kama 7 au 8 hivi akiwa anahangaika kumgeuza Mtoto kichwa asiangalie kule kwenye screen, na kama tunavyowajua Watoto basi ilikuwa ni kama wanashindana.
Baadae wakacheza Movie ya Rambo (Rambo 3 ile kama sikosei)Movie imejaa mauaji ya kinyama sana ile, na hata baadhi ya hao Watu wazima walishindwa kuiangalia, cha ajabu huyo Muhudumu na Dereva wake wao wapo mbele kule wala hawaangalii.
Hivi mbona wanazo comedy nyingi tu mule za kina Mkojani na Watu walikuwa wanafurahia? Nilitamani kuwaita kuwalalamikia lakini sidhani hata kama watajali Wabongo hawa na siku inayofuata kila kitu kinaendelea kama kawaida.
Ni lazima kuwe na Miongozo rasmi la sivyo ni tabu sana kwa Abiria.
Chama cha kutetea Abiria na LATRA amkeni, safari inapaswa kuwa sehemu ya burudani sio kero.
Hakika kuna mengi nimeshuhudia yanayokera mpaka unajiuliza ziko wapi Mamlaka zinazotakiwa kusimamia na kutoa miongozo, ina mana hawaoni haya?
Kati ya mambo niliyoyaona na kukerwa nayo ni pamoja na aina ya maudhui yanayooneshwa kwenye TV screen zilizopo kwenye Mabasi haya.
Hebu Mamlaka iwakumbushe hawa Watoa huduma/Wamiliki kuwa wanawajibika kuwahudumia Watu wenye imani tofauti tofauti badala ya Watu kulazimika kuangalia na kusikiliza nyimbo za kuabudu zisizomuhusu na zilizoegemea upande mmoja tu wa imani, na sanasana ni ya mmiliki wa chombo.
Au la basi Kampuni husika ziweke wazi kuwa wao ni wa Mrengo wa Imani fulani na wanahitaji Abiria wa Imani hiyo tu...au walau basi wacheze maudhui hayo kwa uchache sana, Nyimbo moja au mbili sio mbaya.
Kama hiyo haitoshi nikakutana na kiroja kwenye moja ya Kampuni ambapo Muhudumu anafanya maombi ya kuombea safari...tatizo ni lile lile la kulazimishana Watu kutumia zaidi ya dakika 5 au 6 kusikiliza kero zisizokuhusu. Yaani kwa kuwa tu Muhudumu yeye ni Muumini wa kwa Wazee wa upako basi ataangusha maombi hapo bila kujali kuwa anachokifanya ni kero tu kwa Abiria wengine.
Ifike mahali kuwe na muongozo wa Mtu kusema maneno machache tu yanayotosha kubeba uzito...kwa mfano "Mungu ibariki Safari yetu" au "Mungu tuongoze kwenye hii Safari yetu" n.k badala ya kukera Watu na sala zao ndefu ambazo kama kuna Abiria wa Kihindi ndani ya Basi nyie mmemtenga kwa hizo sala zenu.
Kero nyingine kubwa ni maudhui ya Video za Muziki na Movie...Huwa najiuliza hawa Watu wanatumia vigezo gani kuchagua haya Maudhui, au wao hunufaika na nini kwa hayo Maudhui wanayoonesha kwenye Vyombo vyao hivyo vya usafiri?.
Mara kadhaa utakuta kuna Watoto wengi tu ndani ya Gari na matokeo yake kile wanchodhani kinatuburudisha huishia kuwa Kero kwa Wazazi walioongozana na Watoto wao ndani ya Basi, Hivi mbona zipo nyimbo nyingi tu zisizohusisha watu wanaoshikana shikana au wakiwa wamevaa chupi tu n.k..kwa mfano walicheza Wimbo wa Msanii Mbosso ambapo anashikana shikana na Mwanamke, baadae wakacheza wimbo wa Julio Iglicious ambapo Watu wananyonyana ndimi na nyingine kadhaa.
Nilimshuhudia Mama au Dada yake aliyekuwa amempakata Mtoto wa miaka kama 7 au 8 hivi akiwa anahangaika kumgeuza Mtoto kichwa asiangalie kule kwenye screen, na kama tunavyowajua Watoto basi ilikuwa ni kama wanashindana.
Baadae wakacheza Movie ya Rambo (Rambo 3 ile kama sikosei)Movie imejaa mauaji ya kinyama sana ile, na hata baadhi ya hao Watu wazima walishindwa kuiangalia, cha ajabu huyo Muhudumu na Dereva wake wao wapo mbele kule wala hawaangalii.
Hivi mbona wanazo comedy nyingi tu mule za kina Mkojani na Watu walikuwa wanafurahia? Nilitamani kuwaita kuwalalamikia lakini sidhani hata kama watajali Wabongo hawa na siku inayofuata kila kitu kinaendelea kama kawaida.
Ni lazima kuwe na Miongozo rasmi la sivyo ni tabu sana kwa Abiria.
Chama cha kutetea Abiria na LATRA amkeni, safari inapaswa kuwa sehemu ya burudani sio kero.