Mamlaka ya Bandari (TPA) yatoa ufafanuzi kuhusu hali ya ajira za Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam

Ahahahahha eti Kemondo...hii ipo Mwanza au Musoma?

Yaani ukithubutu kuchagua DP World ndo umejiua hapohapo...

Bora upelekwe Chonyonyo...

SEMA hii inatupa nguvi sisi tuliochagua biashara
 
Kimsingi TPA hana mamlaka kwenye bandari kwa sasa na kama angekuwa ana mamlaka kama tulivyo ambiwa hawa wafanyakazi walitakiwa kukabidhiwa kwa DPW! Lakini kimsingi hawa wafanyakazi ni kama wamefukuzwa kazi TPA na ndio maana wanapewa option ya kinachoitwa kuajiriwa maana yake watapewa mikataba mipya na yenye masharti mapya na watapimwa kwa vigezo na hakutakuwa na kufanya kazi bila kufukuzwa kazi hivyo wale watakao ajiriwa na DPW wajiandae kuchapa kazi kweli kweli ……!

Kiufupi watakao baki TPA wengi wao watahamishiwa kwenye ofisi za serikali na mashirika mengine na pia watapelekwa kwenye vibandari vidogo vidogo…..!

Kwa watanzania walivyo na mambo ya hovyo,uvivu ,ujinga nawashauri wabaki TPA….
 
Translation.... Tuma maombi kufanya kazi na TPA Bandarini AU endelea kubaki na sisi tukutafutie nafasi katika bandari nyingine nchini...., Swali linakuja huko pengine kuna uhaba au ndio kupewa contract ambayo mwisho wa siku haiwi renewed / terminated ?

Kwa waliodhani DP watakuja na kuwekeza machinery alafu ajira ziongezeke walikuwa wanota (au wanaendelea kuoata Ndoto za Alinacha)
 
Wamepewa gati nane (8) tu katika Bandari ya Dar es Salaam. Gatio namba 0-7.
TPA bado inaendelea kusimamia gati zingine na bandari zingine.
 
Akili kumkichwa Hao watakaohamia DP world watakua wamemake risk decision watakaokua wamebaki TPA watakua safe Na security ya kazi
 
Wamepewa gati nane (8) tu katika Bandari ya Dar es Salaam. Gatio namba 0-7.
TPA bado inaendelea kusimamia gati zingine na bandari zingine.
Unajua kuna gati ngapi pale bandarini!?
Sehemu iliyo baki ni ya wavuvi tu, hata ile aliyo kuwa nayo tics ambayo ilipewa kampuni haileweki ni janja tu za kumshikia dp word.
Hakuna gati inayo baki, na sgr ikikamilika mpaka mwanza na kigoma nazo atachukua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…