Pre GE2025 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yasitisha Leseni ya Mwananchi kutoa maudhui mtandaoni kwa siku 30

Pre GE2025 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yasitisha Leseni ya Mwananchi kutoa maudhui mtandaoni kwa siku 30

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1727899111613.png


KUSITISHWA KWA MUDA LESENI ZA HUDUMA ZA MAUDHUI MTANDAONI ZILIZOTOLEWA KWA MWANANCHI COMMUNICATIONS LIMITED
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano Tanzania, Sheria Na. 12 ya mwaka 2003, kusimamia huduma za mawasiliano ya Kielektroniki na Posta katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa nyakati tofauti kati ya mwaka 2023 na 2024, TCRA ilitoa leseni za huduma za maudhui mtandaoni (online media services licences) kwa kampuni ya Mwananchi Communications Limited kutoa huduma kwa majina ya The Citizen, Mwananchi Digital, Mwananchi na Mwanaspoti kwa ajili ya utoaji wa huduma za maudhui mtandaoni nchini. Katika utoaji wa huduma na kwa mujibu wa Kanuni ya 16 ya Kanuni za Maudhui Mtandao (the Online Content Regulations) za mwaka 2020, Mwananchi Communications Limited anatakiwa kutokutangaza au kuchapisha kwa Umma maudhui yaliyozuiwa ikiwa ni pamoja na maudhui yanayolenga kudhihaki au kuharibu taswira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tarehe 01 Oktoba 2024 Mwananchi Communications Limited ilichapisha maudhui mjongeo na sauti (audio-visual content) kwenye mitandao yake ya kijamii, maudhui yaliyozuiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 16 ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni zilizorejewa hapo juu. Aidha, maudhui hayo yameleta tafsiri hasi kwa Taifa, jambo ambalo linaathiri na kuharibu umoja, amani na mshikamano wa kitaifa.

UMMA UNATAARIFIWA KUWA, kufuatia kuchapishwa kwa maudhui yaliyokatazwa na yanayopingana na sheria, TCRA imesitisha kwa muda leseni za huduma za maudhui mtandaoni (online media services licences) za Mwananchi Communications Limited (The Citizen, Mwananchi Digital, Mwananchi na Mwanaspoti) kutoa huduma za maudhui mtandaoni nchini Tanzania kwa muda wa siku thelathini (30) tangu tarehe ya kutolewa kwa taarifa hii, wakati masuala mengine ya kiusimamizi yanafanyiwa kazi.

Imetolewa tarehe 02 Oktoba, 2024

PIA SOMA
- Siku ya Uhuru wa Habari: Hakuna Uhuru wa Habari, Bila Uhuru wa Kiuchumi wa Media/Waandishi wa Habari!. Media Njaa Inaweza Kuwa Huru?!

UPDATE:
- Gazeti la Mwananchi larejea hewani baada ya zuio la mwezi kuisha. Ni zile video tu au kuna la zaidi?
 
Safi sana.

Ingependeza,kama Jamiiforums kuwa wanatoa sababu za kupigwa ban watu hapa kama inavyosomeka kwenye taarifa hii ya TCRA kwa Umma.

Hakika tungewajua wapotoshaji na wale wote wenye "kudhihaki au kuharivu Taswira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hatahivyo, hii ni safi sana. Tuende na wakati.
 
Sijui ni kwann mtu akiongea kitu ambacho hukipendi n lazima uumfanye kuwa adui yako.

Mfano, kauli za ccm ni uadui kwa Chadema na kauli za Chadema ni uadui kwa ccm.

Hapo ni kampuni ya Mwananchi wamechapisha kitu ambacho hakipendwi na serikali ndio mana wamepewa adhabu hiyo, hiyo haina tofauti na kipindi kile kuchapisha kura za kuonyesha ni rais gani alikubaliana kwenye siasa zake kiuchumi na JPM kushinda kura hizo na wao kuziondoa mitandaoni.
 
Safi saaaaaaaaaaaaana.

Hawa Mwananchi wanafanya uchochezi. Wametengeneza kibonzo kuonesha kuwa Tz kuna kutekana na kuuana jambo ambalo sio la kweli. Nchi yetu ni ya amani hakuna anayetekwa wala kuuawa.

Nikiripoti kutoka makao makuu ya tisiaraei ni mimi msemaji wa sisimizi.
 
habari na propaganda ni siraha kali za mwanasiasa
hapa kwetu kama waamuzi mahakamani wanapigiwa simu kwa mujibu wa aziz bilionea,
tcra watakua wanatumiwa sms kabisa
 
Wakuu huko Venezuela, kituo kimoja cha habari kimefungiwa kwa sababu editors walichapisha katuni inayoelezea matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea kwenye nchi hiyo.

Hivi mtu unamiliki jeshi, FFU nzima iko chini yako na unaweza kuamua kila kitu kwa kauli moja tu, unaanzaje kufungia media just because kuna kikatuni cha dakika moja kinaelezea matukio yanayoendelea nchini? Still bado tunaogopa vikatuni?

Sasa kama katuni tu inakuogopesha kiasi cha kufungia media nzima upande wa digital kwa siku 30, wale wakina Netanyahu wanaopambana na makombora kutoka Iran, mashambulizi kutoka Hezbollah na mabomu kutoka Hamas mngekuwa kwenye nafasi yao mngeweza?

Je ni sahihi kusema kuwa Venezuela inaongozwa na viongozi dhaifu zaidi kuwahi kutokea?

Nawaonea huruma sana wananchi wa Venezuela na yangu matumaini viongozi wake watajitafakari maana kama vikatuni tu wanaogopa, vita ikitokea bila shaka watakimbia kabisa nchi.

Naomba kuwasilisha!
 
Back
Top Bottom