Pre GE2025 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yasitisha Leseni ya Mwananchi kutoa maudhui mtandaoni kwa siku 30

Pre GE2025 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yasitisha Leseni ya Mwananchi kutoa maudhui mtandaoni kwa siku 30

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Na nyie media pia ni sehemu ya haya, hasa zile media ambazo kutwa kucha hazizungumzii Uhuru wa habari zaidi ya mapambio tu.
Hiyo pia part and parcel of freedom of the press, media iko huru kusema chochote, anayesifu, yuko huru kusifu, anayetaka kuzungumzia uhuru wa habari yuko huru na hata kumsifu mama anaupiga mwingi, rukhsa.
P
 
Mamlaka Tanzania zaifungia Mwananchi kuchapisha habari mtandaoni kwa 'ukiukaji wa kanuni'
h

Chanzo cha picha,MCL
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) imesitisha kwa muda huduma za maudhui ya mtandaoni za Mwananchi Communication Limited (ML) kwa 'ukiukaji wa kanuni'
Katika tangazo lake kwa umma TCRA imesema imesitisha leseni ya huduma za maudhui ya mtandaoni dhidi ya kampuni ya habari ya MCL nchini humo, kwa ukiukaji wa kanuni ya mwaka 2020.
TCRA imesema tarehe 01 Oktoba 2024, MCL ilichapisha maudhui mjongeo na sauti (audio-visual kwenye mitandao yake ya kijami, maudhui yaliyozuiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 16 ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni za mwaka 2020.
''Maudhui hayo yameleta tafsiri hasi kwa taifa, jambo ambalo linaathiri na kuharibu umoja, amani na mshikamano wa taifa’’, imeeleza taarifa ya TCRA , iliyotumwa kwenye mitandao yake ya kijamii:
''Umma unaarifiwa kuwa, kufuatia kuchapishwa kwa maudhui yaliyokatazwa na yanayopingana na sheria, TCRA imesitisha kwa muda leseni za huduma za maudhui mtandano za Mwananchi Communication Limited (The Citizen, Mwananchi Digital, Mwananchi na Mwanaspoti) tangu tarehe ya kutolewa taarifa hii, wakati masuala mengine ya kiusimamizi yanafanyiwa kazi,’’ limehitimisha tangazo hilo.
Mwananchi Communication Limited imesemaje?
Kufuatia kuondolewa kwa leseni hiyo, MCL imetangaza kuondoa maudhui yake ya michoro kwenye mitandao yake ya kijami.
Kupitia gazeti lake la lugha ta Kiingereza The Citizen, kampuni hiyo imesema: ‘’Tumeamua kuondoa michoro iliyoshirikishwa Oktoba 1, 2024 kwenye mitandao ya kijamii (X na Instagram), kwa kuwa ilionyesha matukio yaliyoibua hofu kuhusu usalama wa watu binafsi nchini Tanzania.’’
''Uamuzi wetu wa kuondoa katuni unatokana na kusababisha tafsiri mbaya ambayo ni kinyume na nia yetu’’, taarifa hiyo iliongeza.
Maudhui yaliyoiweka MCL lawamani ni ya katuni ambayo ilikuwa ikionesha raia wa nchi hiyo wakilalama kwenye runinga juu ya matukio ya watu kutekwa na kuuawa nchini humo. Katuni hiyo ilikuwa ikimuonesha mtu ambaye alikuwa akitizama runinga ambaye wengi wametafsiri kuwa ni Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan.
Matukio ya watu kutekwa, kupotezwa na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha yamezua gumzo katika miezi ya hivi karibuni nchini Tanzania.
Chanzo.BBC
 
Mamlaka Tanzania zaifungia Mwananchi kuchapisha habari mtandaoni kwa 'ukiukaji wa kanuni'
h

Chanzo cha picha,MCL
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) imesitisha kwa muda huduma za maudhui ya mtandaoni za Mwananchi Communication Limited (ML) kwa 'ukiukaji wa kanuni'
Katika tangazo lake kwa umma TCRA imesema imesitisha leseni ya huduma za maudhui ya mtandaoni dhidi ya kampuni ya habari ya MCL nchini humo, kwa ukiukaji wa kanuni ya mwaka 2020.
TCRA imesema tarehe 01 Oktoba 2024, MCL ilichapisha maudhui mjongeo na sauti (audio-visual kwenye mitandao yake ya kijami, maudhui yaliyozuiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 16 ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni za mwaka 2020.
''Maudhui hayo yameleta tafsiri hasi kwa taifa, jambo ambalo linaathiri na kuharibu umoja, amani na mshikamano wa taifa’’, imeeleza taarifa ya TCRA , iliyotumwa kwenye mitandao yake ya kijamii:
''Umma unaarifiwa kuwa, kufuatia kuchapishwa kwa maudhui yaliyokatazwa na yanayopingana na sheria, TCRA imesitisha kwa muda leseni za huduma za maudhui mtandano za Mwananchi Communication Limited (The Citizen, Mwananchi Digital, Mwananchi na Mwanaspoti) tangu tarehe ya kutolewa taarifa hii, wakati masuala mengine ya kiusimamizi yanafanyiwa kazi,’’ limehitimisha tangazo hilo.
Mwananchi Communication Limited imesemaje?
Kufuatia kuondolewa kwa leseni hiyo, MCL imetangaza kuondoa maudhui yake ya michoro kwenye mitandao yake ya kijami.
Kupitia gazeti lake la lugha ta Kiingereza The Citizen, kampuni hiyo imesema: ‘’Tumeamua kuondoa michoro iliyoshirikishwa Oktoba 1, 2024 kwenye mitandao ya kijamii (X na Instagram), kwa kuwa ilionyesha matukio yaliyoibua hofu kuhusu usalama wa watu binafsi nchini Tanzania.’’
''Uamuzi wetu wa kuondoa katuni unatokana na kusababisha tafsiri mbaya ambayo ni kinyume na nia yetu’’, taarifa hiyo iliongeza.
Maudhui yaliyoiweka MCL lawamani ni ya katuni ambayo ilikuwa ikionesha raia wa nchi hiyo wakilalama kwenye runinga juu ya matukio ya watu kutekwa na kuuawa nchini humo. Katuni hiyo ilikuwa ikimuonesha mtu ambaye alikuwa akitizama runinga ambaye wengi wametafsiri kuwa ni Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan.
Matukio ya watu kutekwa, kupotezwa na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha yamezua gumzo katika miezi ya hivi karibuni nchini Tanzania.
Chanzo.BBC
Kazi imeanza!
 
Tanzania imesitisha shughuli zake za mtandaoni za wachapishaji maarufu wa magazeti baada ya moja ya machapisho yake kutoa tangazo la katuni linalomuonyesha Rais wa nchi hiyo, Samia Suluhu Hassan, na kurejea matukio ya hivi karibuni ya kutekwa na mauaji ya wapinzani.

Tangazo hilo, lililochapishwa kwenye X na Instagram siku ya Jumanne na Citizen, gazeti la lugha ya Kiingereza, lilionyesha rais akipitia chaneli za TV. Kila kituo kilionyesha watu wakizungumza kuhusu wapendwa wao waliowapoteza kwa kupotea.

Katika taarifa yake usiku wa kuamkia leo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania imesema imeifungia leseni ya mtandao ya Mwananchi Communications inayochapisha Mwananchi na hatimiliki nyinginezo kwa siku 30 kusubiri hatua nyingine za kikanuni. ilisema maudhui yanayokera "yanatishia na huenda yakaathiri na kudhuru umoja wa kitaifa na amani ya kijamii".

Gazeti la The Citizen lilisema litaendelea kuchapisha matoleo ya kuchapisha huku likishirikiana na mdhibiti. mhariri wake mkuu, Mpoki Thomson, alisema katika taarifa kwamba uhuishaji huo umeondolewa kwa sababu ya "tafsiri potofu ambayo imezalisha".

Kipande hicho cha dakika moja kiliwaonyesha watu sita akiwemo kiongozi wa upinzani Tundu Lissu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakieleza masikitiko yao na kusikitishwa na mauaji na kupotea kwa watu.

“Hali ya kisiasa ya nchi yetu si nzuri hata kidogo. Kwanza kabisa, sisi kama chama pinzani, tuko kwenye mazishi. kiongozi wetu ametekwa nyara na kuuawa kikatili,” alisema mhusika Lissu akionekana kuzungumzia kifo cha Ali Mohamed Kibao, mjumbe wa Sekretarieti ya Taifa ya chama hicho, aliyekutwa na umauti mwezi uliopita, kumwagiwa tindikali usoni baada ya kumwagiwa tindikali. kutekwa nyara na watu wenye silaha.

Mhusika mwingine alisema: “Mpaka sasa, kila ninapofikiria kuhusu mtoto wangu mimi hulia tu. Nimechanganyikiwa. Imekuwa muda mrefu, lakini bado siwezi kusahau."

Hassan amekabiliwa na ukosoaji mkubwa wa ndani na kimataifa juu ya madai kwamba vikosi vya usalama vinahusika na utekaji nyara na mauaji ya viongozi wa upinzani. Katika kipindi cha miezi miwili, Serikali imepiga marufuku mikutano miwili ya Chadema na kuwakamata viongozi na wafuasi wake.

Hassan alichukua madaraka baada ya kifo cha ghafla cha kiongozi wa kimabavu John Magufuli mwaka 2021. Hapo awali alitunukiwa kwa kuondoa vikwazo vya mikutano ya upinzani na vyombo vya habari. hata hivyo, waangalizi na makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema Hassan anatumia mbinu za udhibiti na ukandamizaji zilizotumiwa na mtangulizi wake.

Utawala wa Magufuli mara kwa mara ulifuta leseni za magazeti, ikiwa ni pamoja na ile ya Mwananchi, kwa kuchapisha maudhui ambayo uliyaona kuwa mabaya kwa serikali.
 

Attachments

  • 1AA0B44C-07CF-419B-B0DF-F36CB8666B7E.jpeg
    1AA0B44C-07CF-419B-B0DF-F36CB8666B7E.jpeg
    141.2 KB · Views: 2
Mumefikiwa, zamu yenu na nyie
 
Wakuu huko Venezuela, kituo kimoja cha habari kimefungiwa kwa sababu editors walichapisha katuni inayoelezea matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea kwenye nchi hiyo.

Hivi mtu unamiliki jeshi, FFU nzima iko chini yako na unaweza kuamua kila kitu kwa kauli moja tu, unaanzaje kufungia media just because kuna kikatuni cha dakika moja kinaelezea matukio yanayoendelea nchini? Still bado tunaogopa vikatuni?

Sasa kama katuni tu inakuogopesha kiasi cha kufungia media nzima upande wa digital kwa siku 30, wale wakina Netanyahu wanaopambana na makombora kutoka Iran, mashambulizi kutoka Hezbollah na mabomu kutoka Hamas mngekuwa kwenye nafasi yao mngeweza?

Je ni sahihi kusema kuwa Venezuela inaongozwa na viongozi dhaifu zaidi kuwahi kutokea?

Nawaonea huruma sana wananchi wa Venezuela na yangu matumaini viongozi wake watajitafakari maana kama vikatuni tu wanaogopa, vita ikitokea bila shaka watakimbia kabisa nchi.

Naomba kuwasilisha!
Hii imekuja dakika chache baad ya kuposti pia mauaji y kijana alieuliwa unguja na wasiojulikana, mwananchi ndo wakwanza kuposti hiiii


Hii nchi imemshinda
Uovu wa watawala unapowekwa wazi hadharani matokeo yake huwa ni watawala hao kushikwa na hofu Kuu na huwa wanaamua kuwashughulikia Watu walioanika uovu wao hadharani. Ukweli mchungu daima huwa una kawaida ya kuchoma Sana moyoni.
Hata gazeti la MwanaHalisi la Bw. Saed Kubenea liliwahi kufungiwa kwa kufichua uovu wote kabisa kuhusu mpango mzima wa kumteka Dkt. Ulimboka, waovu na wahalifu waliohusika na mpango huo wa kumteka Dkt. Ulimboka walipatajwa hadharani, wenyewe walipata hasira na kuamua kulifungia gazeti lililofichua uovu huo.
 
Back
Top Bottom