Mamlaka za Usafiri Dar hazijali muda wa abiria

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Habari wanaJF,

Hoja hii ni mahsusi kwa watumiaji wa usafiri wa Daladala wanaotumia Mabasi ya Mbezi - Kawe na Mbezi Makumbusho pia wale wa Makumbusho - Mbezi na Kawe - Mbezi.

Angalieni huu mzunguko;

Unatoka Mbezi/Kimara unasimama Taa za Ubungo, ukivuka unasimama tena taa za TCRA kisha unakunja Kona kwenda Kituo Cha Mawasiliano (Simu 2,000) baada ya kutoka kituo cha Mawasiliano unarudi tena Ubungo.

Ubungo unaanza mchakato upya wa kusimama kwenye taa ili uzunguke kurudi kusimama kwenye taa za TCRA ambazo ulishapita.

Zaidi ya Dakika 20 zinatumika kuzunguka eneo moja.

Kwanini msitengeneze ruti mpya ya Mbezi kupitia Mawasiliano na kisha kwenda Makumbusho? (magari haya yapite Sinza, Bamaga na kuelekea Makumbusho)

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Mainjinia hao wanatuchelewesha sana
 
Duh mkuu kumbe siku hizi hiyo ruti ndo ina ujinga huo wa kurudi tena Ubungo utokapo mawasiliano.
Mara ya mwisho kupanda hizo gari ilikuwa ukitoka simu 2000, unaingia barabara ya shekilango/Sinza -mlimani city na kuelekea Kawe/Makumbusho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…