KERO Mamlaka zishughulikie changamoto za Mfumo wa ESS, zinatusumbua Watumishi tunashindwa kujaza taarifa kwa wakati

KERO Mamlaka zishughulikie changamoto za Mfumo wa ESS, zinatusumbua Watumishi tunashindwa kujaza taarifa kwa wakati

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Screenshot_20250205-004557.png
Kumekuwa na changamoto kwa takribani wiki moja sasa kwenye MFUMO wa ESS (Employee Self Service) kushindwa kupakia majukumu ya kiutumishi kwenye kipengele kilichomo ndani ya mfumo huo cha PEPMIS (Public Employee Performance Management Information System) bila kujua changamoto hizo zinatokana na nini.

Mamlaka zipo kimya na Watumishi hawana majibu juu ya changamoto hiyo ya kimfumo kwani unasumbua sana kupita kiasi.

Pia, wakuu wa Idara wamekuwa wavivu kuingia kwenye mfumo kwa kisingizio cha kuwa wako busy na majukumu na kuwaachia MAAFISA ELIMU KATA ambao kimsingi wengi wao nao ni wavivu wa kushughulikia suala hilo na hawajui chochote kuhusiana na mfumo huo kwani nao wamekuwa wakiwaachia Wakuu wa Shule kwa kuwaongezea majukumu bila sababu za msingi.

Mamlaka zione hili na ikiwezekana ziwawajibishe Wakuu wa Idara kwa kutegea majukumu yao.

Pia soma:
~
Tapeli anapigia Watumishi wa Umma na kuwaambia Taarifa zao Binafsi, anazitoa wapi? Mfumo wa ESS upo salama kweli?
~ Serikali iangalie hii changamoto ya Mfumo wa ESS, kuhusiana na Uhamisho
~ Kwa huu utitiri wa matangazo ya kazi ya kuhamia (Transfer vacancy) ndipo tunaamini mfumo wa ESS haufanyi kazi kabisa
~ Wilaya ya Chemba (Dodoma) hawataki kupitisha maombi kwenye Mfumo wa ESS
 
Back
Top Bottom