Man Utd itakuwa timu ya kwanza kuifunga Liverpool katika EPL msimu huu

kama hiyo ni derby bas hata Barcelona na real Madrid ni derby
Ni derby mkuu, ndio maana inaitwa North West Derby. Tena ni miongoni mwa derby bora barani ulaya na duniani kwa ujumla.

Upinzani wao ulianza miaka ya 1880 kuhusu masuala ya bandari. Na sasa ni miaka takribani 55 hakuna mchezaji aliyehama moja kwa moja kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine.
 
Liverpool wako fomu ila hawatoamini watakachokutana nacho. United itacheza kwa mbinu zaidi na itapata matokeo.
Unaweza kuwa sahihi man u kushinda ila maelezo yako kwamba liver watachezea mpira na man u kupak sidhan kama itatokea. Kama umeangalia game kubwa zote za liver mchezo huu wanacheza kwa tahadhari Sana ndo mana mechi na man city, Chelsea na aseno zote ziliisha sare . Klopp amebadilika siku hiz kwa wakubwa anatafuta sare af ndogo anazifunga kama ilivyokua kwa morinho kpnd anachukua ubingwa. Klopp sio wa misimu ya zamani wa kucheza game kubwa na kupoteza ndogo
 
Hebu jiulize, kuna siku gani Man United ya Mou ilishawahi kwenda lini pale Anfield kuchukua Point tatu na kusepa
 
Kama Herrera atakuwa fiti na ataanzishwa siku hiyo, basi Liverpool atakuwa hana chake.

Pia namuona Ashley Young akipewa jukumu flani la kuhakikisha ule upande hatari wa kulia wa Liverpool akiudhibiti ipasavyo kwanzia kwa Trent Alexander Anold mpaka kwa Mo Salah.
 
4-0 Liverpool win
 
Mimi Huwa Nyuzi kama Hizi za Wapiga Ramli Ninaziangalia tu na Kupotezea Coz Zinaandikwa Kwa Ajili ya Mwandishi Kupata Likes tu na si Jengine
Nilitegemea jibu hili, twenzetu kwenye jukwaa letu na thread yetu ya chama letu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…