Maneno aliyoyaongea Nabii Mkuu kipindi anampa gari Muimbaji wa nyimbo za injili yalikuwa ndiyo zawadi na siyo gari: Mwimbaji alishindwa kutafsiri

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Rejea maneno haya ya nabii Mkuu wakati anampa Mwimbaji gari "Mimi napenda kuuona uzuri wa watu na kuuyoa nje". Kwa haraka sana gari hapo limekuja la kiwakilisho tu katika ulimwengu wa vitu (material world) ila ukweli ni kuwa yule Mwimbaji alipewa mguvu ( energy).

Waliomshauri kuchoma gari sijajua kama wanafahamunkuwa nguvu haichomeki na ( unaweza kuchoma nguvu kweli?). Maneno aliyoambiwa na matendo aliyoyafanya yule Mwimbaji mfano kupiga mahoti na kushika viayu vya nabii ni vitendo vya kuruhusu kupokea nguvu. Ninahisi yule Mwimbaji alipokea asichokijua kwa kutawaliwa sana na ulimwengu wa vitu.

Soma Pia: Muimbaji wa injili GodLucky achoma moto gari alilopewa zawadi na mchungaji

Mtu Kwa kujua au kutojua ni nguvu na anaweza kupokea nguvu yoyote ile Kwa kuiruhusu yeye mwenyewe kwa kujua au kutojua.
 
Kwanza ondoa neno NABII MKUU, huyo si nabii mkuu na wala si nabii, hana sifa hizo. Nabii gani anaishi maisha ya kifahari namna hiyo, kuna unabii gani aliuotoa duniani? Simuiti tapeli, namuita mjanja fulani anayecheza na akili za watu wenye ufahamu mdogo wa mambo ya kiroho
 
Mnamuita nabii mkuu kwao mnapajua? Inakuaje kwao ni duni lakini anagawa hela na magari kwa wengine? Anaonekana wa kifahari lakini wazazi wake (baba yake alifariki miaka mitatu iliyopita) na alienda msibani na timu yake toka arusha wakiwa na full chakula cha kuliwa msibani. Aliishia kumsifia mama yake kuwa kazaa nabii mkuu. Cha ajabu mama yake anaishi maisha duni, ina maana msafara wa timu yake toka arusha hawakumshangaa nabii wao kuwa wazazi wake wanaishi mazingira duni na kuona kuwa ana majivuno, kujikweza na kupenda kusifiwa kwa majina makubwa kama dr, mheshimiwa, nabii mkuu? Hao wafuasi wake nao ni kama nyumbu tu!
 
Uduni wa nyumbani hauondoi ukweli kuwa kuna uwezekano wa mtu kufanikiwa kimwili au kiroho.
 
Victor unajua ni kwanini Mungu aliamua kuiteketeza Sodoma na Gomorrah kwa moto na si kwa gharika?
 
NABII MKUU? WHO GAVE HIM THIS AUTHORITY
 
Maneno hata humu JF yamo. Zawadi iliyotolewa ni gari, hakuna haja ya kupindisha kitu kinachoonekana
 
Toa ushauri wako tafadhari, maana hapa wengi tutashindwa kuelewa kama uliunga mkono kuchoma gari au unaungamkono hoja kupewa gari, Hivi huyo mchungaji ndo alisema Yesu akija atapanda gari lake??
 
Hivi kwao ni wapi?
 
Kumpigia mwanadamu magoti na kumshika viatu ni ishara mbaya kiroho na fumbo kwa hadhara. Hao watu 2 wanajua walichokifanya.
 
Je asingempatia gari angekuwa anasikika na kufanya vizuri katika muziki wake ?.
 
Uduni wa nyumbani hauondoi ukweli kuwa kuna uwezekano wa mtu kufanikiwa kimwili au kiroho.
muwe mnajua na kupajua wanakotoka hao manabii wenu, mmezidi mno kuwatukuza na kuwapa sifa zaidi ya Yesu Kristo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…