Maneno matatu ya Kiingereza yaliyobadilishwa maana yake hapa Tanzania

Maneno matatu ya Kiingereza yaliyobadilishwa maana yake hapa Tanzania

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Wataalamu wa lugha husema kwamba lugha ni kitu hai; hukua na kufa. Lugha kadhaa hapa duniani zilikua kisha zikafa mazima, kama kilatini, sanskrit n.k. Sijui jinsi lugha zinavyokufa mazima ila najua jinsi maneno ya lugha fulani yanavyobadili maana.

Pengine huku kubadili maana ndio kukua kwenyewe. Kama ni hivyo, huenda maneno haya ya Kiingereza hapa Tanzania ni ishara kwamba Kiingereza kinapanuliwa hapa nchini.

Maneno ya Kiingereza yanayotumika kwa maana tofauti kabisa hapa nchini ni matatu: local, booking na personality. Tuanze kuyatezama moja moja, maana halisi na jinsi maana ilivyobadilishwa hapa nchini.

1. Local

Neno hili ni kivumishi (adjective) kuelezea kitu cha mahali fulani chenye asili yake hapohapo. Kwa hiyo unapata misemo kama local food = chakula cha eneo hilo, local drinks = vinywaji vya eneo fulani nk.

Local inavyotumika Tanzania

Neno local hutumiwa na watanzania wengi kumaanisha kitu cha ovyoovyo cha kudharaulika. Utasikia wakisema: "Mambo yake ni ya kilocal sana =Mambo yake ya ovyo sana. Kama mtu hajavaa vizuri utasikia: Kavaa kilocal sana huyo!

2. Booking

Hili ni neno linalotumika sana kwenye usafiri likiwa na maana ya kununua tiketi ya usafiri siku kadhaa kabla ya kuanza safari ili kujihakikishia usafiri. Kwa wenzetu kuna ofisi maalumu ya kuuza tikiti kwa wale wanaotaka kusafiri siku za mbeleni. Ofisi hiyo huitwa booking office.

Booking office inavyotumika Tanzania

Niligundua maana ya kitanzania ya booking office nilipofika stendi ya bus na mzigo wa ndizi. "Mzee," waliniambia vijana. "Kwa kuwa gari yako itaondoka mchana, weka huu mzigo booking office." Nikajua kumbe sehemu ya kuhifadhi mzigo kibongobongo huitwa booking.

3. Personality.

Hili ni neno linalotumiwa sana na wanasaikolojia kuzungumzia hali na tabia za watu katika mazingira tofauti.Mathlan, mwanaume akinywa pombe kisha akatokea msichana mrembo mbele yake huyo mwanaume atabadilika? Kubadilika kwa huyo mwanaume na tabia atakayoonesha ndiyo personality yake.

Personality inavyotumika kibongobongo

Mwanaume mrefu mnene aliyevalia suti na kupendeza eti huyo ndiye husemwa ana personality. Utasikia sana: Aisee Mkurugenzi wa ..........ana personality huyo! Kibongobongo msukuma mkokoteni hana personality ni wakubwa tu!
 
Ninavyojua

Local = Kienyeji

Umevaa kilocal, una mambo local = umevaa kienyeji, una mambo ya kienyeji n.k.

Kampuni nyingi za magari, eneo lao la kukatia tiketi hua ni hilo hilo wanahifadhi mizigo. Ulipoambiwa peleka mizigo booking office kwa mazingira yetu walikua sahihi.
 
Ninavyojua

Local = Kienyeji

Umevaa kilocal, una mambo local = umevaa kienyeji, una mambo ya kienyeji n.k.

Kampuni nyingi za magari, eneo lao la kukatia tiketi hua ni hilo hilo wanahifadhi mizigo. Ulipoambiwa peleka mizigo booking office kwa mazingira yetu walikua sahihi.
Hata mie najua local sio ovyo ila ki-local nikienyeji, kiasili zaidi sio modern, kisasa

Iyo booking pia kashindwa ijengea hoja. Personality ni neno linalotumiwa na minority hata Tanzania
 
Wataalamu wa lugha husema kwamba lugha ni kitu hai; hukua na kufa.Lugha kadhaa hapa duniani zilikua kisha zikafa mazima, kama kilatini, sanskrit nk.Sijui jinsi lugha zinavyokufa mazima ila najua jinsi maneno
ya lugha fulani yanavyobadili maana.Pengine huku kubadili maana ndio kukua kwenyewe.Kama ni hivyo, huenda maneno haya ya kiingereza hapa tanzania ni ishara kwamba kiingereza kinapanuliwa hapa nchini.

Maneno ya kiingereza yanayotumika kwa maana tofauti kabisa hapa nchini ni matatu: local, booking na personality.Tuanze kuyatezama moja moja, maana halisi na jinsi maana ilivyobadilishwa hapa nchini.

1. Local. Neno hili ni kisifa, (adjective) kuelezea kitu cha mahali fulani chenye asili yake hapohapo. Kwa hiyo unapata misemo kama local food = chakula cha eneo hilo, local drinks = vinywaji vya eneo fulani nk.

Local inavyotumika tanzania. Neno local hutumiwa na watanzania wengi kumaanisha kitu cha ovyoovyo cha kudharaulika.Utasikia wakisema: "Mambo yake ni ya kilocal sana =Mambo yake ya ovyo sana. Kama mtu hajavaa vizuri utasikia: Kavaa kilocal sana huyo!

Booking. Hili ni neno linalotumika sana kwenye usafiri likiwa na maana ya kununua tiketi ya usafiri siku kadhaa kabla ya kuanza safari ili kujihakikishia usafiri.Kwa wenzetu kuna ofisi maalumu ya kuuza tikiti kwa wale wanaotaka kusafiri siku za mbeleni. Ofisi hiyo huitwa booking office.

Booking office tanzania.Niligundua maana ya kitanzania ya booking office nilipofika stendi ya bus na mzigo wa ndizi. "Mzee," waliniambia vijana. "Kwa kuwa gari yako itaondoka mchana, weka huu mzigo booking office." Nikajua kumbe sehemu ya kuhifadhi mzigo kibongobongo huitwa booking.

Personality. Hili ni neno linalotumiwa sana na wanasaikolojia kuzungumzia hali na tabia za watu katika mazingira tofauti.Mathlan, mwanaume akinywa pombe kisha akatokea msichana mrembo mbele yake huyo mwanaume atabadilika? Kubadilika kwa huyo mwanaume na tabia atakayoonesha ndiyo personality yake.

Personality kibongobongo.Mwanaume mrefu mnene aliyevalia suti na kupendeza eti huyo ndiye husemwa ana personality.Utasikia sana: Aisee Mkurugenzi wa ..........ana personality huyo! Kibongobongo msukuma mkokoteni hana personality ni wakubwa tu!
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Tena walikuwa sahihi kuliko kawaida,Ofisi nying za kukatia tiketi za kusafiria ndipo hapohapo wanatunzia na mizigo ya wasafiri wao,hata ukituma kifurushi(parcel)utaenda kuchua hapohapo Booking office.
 
Ninavyojua

Local = Kienyeji

Umevaa kilocal, una mambo local = umevaa kienyeji, una mambo ya kienyeji n.k.

Kampuni nyingi za magari, eneo lao la kukatia tiketi hua ni hilo hilo wanahifadhi mizigo. Ulipoambiwa peleka mizigo booking office kwa mazingira yetu walikua sahihi.


Hata local motive (na sio locomotive) ni msukumo wa kienyeji.
 
Ninavyojua

Local = Kienyeji

Umevaa kilocal, una mambo local = umevaa kienyeji, una mambo ya kienyeji n.k.

Kampuni nyingi za magari, eneo lao la kukatia tiketi hua ni hilo hilo wanahifadhi mizigo. Ulipoambiwa peleka mizigo booking office kwa mazingira yetu walikua sahihi.
Kula tano, tafsiri ya maneno inatokana na tafsiri halisi kwenye matumizi ya neno.
 
Usisahau na phrase "some how".

- kwenye kizungu inamaana inayotaka kufanana na ajabu, kimaajabu. Viz. Despite being lazy at school he some how managed to pass all his exams.
- kibongobongo some how inatumika kuashiria hali ya nafuu, angalau au afadhali.

Zimekuja na meli Hizi....sio shida sana bora tunaelewana tu.

Huwa napenda sana neno "issue" likitamwa "inshu"..... Lakini angalau katika hili maana yake haijabadilika sana katika ile halisi.
 
Mtoa mada umeshindwa 100% . kwanza umeshindwa kuwasikikiza wazungumzaji na kuwaelewa ipasavyo. Wazungumzaji wapo sahihi kabisa kwenye hayo maneno kama yanavyotumiwa na waingereza Ila ni wewe tu umetafsiri ujuavyo. Local ni kienyeji ,
 
Hiv huwa zinaitwa side-mirror au site-mirror
 
Umesahau
1. Roast
2. Amazing
3. At the end of the day
Kweli ndugu! Asante kunikumbusha. Sina muda wa kuzizungumzia hapa, (hasa roast na amazing) huenda nikaziandikia thread baadaye.
 
Back
Top Bottom