Maneno ya Rais wa Tunisia ni dharau kwa Waafrika

Ubaguzi hata sisi tunao,
Tunaona Ngozi nyeupe ni bora kuliko nyeusi,
Mtoto mdogo akiwa mweupe kila Mtu atamsifia kua ni Mzuri lakini akiwa Mweusi watamzungumzia kwa Weusi wake,

Mwanamke akiwa Mweupe huonekana mzuri na mrembo akiwa Mweusi ataonekana havutii na hao Wanawake hata kwenye thamani ya Mahari hutofautishwa,

Ukifua utatenganisha nguo nyeupe na nyeusi, utaanza kwa kufua nyeupe kwa ustadi mzuri na kumalizia kulipua lipua nguo nyeusi,

Rais ana haki ya kupata hiyo hofu, wahamiaji wakiwa wengi kuna uwezekano wa kuzaliana kwa wingi na baada ya Miaka fulani kizazi cha weupe asilia kikapotea,

Sio WaTunisia pekee wenye hofu hiyo hata Wachina, Warusi, Waingereza,Wajerumani, tena Waisrael walienda mbali sana kwa kusema Ngozi nyeusi ni kama Kansa isipoondolewa haraka husambaa kila sehemu.
 
Mbona team kama Al hilal ya Sudan haina mwarabu koko hata mmoja
 
Upo sahii mkuu ubaguzi ni dhambi ya wote
 
FaizaFoxy huwa anawaita hao Waarabu ni waafrika kumbe ni 'race' mbili tofauti kabisa.
Tatizo lako huelewi Uarabu ni nini na Uafrika ni nini .

Pata darsa ili uelewe ukiwa na uwezo wa kuelewa...
Mwafrika = ni mtu anaetoka kontinenti la Afrika, sio rangi yake, sio kabila lake.

Mwarabu = ni mtu ambae lugha yake ni Kiarabu na anafata mila za Kiarabu (ustaarabu). Siyo rangi yake wala siyo dini yake, wala siyo kabila lake.

Wewe siyo mstaarabu?
 
Mbona Sudan hujaitaja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…