Maneno yaliyoandikwa kwenye geti la kuingia Chuo Kikuu cha Cape Town, yana funzo kubwa!

Maneno yaliyoandikwa kwenye geti la kuingia Chuo Kikuu cha Cape Town, yana funzo kubwa!

Heci

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
3,591
Reaction score
6,114
education.jpg

Kwenye geti la chuo kikuu cha Cape Town nchini Afrika kusini kuna maandishi yasemayo "Ukitaka kuangamiza taifa lolote duniani huhitaji kutumia silaha za nyuklia wala mabomu ya atomic. Njia nzuri ya kuangamiza taifa ni kuharibu mfumo wa elimu. Ruhusu "mbumbumbu" waonekane wamefaulu na wasonge mbele.

Matokeo yake yatajionesha baada ya muda, "mbumbumbu" hao wakishahitimu. Wagonjwa watafia mikononi mwa madaktari, majengo yataanguka mikononi mwa wahandisi, pesa zitapotelea mikononi mwa wachumi, utu utapotea mikononi mwa viongozi wa dini, na haki itapotelea mikononi mwa mahakimu. Kuchezea elimu ni kuangamiza taifa!
 
kusahihisha mitihani kwa njia ya mashine kumepekekea wanafunzi kufanya mitihani ya hesabu kwa njia ya kuchagua maswali bomu hilo

usitoze michango ya walimu wa ajira za muda huku shule nzima walimu wa sayansi na hisabati ni wanne tu bomu hilo

tunapanda mbegu ya uharibifu sisi wenyewe
 
kusahihisha mitihani kwa njia ya mashine kumepekekea wanafunzi kufanya mitihani ya hesabu kwa njia ya kuchagua maswali bomu hilo

usitoze michango ya walimu wa ajira za muda huku shule nzima walimu wa sayansi na hisabati ni wanne tu bomu hilo

tunapanda mbegu ya uharibifu sisi wenyewe
Kweli kabisa.
 
Kwenye geti la chuo kikuu cha Cape Town nchini Afrika kusini kuna maandishi yasemayo "Ukitaka kuangamiza taifa lolote duniani huhitaji kutumia silaha za nyuklia wala mabomu ya atomic. Njia nzuri ya kuangamiza taifa ni kuharibu mfumo wa elimu. Ruhusu "mbumbumbu" waonekane wamefaulu na wasonge mbele.

Matokeo yake yatajionesha baada ya muda, "mbumbumbu" hao wakishahitimu. Wagonjwa watafia mikononi mwa madaktari, majengo yataanguka mikononi mwa wahandisi, pesa zitapotelea mikononi mwa wachumi, utu utapotea mikononi mwa viongozi wa dini, na haki itapotelea mikononi mwa mahakimu. Kuchezea elimu ni kuangamiza taifa
 
Vioni kuna vituko na mashuleni kuna uozo, alafu tunahubiri serikal ya viwanda, labda v-war nda.
 
Back
Top Bottom