Nani kasema naogopa kufa? Umemtilia maneno Lowassa unaona haitoshi sasa unanitilia maneno na mimi? Kipi bora, aliyedhoofu na anaishi akiwa na akili timamu au anayepiga pushapu kumbe ana magonjwa yanayoweza kumuua anytime? Pili, Lowassa udhoofu kaanza lini? Maana kabla hajahama si alikuwa na vyeo kibao ndani ya CCM? Hamkuuona udhaifu wake back then? Tufanye Lowassa alienda kwa babu wa Loliondo kwa sababu ni mgonjwa, je huyu anayepiga pushapu hovyo yeye alienda kwa sababu anaumwa nini?
Tukitaka Rais wa kiingereza, tumpigie kura mzungu tumalize. Halafu ndio unajiita msomi wa enzi? Hahaha. Putin kila siku anahutubia kwa uhuru kwa lugha yake, hana kiingereza. Lugha sio Ishu na kuchapia ni suala la kawaida. Rais ambaye amepimwa kwa vigezo vya uwajibikaji ndiye suluhisho. Magufuli unamwonaje?? Ukitafuta records za Lowassa ni za kumwulika kwa tochi. Sana sana utasikia madili aliyokuwa anashiriki yeye na mzee wake Kingu (watoto wao pia ni shida nyingine mjini, wanatumia mivuli ya dingi zao kufanya dirty stuffs, u want me to name them? Rizimoko inclusive)..
Nilijua tu utajaribu kupindua hoja hii, lakini kwenye hili huchomoki kijana. Putin elimu yake toka msingi anafundishwa kwa lugha yake ya kirusi. Hivyo si ajabu kutojua kingereza. Huku kwetu kuanzia form one lugha ya kufundishia ni kingereza, sasa kama mtu ana degree tatu halafu anashindwa kujua matumizi ya singular na plural, mambo tuliyofundishwa primary school kwenye vitabu vya musa na neema (ulivitumia?), tumueleweje? Huyu ni bingwa wa kukariri tu, ndio maana hata kampeni yake anakopi na kupesti. Wewe lete video za Lowassa na Magufuli hapa tulinganishe sio unipe kazi za kwenda kuzitafuta, hoja si yako? Hoja zangu nilete video na za kwako pia nilete video? Mi nitachukulia kuwa hakuna kitu kama hicho.
Hayo mambo ya sijui mzee nani ni zile zile stori zako zisizokuwa na mashiko, sihangaiki kuzijibu kwa sababu HAZINA USHAHIDI. Halafu isitoshe wewe ndio ujieleze kwa sababu hao kina Rizmoko si ni wabunge wa CCM? Huyo mzee Kingu si mwanachama wa CCM? Mmewafukuza? Hapo ndipo unaponishangaza, mafisadi wamo kwenu lakini huishi kumtaja Lowassa tuu. Anyway, ushahidi uliopo ni ule wa kuuza nyumba za serikali kwa MICHEPUKO! Soma habari hii ambayo mwandishi wake ni MSEMAJI WA SASA WA IKULU YA CCM, jinsi inavyomuelezea mgombea wako wa CCM! Patamu hapo!
Bomu linalomwandama Magufuli
Info Post
Subi Nukta
7/26/2015 07:50:00 PM
No Comment
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD="align: center"]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption, align: center"]John Magufuli[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...
Huyu Ndiye Pombe Magufuli:
- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani
ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.
Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo' katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.
Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.
Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.
Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.
"Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi," vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.
Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.
"Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili," chanzo hicho cha habari kinaeleza.
Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.
Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.
Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.
Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.
Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.
Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.
Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.
Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.
Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.
Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.
Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.
Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.
Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.
Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.
"Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.
Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.
Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.
Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.
SALVA RWEYEMAMU
RAI
Na nyingine tena just in case hutaki kuamini kuwa mgombea wako ana utata:
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, ameweka kiporo baadhi ya maswali likiwamo kuhusu uuzaji wa nyumba za serikali, kazi aliyoisimamia akiwa Waziri wa Ujenzi, katika Serikali ya Awamu ya Tatu.
Magufuli aliweka kiporo kujibu maswali hayo yaliyoelekezwa kwake wakati wa mahojiano maalumu yaliyofanyika mjini Tabora, Septemba 15, mwaka huu. Mahojiano hayo yalichapishwa Jumatano wiki iliyopita, katika Gazeti la Raia Mwema.
Mbali na swali kuhusu uuzaji wa nyumba za serikali, maswali mengine aliyoahirisha kuyajibu ni pamoja na kuhusu gharama kubwa za ujenzi wa barabara nchini ikilinganishwa na baadhi ya nchi, sambamba na ubora wa barabara hizo.
Swali hilo la nyumba, ambalo ni sehemu ya maswali 11 kwake liliuliza; "Suala la uuzaji wa nyumba za serikali ambalo limetekelezwa katika wakati ambao ukiwa Waziri wa Ujenzi bado gumzo na limekera Watanzania wengi. Unasemaje kuhusu hili?"
Kutokana na maswali hayo ambayo yalitangulizwa kwa Magufuli takriban wiki moja kabla ya mahojiano rasmi, maswali husika hayakujibiwa kwa maelezo kwamba yatajibiwa na Magufuli katika mahojiano yatakayopangwa wakati mwingine.
Uuzaji wa nyumba za serikali ulitekelezwa katika uongozi wa Rais Benjamin Mkapa na nyumba zaidi ya 8,000 ziliuzwa, baadhi zikiwa zimejengwa katika maeneo nyeti.
Inadaiwa kwamba katika uuzaji huo wa nyumba, Magufuli aliingilia mchakato wa uuzaji ambao unatajwa ulipaswa kusimamiwa moja kwa moja na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA).
Katika uingiliaji huo, Magufuli anadaiwa kufanikisha uuzaji wa mojawapo ya nyumba hizo za kwa Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo anayedaiwa kuwa ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.
Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa serikali na si Waziri wa Ujenzi wa wakati huo. Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee TBA ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.
Katika mauzo hayo ya nyumba, serikali inatajwa kutarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00, lakini taarifa zilikuwa zikionyesha kwamba imepata shilingi 22,684,108,115.08.
Miongoni mwa nyumba zinazomilikiwa na serikali kwa sasa ni 1,098 zinazosimamiwa na TBA, kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.
Katika bajeti ya mwaka 2010/2011, serikali, kupitia Wizara ya Ujenzi iliwasilisha bajeti yake bungeni mjini Dodoma na kueleza kwamba inataraji kutumia takriban Sh bilioni 5.7 kujenga nyumba mpya ili kuokoa mamilioni yanayotumika kuwalipia watumishi wanaolazimika kukaa hotelini kwa kukosa nyumba.
Hata hivyo, kiasi hicho cha fedha kilichotengwa kwa wakati huo ni pungufu ikilinganishwa na kile kilichotengwa awali, katika bajeti iliyotangulia ya 2009/2010, Sh bilioni 11.4 kwa ajili ya ujenzi huo wa nyumba. - See more at:
Raia Mwema - Magufuli aweka kiporo uuzaji nyumba