Manguli wa Siasa, Zitto Kabwe, Stephen Wassira, John Cheyo, Kuunguruma Kwenye Kipindi cha KMT cha Channel Ten, Kila Jumapili Saa 3:00 Usiku, Usikose!

Manguli wa Siasa, Zitto Kabwe, Stephen Wassira, John Cheyo, Kuunguruma Kwenye Kipindi cha KMT cha Channel Ten, Kila Jumapili Saa 3:00 Usiku, Usikose!

Nitawatafuta in due time!.
P
Wewe unafanya hiyo kazi under ccm instructions kwahiyo watu wenye akili hawawezi kuwa kwenye vipindi vyako ; kwani watawaumbua na propaganda zenu!! Hao wakina Lipumba, Cheyo na Wasira hao wote ni waganga njaa ; wapo hapo kwa maslahi yao binafsi na sio maslahi mapana ya wananchi!
 
Kwanini usiende polisi kutoa taarifa,maana uvutaji bangi ni kosa kisheria.Hiyo itakua njia nzuri ya kumsaidia Mdude na wanajamii wengine,au polisi wenyewe wangekuita,ili uwasaidie katika kutoa ushahidi mahakamani.Fanya hivyo mkuu.
Msimpeleke Mdude peke yake na Chalamila nae mumpeleke!
 
Naunga mkono hoja, kiukweli tuna tatizo kubwa sana na wanasheria majanga kwenye mihimili yote, serikali inatunga muswada wa sheria batili, Bunge linaitunga kuwa sheria. Mahakama inashindwa kutafsiri katiba!, kati ya wanasheria majanga wote, madhara kakubwa ni majaji!, Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?
P
Tanzania ilikuwa inatoa Wanasheria wazuri sana ukanda wa EA. Kwasasa sijui Majaji wanapatikanaje

Hii kesi ina 'effect' mbele ya safari kwa upekee wake. Haikuwa kubwa kihivyo, Hakim Mkazi Kisutu angeimaliza.
Kutokana na Figisu Mahakama kuu ikaingia na matokeo ni kujipaka matope.

Imekuzwa kwasasa ni 'landmark' . Maamuzi kama alivyoanisha JokaKuu utagundua Mahakama imeboronga.

Kwavile ni 'landmark' vyama vya siasa vinapaswa kuangalia katiba zao ili asije mtu kutumia hukumu dhidi yao.

Hilo ni kinyume na misingi ya uendeshaji wa vyama. Hatuwezi kuwa na mfumo mmoja unaoratibu Katiba za vyama.

Si kazi ya Jaji kueleza Katiba za vyama ziweje, ni kazi ya Jaji kutafsiri Katiba hizo kwa mujibu wa sheria.

Uwepo wa Wajumbe wa CC ya Chadema hata kama ulikuwa na influence katika maamuzi, Katiba haikukiukwa.

Lakini pia ' Professional judgement' ipo wapi.

Tayari alisharidhia CC ilitenda haki, je, Wajumbe wa CC katika baraza kuu waliathiri kura kivipi?
Na ikiwa Chadema itaitisha Baraza kuu na kuondoa Wajumbe wa CC hilo litabadili vipi matokeo?

Tuna tatizo kubwa katika mhimili wa sheria, Majaji wetu ni 'sub standard' . Pengine tunahitaji uongozi mpya, ule wa akina Nyalali, Samatta, Nassoro Mzavas, Kisanga, Lugakingira na watu kama akina Murtaza , Manning na Longway! n.k.

Sijui Mahakama inahitaji 'revamp au overhaul' sijui! ninachojua ipo compromised
 
Tanzania ilikuwa inatoa Wanasheria wazuri sana ukanda wa EA. Kwasasa sijui Majaji wanapatikanaje
Upatikanaji wa majaji ni mchakato mzuri tuu, tatizo ni hakuna kipimo cha amplitude test kupima uwezo wa majaji kubaini haki.
Hii kesi ina 'effect' mbele ya safari kwa upekee wake. Haikuwa kubwa kihivyo, Hakim Mkazi Kisutu angeimaliza.
Kutokana na Figisu Mahakama kuu ikaingia na matokeo ni kujipaka matope.
The truth hapa kulikuwa hakuna kesi kabisa kama Chadema wangetimiza wajibu wao kikamilifu.
  1. Baada ya wabunge 19 kuibukia bungeni huku chama hakija wateua, hii ni forgery, hili ni kosa la jinai, hivyo Chadema walipaswa wafanye a due diligence process to establish forgery.
  2. Walipaswa kuripoti uhalifu huu polisi ili uchunguzi wa kihalifu ufanyike, uchunguzi huo ndio ingeipa Chadema mamlaka ya kuiona barua ya uteuzi na kuthibitisha it's fake.
  3. Baada tuu ya uthibitisho wa kughushi, NEC ingetengua barua za uteuzi, Bunge lingewafuta ubunge ubunge wao.
  4. Hatua za kijinai kwa perpetrators zingeanza kwa kesi ya jinai ya Kughushi
  5. Chadema sasa ndipo kingeanza na hatua zao za kinidhamu ndani ya chama, kwa mujibu wa katiba ya Chadema.
Imekuzwa kwasasa ni 'landmark' . Maamuzi kama alivyoanisha JokaKuu utagundua Mahakama imeboronga.
Ni kweli Mahakama imeboronga big time.
Kwavile ni 'landmark' vyama vya siasa vinapaswa kuangalia katiba zao ili asije mtu kutumia hukumu dhidi yao.
Sio vyama vya siasa kuangalia katiba zao, ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kufanya mapitio ya katiba za vyama ziendane na katiba ya JMT.
Hilo ni kinyume na misingi ya uendeshaji wa vyama. Hatuwezi kuwa na mfumo mmoja unaoratibu Katiba za vyama.

Si kazi ya Jaji kueleza Katiba za vyama ziweje, ni kazi ya Jaji kutafsiri Katiba hizo kwa mujibu wa sheria.
true
Uwepo wa Wajumbe wa CC ya Chadema hata kama ulikuwa na influence katika maamuzi, Katiba haikukiukwa.
true
Lakini pia ' Professional judgement' ipo wapi.

Tayari alisharidhia CC ilitenda haki, je, Wajumbe wa CC katika baraza kuu waliathiri kura kivipi?
Na ikiwa Chadema itaitisha Baraza kuu na kuondoa Wajumbe wa CC hilo litabadili vipi matokeo?
true
Tuna tatizo kubwa katika mhimili wa sheria, Majaji wetu ni 'sub standard' . Pengine tunahitaji uongozi mpya, ule wa akina Nyalali, Samatta, Nassoro Mzavas, Kisanga, Lugakingira na watu kama akina Murtaza , Manning na Longway! n.k.

Sijui Mahakama inahitaji 'revamp au overhaul' sijui! ninachojua ipo compromised
Kwa hapa I reserve my comments for conflict of interest.
P
 
Wewe unafanya hiyo kazi under ccm instructions
Freedom to think, ndio the only absolute freedom, hivyo naomba niheshimu freedom yako hiyo kuwa mimi Pasco Mayalla nafanya kazi under CCM instructions.
kwahiyo watu wenye akili hawawezi kuwa kwenye vipindi vyako
I keep this in mind and proves you otherwise in due time.
kwani watawaumbua na propaganda zenu!!
Kipindi changu sio Kipindi cha propaganda
Hao wakina Lipumba, Cheyo na Wasira hao wote ni waganga njaa ; wapo hapo kwa maslahi yao binafsi na sio maslahi mapana ya wananchi!
Naomba niheshimu opinion yako.
P
 
Watanzania tunajuana ktk suala la Katiba Mpya, na Tume Huru ya Uchaguzi.

..Ungeniambia unataka kuwe na balance ktk maoni ya wageni unaowahoji ningekuelewa.

..Sio sahihi kutufanya wasomaji wako wajinga kwa kudai hujui mitizamo ya wageni unaotarajia kuwaalika.
Kipindi changu kinaendeshwa kwa haki, nikiita viongozi wa vyama, status ya mwenyekiti wa CCM is the same na mwenyekiti wa Chadema, CUF, NCCR, Tadea etc. Sibagui.
Wakati mwingine unajidhalilisha Pascal Mayalla kwa mambo unayoandika. Hata kama unatafuta maokoto usifanye kwa kuzidisha na kujidhalilisha.
Naomba niheshimu opinion yako on me.
P
 
Wanabodi

Mimi mwanabodi mwenzetu Paskali Mayalla, nimerudi hewani kupitia kipindi kipya cha TV kiitwacho "KMT" ( Kwa Maslahi ya Taifa), ambacho kinarushwa na Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, kila siku Jumapili saa 3:00 usiku na marudio kila siku za Jumatano Saa 9:30 jioni.


View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=5AQk8igiLzsUr0Ee

Jumapili hii, manguli wa Siasa hapa nchini, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mzee John Memosa Cheyo, " Mzee wa Mapesa", Mwanasiasa Mkongwe wa CCM toka enzi za Nyerere, Mzee Stephen Wasira, Mwanasiasa Kijana Machachari, na Kiongozi Mkuu, wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe, Dorothy Semu wa ACT Wazalendo, Mrajis Azasi Zanzibar, Ahmed Khalid Abdullah, na Profesa wa Siasa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Bernadeta Killian, kuunguruma kwenye Vox Pop, ya kipindi cha KMT cha leo on Channel Ten, kuzungumzia mustakabali wa siasa zetu kuelekea 2025


View: https://youtu.be/4xNWWz3kNLg?si=34IxqjI2gidc1Ul_


View: https://youtu.be/UR6qPKMfZXw?si=rcKwROx3mQ7lfB6V


View: https://youtu.be/RPpcwlnNJ0A?si=tl2ijqUepC2xhqfn


View: https://youtu.be/5kIid09GCqQ?si=g9-ypBQST35xYXOh


View: https://youtu.be/GviVxNkF0Zs?si=soyp0kMA6Wgfu45z


View: https://youtu.be/YN16dYs2QU8?si=FqsPdQH_b2kS53AX


View: https://youtu.be/NnLDbbLitfY?si=qYk-VKw2wd4Z79SU

Usikose!.

Paskali

Kwa waliokosa kipindi hiki, Kitarudiwa Jumatano saa 9:30 on Channel Ten,
Kwenye vipindi vinavyofuata, nimeongea na KM wa Chadema, JJ. Mnyika, NKM Chadema, Salum Mwalimu, na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Chadema. Juhudi za kumpata Mwenyekiti, Freeman Mbowe, zinaendelea. Siku ya siku pia nitawaletea Sugu, Lema, Heche na wengine!.
P
 
Back
Top Bottom