Mantiki ya kiingilio 7-7 ni nini?

Mantiki ya kiingilio 7-7 ni nini?

Inashangaza sana kuitwa Dar es Salaam International trade fair. Ukweli kinachofanyika hapo ni sawasawa na magulio mengi yanayofanyika sehemu mbali mbali hapa nchini, tofauti gulio hili linatoza kiingilio.

International trade fair yeyote ni kualika makampuni, mashirika ya serikali mbalimbali za nje kuja kuona bidhaa za viwandani, mazao mbali mbali kutoka mashambani, mifugo, samaki, madini nk. lakini maonyesho yetu yanaonyesha bidhaa za nchi nyingine na kutumia fursa hiyo kufanya mauzo ya bidhaa zao.

Tunataka bodi inayohudumia gulio hilo watuambie ni order au mikataba ya bidhaa zipi zinazozalishwa hapa nchini zilisainiwa na taifa litauza tani ngapi nje ya nchi na taifa litaingiza kiasi kadhaa cha fedha ya kigeni.

Lakini utashangaa uongozi wa gulio la saba-saba watajivuna mwaka huu wameingiza kiasi fulani cha fedha na kuvuka lengo walilojiwekea.
 
Kiingilo sio mbaya kuwepo cha msingi huduma ziboreshwe humo ndani ukiruhusu watu waingie bure itakuwa vurugu tupu!
 
Kila sehemu kiingilio
1. STENDI UBUNGO (Kiingilio),
2. PANTONI (Kiingilio),
3. DARAJA KIGAMBONI (kiingilio),
4. 7-7 (Kiingilio), 8-8 (kiingilio)
5. .......................
 
Kwa hiyo ulitaka vile vitu vinavyooneshwa vigawiwe bure kwa watanzania ili iwe maonesho ya biashara siyo? Kuna haja ya WaTZ tukaweka haya mambo ya UKAWA pembeni tuwe serious kwenye kutafuta.
Maonesho ni kuonyesha kitu kisha kikaachwa hapo ya kutambulisha shughuli zako yaani siuzi wala kukupa bure Hapo ukawa umekujaje basi kama hakuna kitu cha bure isipokua umeripia kama si leo basi kesho
 
Kila sehemu kiingilio
1. STENDI UBUNGO (Kiingilio),
2. PANTONI (Kiingilio),
3. DARAJA KIGAMBONI (kiingilio),
4. 7-7 (Kiingilio), 8-8 (kiingilio)
5. .......................
Viingilio na kutoa gawio kwa mashirika ya Umma Ni model ya wapi hii?
 
Kwa ajili ya kulimit watu maana wakiweka bure nadhani target market wasingeweza kuingia,na kiingilio tu kunakuwa na watu kama wote.
 
Ku-limit watu?

Yes ukiweka bure hapatatosha ndani...watu watajaza mpaka pa kukanyaga kutakuwa hakuna....halafu wale wenye kwenda kujifunza na kununua vitu hawataingia ,wataenda wale wazee wa kitonga/sadala kwa ajili ya kwenda kuangalia wanyama tu na hawana hata mia ya kununua vitu.

Kwahiyo watu waenye fedha wakiona shazi kubwa hawatoingia......lakini ukiweka kiingilio utawaondoa hao wazee wa kitonga na kuwapata wenye nia ya dhati ya kuingia 77.
 
Yes ukiweka bure hapatatosha ndani...watu watajaza mpaka pa kukanyaga kutakuwa hakuna....halafu wale wenye kwenda kujifunza na kununua vitu hawataingia ,wataenda wale wazee wa kitonga/sadala kwa ajili ya kwenda kuangalia wanyama tu na hawana hata mia ya kununua vitu.

Kwahiyo watu waenye fedha wakiona shazi kubwa hawatoingia......lakini ukiweka kiingilio utawaondoa hao wazee wa kitonga na kuwapata wenye nia ya dhati ya kuingia 77.
Swali langu lilikua dogo tu. Jiwe yupo wapi? Pia, Dubai Expo 2021 Wana kiingilio?
 
kwenda sabasaba kulipa kiingilio wakati bidhaa umeziacha mtaani ni upuuzi mtupu hii haina tofauti na wanaokwenda kwa manabii feki kupeleka sadaka, nunua vitu vyako mtaani acahana na tantrade
 
WAKATI MAONYESHO YA 7-7 YAKIENDELEA UWANJA WA MWL. NYERERE KILWA ROAD NAJIULIZA HIVI IWEJE TANTRADE WAWEKE VIINGILIO KWA ANAEINGIA HUMO UWANJANI?

WAKATI HAKUNA HUDUMA YOYOTE (mfano vyoo, maji nk) wanayotoa kwa waonyeshaji au wanunuzi? je hawaoni kuweka kiingilio kunafanya watu wengi kutotembelea maonyesho hayo? hivyo wafanyabiashara kuzidi kukosa wateja?
Bongo raha
 
Back
Top Bottom