Manyara: Ahukumiwa kifo baada ya kunyonga mkewe na mtoto baada ya mkewe kumkatalia kuongeza mke wa pili

Manyara: Ahukumiwa kifo baada ya kunyonga mkewe na mtoto baada ya mkewe kumkatalia kuongeza mke wa pili

TheCrocodile

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2021
Posts
1,199
Reaction score
3,307
Mahakama ya Kuu ya Tanzania Kanda ya Manyara imemhukumu Shamsudini John maarufu SIKUKUU mwenye miaka 35 kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kuwauwa kwa kukusudia kwa kuwanyonga kwa kanga mkewe Asia John aliyekuwa na umri wa miaka 25 na mtoto wake Ahmed Shamsudini aliyekuwa na miaka Tisa (9) baada ya mke wake kumkatalia kuongeza mke wa pili.

Hukumu hiyi namba 13 ya mwaka 2020 imetolewa leo Disemba 07 kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Manyara na Jaji Devota Kamzola ambapo ameieleza mahakama kwamba mshtakiwa alitekeleza mauaji yao kwa kukusudia.

Awali Jaji Devota aliieleza mahakama kwamba mshatakiwa huyu Shamsudini John alikuwa na ugomvi na mkewe Asia John baada ya kutaka kuoa mke wa pili ndipo marehemu mkewe alikataa jambo hilo na kupelekea mumewe kufanya mauaji hayo katika Kijiji cha Hidet wilayani Hanang mkoani Manyara.

Jaji Devota aliendelea kwa kusema, mshtakiwa Shamsudini alitekeleza mauaji hayo kando ya Bwawa la Hidet wilayani Hanang umbali wa zaidi ya kilo mita moja kutoka kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi na kwamba mshtakiwa alianza kumnyonga mkewe Asia kwa kutumia kanga, huku mtoto wao Ahmed Shamsudini akipiga kelele baada ya kuona mama yake ananyongwa na kisha kunyonga na mtoto wao na kumtupa kwenye bwawa hilo, kabla ya kumtoa na kisha kuondoka na mwili wa mkewe hadi nyumba.

Imeelezwa kuwa mshtakiwa alipofika nyumbani alianza kuchimba shimo kwa minajili ya kuuzika mwili wa marehemu Asia, kabla ya mke mdogo kumuona na kumuhoji mshtakiwa ambaye alijibu anachimba shimo la taka na kuuzika jirani na nyumba waliyoishi.

Imeelezwa mahakamani hapo kwamba mshatakiwa alikana kuhusika na vifo hivyo na kueleza kwamba mke wake na mtoto walikufa maji, huku shahidi namba tatu ambaye ni daktari alithibitisha vifo hivyo vilisababishwa na kukosa hewa na siyo kufa kwa maji kama alivyojitetea mshtakiwa lakini baadaye Shamsudini alikiri kutenda matukio hayo na kuwapeleka polisi mahali alipouzika mwili wa mke wake na ulipo mwili wa mtoto kando ya bwawa.

Mshtakiwa amekutwa na hatia kinyume na vifungu vya Kanuni ya 196 na 197 vya kanuni ya adhabu Sura namba 16 Toleo mwaka 2002.

My take: Jamaa anastahili adhabu zaidi ya kunyongwa kwa kitendo hiki cha kikatili kabisa, ingefaa afungwe jiwe zito shingoni kisha atupwe mto Kagera akawe chakula cha mamba.
 

Attachments

  • FB_IMG_1670423522307.jpg
    FB_IMG_1670423522307.jpg
    90.2 KB · Views: 16
Itakuwa jamaa alikuwa ana magonjwa ya akili sio kawaida

Bora uoe au uolewe na malaya, atacheat ila jion atarudi, watoto watakula, watasoma, watalala.

Ila ukiolewa na mgonjwa wa akili yani mentally unstable atafanya jambo la hatari mda wowote ndio hao wakupiga risasi wake zao

Na ukioa mgonjwa wa akili anaweza wafanya watoto wako kama mawe, unakuta mwanamke anampiga mwanae kama anampiga mnyama au mti kumbe kamzaa mwenyew

Kwenye uchumba tu ukiona tu dalili zozote za uchizi chizi, hasira za kijinga, sheria za kipumbavu, mipaka isiyo namantiki, bora umwepuke mapema.

Sheria ifuate mkondo wake.
 
Itakuwa jamaa alikuwa ana magonjwa ya akili sio kawaida

Bora uoe au uolewe na malaya, atacheat ila jion atarudi, watoto watakula, watasoma, watalala.

Ila ukiolewa na mgonjwa wa akili yani mentally unstable atafanya jambo la hatari mda wowote ndio hao wakupiga risasi wake zao

Na ukioa mgonjwa wa akili anaweza wafanya watoto wako kama mawe, unakuta mwanamke anampiga mwanae kama anampiga mnyama au mti kumbe kamzaa mwenyew

Kwenye uchumba tu ukiona tu dalili zozote za uchizi chizi, hasira za kijinga, sheria za kipumbavu, mipaka isiyo namantiki, bora umwepuke mapema.

Sheria ifuate mkondo wake.
Ni kweli aisee, inawezekana jamaa ana shida kiakili.
 
Sasa anaenda kuolewa yeye na manyapara
 
Hiyo Dini ndo inaruhusu umnyonge, Dini inasema ishi nae Kwa wema, ikitokea kuachana muache Kwa wema....Kama alipata inayofinyia Kwa ndani huko nje angempa talaka zake tu, sio kumtanguliza kaburini.
Hakufata mafundisho ya Dini.
 
Hiyo Dini ndo inaruhusu umnyonge, Dini inasema ishi nae Kwa wema, ikitokea kuachana muache Kwa wema....Kama alipata inayofinyia Kwa ndani huko nje angempa talaka zake tu, sio kumtanguliza kaburini.
Hakufata mafundisho ya Dini.
Ni kweli uko sahihi.
Lakini pia, mke hakua sahihi kumkatalia kuongeza mke, japokua kama ulivyosema hatua aliyochukua jamaa ni sio sahihi pia hata kidogo. Angempa talaka tuu.
 
Back
Top Bottom