Manyara: Basi la Mohammed Classic lapata ajali na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi 26

Manyara: Basi la Mohammed Classic lapata ajali na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi 26

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Basi kampuni ya Mohammed Classic ya kutoka Arusha-Kigoma imepata ajali Eneo la Gehandu Hanang mkoani Manyara.

==============================

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Benjamin Kuzaga amesema: "Ajali hiyo imetokea imetokea Kijiji cha Ming’enji Wilaya ya Hanang katika Barabara ya Babati, ajali imehusisha gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T380 DWF lililokuwa likitoka Tabora kwenda Moshi limegongana uso kwa uso na Basi la Mohammed Classic.

“Basi hilo lilikuwa likifanya safari zake kutoka Arusha kwenda Kigoma, katika ajali hiyo waliopoteza maisha ni dereva wa Fuso jina Amir Haruna pamoja na msaidizi wake ambaye jina halijajulikana.

“Wengine waliofariki ni ni msaidizi wa dereva wa basi aliyefahamika kwa jina moja la Omari na utingo wake.

“Chanzo cha ajali ni dereva wa basi kutozingatia alama za barabarani, kwani eneo la tukio kuna ujenzi wa barabara unaendelea, kuna alama ambazo hakuzizingatia, badala yake akajikuta alivaa gari hilo aina ya Fuso.

“Kuna majeruhi 26, kati yao wanaume ni 14, wanawake 10 na watoto wawili, wote wamefikisha hospitali kwa ajili ya matibabu, lakini wanaendelea vizuri.

“Natoa wito kwa madereva wote wa vyombo vya moto kuzingatia alama za barabarani kwani zina maana yake, kufanya uzembe kama huyo unakuwa unasababisha madhara makubwa.”

Mohammed.JPG
Mohammed 2.jpg

PICHA: Hawa na BobDere Omari Marangi
 
Watu hua wanadai ngono imekua rahisi wanasahau kifo kimekua rahisi tangu Adam na Hawa walipokubaliana kuzini
 
RIP kwao. [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Imesababisha "Vifo vya Konda na Dereva", hata Fuso si lina Dereva?.
 
Roho za marehemu zipumzike salama.

Ukitoka kwako na kurudi salama ni jambo kumshukuru mungu
Ni muujiza ambao hata wewe mwenyewe huhitaji kumshukuru Mungu kwa sababu shukrani zako haziwezi kulingana hata na chembe ya kile ambacho Mungu amekufanyia. Badala ya kumshukuru Mungu, unatakiwa umuombe Roho Mtakatifu akusaidie kutoa shukrani zilizo sahihi kwa Mungu. Usimshukuru Mungu wewe, mwambie Roho Mtakatifu akusaidie kutoa hizo shukrani
 
Basi kampuni ya Mohammed Classic ya kutoka Arusha-Kigoma imepata ajali Eneo la Gehandu Hanang mkoani Manyara.

==============================

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Benjamin Kuzaga amesema: "Nipo eneo la tukio, ni kweli ajali imetokea maeneo ya Hanang katika Barabara ya Babati, ajali imehusisha gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T380 DWF lililokuwa likitoka Singida kwenda Moshi.

"Dereva bado hatujamfahamu, tunaendelea kukagua mifukoni kwa kuangalia leseni au kitambulisho kingine chochote, baadaye nitatoa taarifa kamili ya tukio hili."

View attachment 2236678View attachment 2236677
PICHA: Hawa na BobDere Omari Marangi
Sasa kamanda anasema Babati wewe unatuambia mbulu???!
 
Back
Top Bottom