Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wakati yamebaki masaa kabla ya kukoma kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura katika daftari la makazi kufikia ukomo leo Oktoba 20, Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga tarehe 19.10.2024 alitembelea jamii ya Wahadzabe katika kijiji cha MONGO-WA-MONO wilayani Mbulu ambao maisha yao bado yanategemea uwindaji na kuokota matunda na asali ambapo amewahimiza kujiandikisha katika daftari la makazi ili waweze kuchagua viongozi wao katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.
Soma Pia: Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu aamua kutembelea ofisi mbalimbali kuhamasisha Watu wakajiandikishe katika Daftari la Kupiga Kura
Sendiga alifika katika kijiji hicho kilichopo kata ya Yaenda Chini wilayani Mbulu akiwa na zawadi ya kitoweo cha nyama ya nyumbu ili kushawishi jamii hiyo kuwa na utulivu wa muda kujiandikisha katika daftari la makazi kabla ya zoezi hilo kufikia ukomo Oktoba 20 ili waweze kushiriki katika katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Pia amewata kushiriki kuwachagua viongozi wa jamii yao wenye uwezo wa kuwaongoza kuharakisha juhudi za maendeleo katika eneo lao wakati wa uchaguzi huo.
Wakizungumza kwa niaba ya wenzao baada ya kupokea zawadi hiyo na ujumbe wa kujiandikisha, Salum Joseph Duduqwe na Zuberi Mathayo wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwathamini kwa kuwatembelea, ambapo wamemweleza kuwa asilimia kubwa tayari wameshajiandikisha na wameahidi kuendelea kuwashawishi wengine ambao bado wakajiandikishe kabla ya zoezi hilo kufikia ukomo.
Soma Pia: Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu aamua kutembelea ofisi mbalimbali kuhamasisha Watu wakajiandikishe katika Daftari la Kupiga Kura
Sendiga alifika katika kijiji hicho kilichopo kata ya Yaenda Chini wilayani Mbulu akiwa na zawadi ya kitoweo cha nyama ya nyumbu ili kushawishi jamii hiyo kuwa na utulivu wa muda kujiandikisha katika daftari la makazi kabla ya zoezi hilo kufikia ukomo Oktoba 20 ili waweze kushiriki katika katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Pia amewata kushiriki kuwachagua viongozi wa jamii yao wenye uwezo wa kuwaongoza kuharakisha juhudi za maendeleo katika eneo lao wakati wa uchaguzi huo.
Wakizungumza kwa niaba ya wenzao baada ya kupokea zawadi hiyo na ujumbe wa kujiandikisha, Salum Joseph Duduqwe na Zuberi Mathayo wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwathamini kwa kuwatembelea, ambapo wamemweleza kuwa asilimia kubwa tayari wameshajiandikisha na wameahidi kuendelea kuwashawishi wengine ambao bado wakajiandikishe kabla ya zoezi hilo kufikia ukomo.
