Hayo mambo ya mungu ni hadithi za kusadikika ! Angekuwepo kweli asingekaa kimya mpaka Leo, hajawahi kutuonyesha hata kwa dalili alipo Ben saanane! Angekuwepo na kama angekuwa anasikia maombi yetu mwanetu Paul mwangosi asingekufa kinyama namna ile na mungu akawa anaona tu ! Kama angekuwepo waliomteka na kumpoteza mwandishi wa mwananchi ndugu azory gwanda huko kibiti mungu asingewaacha bila kuwaumbu na ikabaki Siri mpaka Leo ! Nasema hivi ni habari za kusadikika kumhusu mungu !angekuwepo Watu maelfu wasingetupwa na kuokotwa kwenye mifuko ya sandarusi baharini , mungu asingenyamaza angeshuka kutuonyesha ukuu wake na angetoa hukumu Kila mtu angeona ! Nahisi labda mungu anaesimuliwa kwenye hivi vitabu alikuwa mungu wa enzi zile za akina ibrahimu na akina Musa na isaka ,ama Joshua eliya na Gideon ,huenda aliyepo sasa sio yule Jehova ! Kwa nini huyu hatoi majibu !? Kwa nini huyu anakaa kimya hata watu wake wanapoonewa ? Angalia sasa juzi watu wameenda kumwabudu yeye huko saudia maelfu wamekufa na kuacha watoto yatima na wake zao wajane ! Mungu wa akina ibrahimu asingekubali maafa ya aina hii ! Ona mji Rafah yamebaki magofu lakini mungu yupo kimya ! Tuziamini nguvu zetu huenda tukifa ndio mwisho wetu !