Maombolezo ya Kawawa na Rais Mpirani

..Raisi hakitakiwa kwenda uwanja wa taifa.

..yaani hata mechi za kirafiki Raisi hataki kukosa?!!
 
Alipofariki mgombea mwenza wa CHADEMA ilibidi hata yeye mwenyewe Kikwete aache kufanya kampeini za uchaguzi kwa siku tatu; na wala kampeini zile hazikuwa burudani kama ilivyo huu mpira. Inakuwaje leo anashindwa kutoa heshima kwa marehemu Kawawa namna ile?
 
- Mechi ya kimataifa ilikuwa imeshapangwa, sasa kama kweli tuko serious na maombolezo basi tatizo liwe kwa nini as a nation tuliruhusu mechi kuwepo, unless kama hiyo responsibility inamuanguklia Rais,

- Otherwise, Rais asingekwenda kwenye huu mchezo wa timu ya taifa, as per who and what? hapo tu ndipo ninapokwazika unless kuna something hakijasemwa hapa, na sitaki kulinganisha na nchi zingine kwa sababu sio kila wanayofanya wengine isipokuwa sisi tu ni mazuri,

- Bado sielewi kulikuwa na tatizo gani Rais kwenda mpirani, somebody needs to explain nini maana ya nchi yetu kuwa kwenye maombolezo, na je walipofariki Mwalimu na Sokoine kuna mechi zozote za kitaifa zilizokuwa postponed au anything esle, kuliko kujadili bila muongozo kama tunavyofanya hapa so far! Au kuna kifungu cha katiba ya jamhuri yetu kinagusia haya ya maombolezo ya taifa iwekeni hapa wakuu! ili tujadili na facts, au?

- Lakini so far binafsi ninaridhika sana na heshima zote alizopewa Kawawa na taifa hili kwamba kwa hilo Rais amejitahidi sana kwenye ukweli huwa tunakubali kama hili.

Respect.


FMEs!
 
FMES,

..yaani bendera mpaka ya Raisi inapepea nusu mlingoti, halafu unashangaa kwanini wananchi tunamlaumu Raisi kwa kuhudhuria mechi ya mpira ya kirafiki?

..kuna uwezekano mkubwa hiyo mechi ilishapangwa na haingewezekana kuiahirisha. that was already enough compromise kwa upande wa Watanzania na serikali. sasa hili suala la Raisi kwenda mpirani kwa kweli amevuka mpaka.
 


- Mkuu please bendera kupepea hata robo mlingoti ni matakwa ya nani sheria ya jamhuri au ni kawaida na mazoea tu? Rais si anakuwa Rais 24/7 au kwenye maombolezo ya taifa anakuwa off duty?

- For once can we talk facts za hii ishu?

Respect.


FMEs!
 
FMES,

..naamini kipo kifungu kinachoelekeza kuhusu masuala ya taifa kuwa ktk kipindi cha maombolezo.

..yeye mwenyewe Raisi alilitangazia taifa kwamba tutakuwa ktk siku 7 za maombolezo. tumeona bendera ya taifa ktk msiba wa Mzee wetu Rashidi Kawawa ikipepea nusu mlingoti. kama bendera ya taifa inapepea nusu mlingoti basi hata ya Raisi na zile za majeshi zinapaswa kupepea nusu mlingoti.

..kitendo cha Raisi kuhudhuria mechi ile hakishabihiani na mwenendo wa Raisi ambaye taifa lake lipo ktk maombolezo na bendera ya taifa na ile ya raisi zikiwa nusu mlingoti.

..lakini hata kama suala hilo halipo ktk sheria zetu, nadhani HESHIMA, UTU, na UUNGWANA, vilitosha kumuelekeza Raisi kwamba hakupaswa kuwepo ktk mechi ile ya kirafiki ya mpira.
 

...mambo mengine,haya hitaji katiba inasema nini bali busara zaidi.
Nyerere aliwahi kusema kuwa katiba ya Tz inampa uhuru RAIS Kuwa DICTATOR,LAKINI HAKUNA RAIS WA TZ UNAYEWEZA KUSEMA KWA UHAKIKA ALIKUWA DIKTETA.HII MAANA YAKE NI KWAMBA
WALIKUWA WANATUMIA BUSARA ZAO.
Kwa hili la JK ni kwamba amekosa busara au "amebusarika vibaya".
TFF wamefanya kazi yao na kwa kukumbuka kuwa Taifa lipo kwenye Msiba Mkubwa,walisimama kwa dk moja pale uwanjani.NINAAMINI hawakusimama kwa sababu JK alikuwa uwanjani bali kwa sababu RAIS ALISHATANGAZA MAOMBOLEZO.
Hivi ukiaga kwa mkeo na watoto kwamba unaenda hosp kwa sababu unaumwa halafu ukarudi jioni umelewa.Familia itakuelewaje?
 

Inategemeana na culture,kwa waislam maombolezo ni siku tatu bila burudani yoyote....Kama Taifa,Mh Rais alitangaza siku saba za maombolezo kama sijakosea.
Tafsiri halisi ya kuomboleza ni pamoja na mengineyo;kutoshiriki kwenye shughuli yoyote ile ya burudani.
Nakuachia uamuzi uwe wako kama kwenda kwenye mechi ni sehemu ya burudani ama la.
 

- As per who? Rais anayefuata baada ya Mkapa lazima atoke visiwani, Mkapa aliuliza as per who? Hakukuwa na majibu, sasa here we are again! tunazunguka pale pale kila siku!

Respect.


FMEs!
 

- Ya kuongozwa kwa busara ndiyo yametufikisha hapa tulipo as taifa, sasa it is about time tukajaribu kuongozana kwa kutumia sheria wakuu, maana sasa hizi busara unazozisema sina tofauti gani na zile za Spika zilizogharimu Sillingi Millioni 100?

- Maombolezo ya taifa hayajawahi kumfanya Rais akawa off duty kuelewa hili ni common sense tu!

Respect.

FMEs!
 
- As per who? Rais anayefuata baada ya Mkapa lazima atoke visiwani, Mkapa aliuliza as per who? Hakukuwa na majibu, sasa here we are again! tunazunguka pale pale kila siku!

Respect.

FMEs!

Ebu tueleze "As per you" maana si umesema huelewi ni yapi ya kufanya na kutofanya wakati wa maombolezo?
Hii tafsiri ya wikipedia,sina muda wa ku reasearch zaidi kwa sasa hii itatosha...Haitatosha kama mechi si social event.
 

- Labda kama hicho kifungu kingepatikana kikawekwa hapa, otherwise ni ishu ya kila mtu kuangalia katika angle yake, lakini sio kuangalia in a uniformity angle, maana hili taifa wengine hawana hata dini, na wengine hupiga muziki mzito sana siku ya msiba, wakuu tuwe considerate sometimes tupunguze ubinafsi!

Respect.


FMEs!
 
Ebu tueleze "As per you" maana si umesema huelewi ni yapi ya kufanya na kutofanya wakati wa maombolezo?
Hii tafsiri ya wikipedia,sina muda wa ku reasearch zaidi kwa sasa hii itatosha...Haitatosha kama mechi si social event.

- Mushi acha kunivunja mbavu bro, sasa toka lini Tanzania tumeanza kuongozwa na wikipedia?

- Anyways naomba kutoka huu mjadala maana sioni facts, zaidi ya kwa kawaida!

Respect.


FMEs!
 
Unajua mkubwa hii debate kwangu inatokana na mlolongo wa mambo mengi ambayo yanafanyika, yanayoashiria dharau kwa mambo muhimu na kuyapa kipaumbele mambo yasiyo na mitazamo ya kitaifa. Kwa mfano, sioni ubaya wa Rais kupumzika Jamaica kama mambo ya msingi aliyoyaacha nyuma yangekuwa yanapatiwa suluhu.Sasa huku wabunge wanashikana makoo kwenye tume ya Mwinyi, unatoka Egypty unaangalia hali ya uwanja unagundua umejaa maji...taratibu unaondoka halafu tunapokuwa na hamu ya kuona action, tunakuona unabembea!Come on kwanini watu wasiwe wakali.
Unfortunately what we do define who we are!!Kama matendo ya aina hiyo yanakuwa mengi, basi hakuna utakalosema ukaonekana unajua unasema nini.Unawapa watu nafasi ya kukunyima hata kupumua maana hawajui uko serious na nini. Tafakari bro!!
 

Dark City alisema hivi hapo chini.....
Dark City said:
Kwa maoni yangu Rais wetu hakutakiwa kuwepo uwanjani kama ambavyo asingeweza kuandaa dhifa ya kitaifa kwa Kiongozi yeyote ambaye angemtembelea Ikulu.
Kama ni kweli Kiongozi yeyote ambaye angemtembelea Ikulu asingeweza kuandaliwa dhifa ya kitaifa,then hayo mambo ya kuwa off duty yametoka wapi tena?Ama ni utumwa wa kibepari kwasababu ya hizo bilioni saba ndizo zinakosesha watu "utu?"
Ni wazi kuwa hiyo ni issue ya ki protokali,unaposema naomboleza halafu ukaja na kudai hujui maana ya kuomboleza then nani alaumiwe?
 
eti nini? imetumika bilioni 7 kwa maandalizi ya hiyo mechi tu? bora hata wangejenga nyumba saba kama za gavana,kilio tungelia, lakini afadhali nyumba zingekuwepo, sasa kama haitakuja timu kuweka kambi kwetu ndiyo itakuwa zimekula kwetu hizo, hivi katika hawa walioizinisha hakuna wasiopenda soka. rais anajuwa sana kwamba kwenda pale ni makosa wakati tuko kwenye maombolezo ya siku 7, imebidi aende kutokana na uchaguzi ujao,hao asilimia 70% anaowasema itabidi aje awaambie kwamba na yeye alikuwepo hili wamchague.
 
- Mushi acha kunivunja mbavu bro, sasa toka lini Tanzania tumeanza kuongozwa na wikipedia?

- Anyways naomba kutoka huu mjadala maana sioni facts, zaidi ya kwa kawaida!

Respect.

FMEs!

Nilikuwa natoa msaada kwasababu hujatatizwa na Rais kwenda mpirani kwenye kipindi cha maombolezo ya kitaifa,ni sawa na kusema hujui maana ya maombolezo,sasa nimekupatia tafsiri ya maombolezo halafu wewe umetafsiri kuwa maombolezo ni "muongozo wa nchi" a Tanzania,huu ni "Uhuni" huna haja ya kutoka kwenye mjadala,mbona kuna mijadala mingi tu hutoki?
Sina nia ya kukupangia kubaki kwenye mjadala huu,lakini hoja kwa hoja,na ukiwa right kihoja basi uko right,na ukiwa wrong si lazima ukimbie na kutoa sababu ambazo hazipo,ku imply kwamba nimesema nchi inaongozwa na wikipedia na kwamba hiyo ndiyo sababu ya wewe kundoka kwenye mjadala huu ni madharau na "Uhuni"
 
- Baada ya kusoma mengi hapo juu inaonekana hii ya kilio cha Rais kwenda mpirani inachukuliwa kama sababu ya hasira ya mengine kama Billioni saba, bembea za Jamaica na the rest,

- Binafsi ninajali sheria, na sio siri kwamba Rais hakukiuka sheria yoyote ya jamhuri kwenda kwenye huu mpira, unless kuna something else anyways I am out maana ni more hisia kuliko facts on the ishu!

Respect.

FMEs!
 

Kama hairuhusiwi kuandaa dhifa ya kitaifa hata kama tumetembelewa na kiongozi mkuu wa nchi nyingine,vipi kuhusu Drogba?
Chief of protocal should be fired.
 
Hii sasa imezidi !! Nyie mbona mlikwenda mpirani na wewe nanihii ulibaki home umekodoa mimacho kwenye luninga yako utadhani chatu anataka kummeza dogi. Acheni mambo mengine bwana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…