Hao wa kimataifa watakuja kumuonyesha nani bidhaa zao wakati wanajua wafanyabiashara wa ndani wanaogopa kufanya uwekezaji kwa hofu ya kukamatwaNi kweli mkuu, huwa wanakuja kuuza bidhaa zao sio maonyesho, mwaka huu itakuwa maonyesho ya kweli na kutoa bidhaa za bure za promosheni
Mbona pale mlimani city na rock city mail huwa tunaingia bureee na kuna hadhi kuliko huko sabasaba, tena na uchumi wenyewe huu siji kabisaM
Maonesho kama neno linavyomaanisha ni watu waingie kuona, watapata taarifa za bidhaa... ubora, bei, matumizi, faida nk... biashara itaanza pale na hasa baadae... pale ni matangazo ya bidhaa... hali itakapokuwa nzuri bidhaa zitauzika tuu... sio lazima pale.... Sabasaba sio mtaa wa Kongo au Karume...
Ni hivi , ukilipa elfu 1 unapewa bia 3 na fulana 1Mkuu dadavua hii vizuri haujasomeka ?
Nenda ofisi za BETNaomba kujua taratibu za kupata mabanda uko sabasaba
Vibaka wote wanahamia hapo , polisi baada ya kujinyakulia rushwa mlangoni wakati wa mchana , huelekea banda la Kizota kula Kitimoto .Nilikuwa na moto wa kwenda Sabasaba baada ya kuondoka nchini kwa miaka mingi.
Nilivyorudi nilikuwa disappointed.
Nilikuta Sabasaba pameachwa bila matengenezo miaka mingi, vyoo vinanuka kiasi cha kuweza kusababisha magonjwa, kilichonisikitisha zaidi, mabanda mengi yakikuea yanafungwa saa 12. Nikauliza kwa nini? Wakasema wanaogopa wizi usiku.
Nikaona kuna sababu nyingi uchumi wetu unakuwa na matatizo mengi.
Uko sahihi mkuu.Kwa kuzingatia uzoefu maonesho ya aina ile na maudhui Yake ni kuwa ilipaswa Watu wawe wanaingia bure ili mradi kunakuwa na umakini mkubwa ktk kuzingatia ulinzi na usalama Kwa ujumla wake ndivyo nchi nyingine kufanya, sasa haya ya hapa kwetu sijui Kwa nini wanataka Watu waingie Kwa kulipia ? Yani kwenda kuona bidhaa au huduma zinazozalishwa au kuuzwa na Watu au makampuni Mimi mwananchi nilipie? [emoji87][emoji87][emoji87] yani ni Kwa mfano Mtu anataka kuingia Kwenye Mall au supermarket halafu Kabla ya kuingia aambiwe lipa kwanza kiingilio kwa pesa ndo ukafanye window shopping au ukanunue unachotaka, je hiyo inaingia akilini? Binafsi naona siyo Sawa hata kidogo! Mwenye hoja tofauti aseme!
Weeeh!Nimepakana nalo , sitaji upande nilipo kwa sababu zinazofahamika , leo wanamalizia kupaka rangi .
Kuna kipindi miaka ya tisini nilikuwa naingia Sabasaba baada ya kutoka kazini. Nimeulamba, simu kwenye mkanda.Vibaka wote wanahamia hapo , polisi baada ya kujinyakulia rushwa mlangoni wakati wa mchana , huelekea banda la Kizota kula Kitimoto .
Dhihaka nyingine hata hazina maana.Tulieni serikali sikivu inafuatilia malipo ya makinikia, kila mtu anaweza kupewa mgao wake🙄
Hapana, hii ni namna ya kuchuja vibaka, wavuta bangi, wakabaji na watu wengine wa aina hiyo.
Asante kwa faraja zako .Acheni kukata tamaa kiasi hicho?????
Hv hua ni Maonesho au Maonyesho pls leo niwekeni sawa.Yanaitwa Maonesho ya biashara , lakini ukweli ni kwamba pamoja na bidhaa kadhaa kuonyeshwa , Wafanyabiashara tumetumia nafasi hiyo kuuza , tena kwa mauzo ambayo huvunja rekodi .
Sasa kutokana na kwamba almost 85% ya wateja wetu ni hawa wananchi wa kawaida ambao wamepigika vibaya sana kiasi cha kushindwa hata kumudu milo mitatu , basi tutegemee maumivu.
Sababu za kupigika kwa wananchi wa Tanzania zinafahamika .
Nachukua nafasi hii kuwatahadharisha wafanyabiashara wenzangu kwamba MAONESHO YA MWAKA HUU NI MAONESHO KWELI , NA WALA SI MAUZO TENA KAMA MLIVYOZOEA
Napendekeza pawe na kiingilio cha kuingia kkoHiyo haipaswi kuwa njia pekee ya kuchuja vibala, wezi na wavuta bangi, njia nzuri Ni kuimarisha ulinzi Na usalama tu that is the best practice na kuwapa wananchi mzigo wa kulipa viingilio ! Mbona Kariakoo Watu huenda bila viingilio? Mbona Kwenye ma malls Na super market Watu huingia bila viingilio? Kwa hiyo hoja yako haina mashiko!
Ngoja tumwite kifimbo cheza Faiza Foxy .Hv hua ni Maonesho au Maonyesho pls leo niwekeni sawa.