Tuongee ukweli WALIMU WALIOCHINI YA HALMASHAURI WATAENDESHWA MPAKA MWISHO WA DUNIA.

#YNWA
Nafikir kwa kiasi kikubwa kama kwa 100%, walimu wako ya usimamizi wa halmashauri.
Ni kweli lakini siku hizi mambo yanabadilika. Kuna halmashuri mojawapo ya mkoa wa Pwani, viongozi wa idara ya elimu hawana hamu na walimu kwa walichofanyiwa kiasi kupelekea kuanzia mkurugenzi kuhamishwa
 
Ualimu ni kazi fulani hivi ya hovyo kichizi yaani, ukiwa mwalimu kila mtu ni bosi wako mwanakijiji, mwenyekiti wa kamati ya shule, mwenyekiti wa Kijiji, diwani, mwenyekiti wa ccm, wajumbe wa kamati ya shule, mwalimu mkuu, mwalimu wa taaluma, mwenyekiti wa kitongoji, afisa elimu kata, mtendaji wa Kijiji, mtendaji wa kata, diwani, wachungaji na masheikh, afisa elimu wilaya...n.k

Tena usiombe uwe mwalimu wa vijijini ndo balaa kubwa
 
Katika jambo nalowaambia watumishi walioajiriwa na certificate na diploma ya ualimu ni kwamba "Ualimu sio ajira ni pakutafutia cheki namba, nenda kasome course nyengine chuo"

#YNWA
 
Ila mwanangu kazi ya ualimu unaipenda sana maana nikikumbuka zile hustle zako kule lindi mpaka ukamtafuna mtoto wa mwalimu mwenzio nakuonea huruma sana. Ila kaza moyo mzee.
 
Nimependa uwasilishaji wako leo, umewasilisha bila kuweka kejeli/matusi.

Alichoandika ni kweli 120% sahihi, kwa kweli kwa tulioingia kwenye kichaka hiki inabidi tufanye juhudi tutoke tukafanye kazi zingine hata kama hazihitaji elimu ya shuleni

Watu ambao hawajaingia kwenye mtego huu (hasa wanaotarajia kuingia mavyuoni) wasijaribu kuingia kwenye hii fani.

Kwa kweli ualimu sio kazi yenye future hata kidogo

Naomba kuwasilisha
 
Kibaya zaidi hadi wanafunzi wanapewa ukubwa wasiostahili,
Angalia lile tangazo la haki elimu, wanafunzi wanapewa airtime eti washiriki kwenye vikao vya bodi

Sasa mtu amesoma hadi university halafu akae na mtoto wa form one au four kwenye kikao cha bodi si upumbavu huo

Maana yake walimu pamoja na kusoma hawaaminiki

Mbona vikao vya madaktari hawakai na wagonjwa?

Polisi mbona hawakai na wafungwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…