Maoni na mapendekezo kwa tume/kamati ya kuangalia mfumo wa haki jinai

Maoni na mapendekezo kwa tume/kamati ya kuangalia mfumo wa haki jinai

Midimay

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2015
Posts
3,036
Reaction score
5,039
Habari za jioni mabibi na mabwana.

Ni maoni kwamba nia hii njema ya RJMT ipate muda wa kutosha katika mitandao ya kijamii na media kuu za nchi yetu.

Ikiwezekana hata na media za kimataifa kama BBC Swahili, BBC Focus on Africa, VOA Swahili, DW Kiswahili na za kikanda kama media za nchi jirani ya Kenya.

Mimi nina maoni yafuatayo kwa Tume hii, naaminini itawafikia.

1. Wakuu wa vyombo vyote vya utoaji wa haki jinai wawe na security of tenure kama ilivyo kwa CAG na Jaji Mkuu.

Kanuni hii itapunguza influence ya Wanasiasa wakuu katika utendaji wa kila siku wa vyombo hivi.

2. Bajeti na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya uendeshaji utajwe na sheria au kuwe na mfuko maalum kwa kila chombo. Iwe kama au bora kuliko ilivyo mfuko wa mahakama. Lengo ni lile lile la kuiongezea chombo cha haki kujiamini dhidi ya maamuzi ya wanasiasa.

3. Wakuu wa vyombo hivi wapatikane kwa mchakato wa wazi na kiushindani utakaobuniwa na sheria na sio kwa bin vuu uteuzi wa RJMT.

4. Maslahi ya wakuu wa vyombo hivi yatajwe na sheria itakayotungwa na Bunge la JMT. Iwe kama ambavyo maslahi ya wakuu wa kisiasa yametajwa na hata ya kustaafu kama ilivyo kwa "Political Service Retirement Benefits Act".

5. Mfumo wa ajira katika jeshi la polisi ubadilishwe. Sifa za kujiunga na jeshi ziimarishwe ili wapatikane watu wenye sifa.

6. Mtaala wa mafunzo katika jeshi la polisi uboreshwe ili wasome kwa muda mrefu kidogo mambo ya sheria, elimu ya uraia,utafiti, haki za binadamu, sociology, maswala ya maendeleo ya jamii, ustawi wa jamii na mengine yatakayofanana kuliko sasa ambapo ni kama wanafundishwa kupambana na uhalifu tu bila kujua yanayoambatana na uhalifu.

7. Tuanzishe chuo maalum(institute) kwa ajili ya mafunzo juu ya haki jinai nchini. Iwe ni Post Graduate Institution. Tuna chuo cha kodi, chuo cha Benki Kuu, cha Ulinzi na zingine kama hizo.

8. Sheria za Criminal Procedure Act(CPA), Penal Code, Prevention and Combating of Corruption Act, Prisons Act ziboreshwe.

Karibuni kwa maoni na mapendekezo mengine.
 
Napendekeza kufutwa kwa sheria inayounda TAKUKURU

Maana naona hawana kazi wala shughuli waliyofanikiwa Tangu ianzishwe

Napendekeza sheria inayounda DPP iboreshwe kwa kuunda ofisi ya waendesha mashtaka
Tusiwe na ofisi inayotambulika kwa cheo na pia ianzishe ofisi za waendesha mashtaka wa wilaya
Pia waendesha mashtaka wapewe majukumu ya Direct or indirect investigation ya matukio yote ambapo kwa namna yoyote wanaweza kufungua shauri kwa ushahidi walionao.

Ntakuja na sheria ya ushahidi
 
Napendekeza kufutwa kwa sheria inayounda TAKUKURU

Maana naona hawana kazi wala shughuli waliyofanikiwa Tangu ianzishwe

Napendekeza sheria inayounda DPP iboreshwe kwa kuunda ofisi ya waendesha mashtaka
Tusiwe na ofisi inayotambulika kwa cheo na pia ianzishe ofisi za waendesha mashtaka wa wilaya
Pia waendesha mashtaka wapewe majukumu ya Direct or indirect investigation ya matukio yote ambapo kwa namna yoyote wanaweza kufungua shauri kwa ushahidi walionao.

Ntakuja na sheria ya ushahidi
Kwa sasa hakuna sheria ya DPP. Kuna sheria ya National Prosecution Services Act(Sheria inayounda Ofisi ya Taifa ya Mashtaka).
 
Pia kwenye sheria ya waendesha mashtaka tuwe special- appointed organization of prosecutors ambao wamethibitishwa na bunge ambao watashughulika na masuala yote uhujumu uchumi, rushwa kubwa, matumizi mabaya ya ofisi, utakatishaji fedha, scandal chafu za viongozi wa serikali


Suala LA Rushwa ni jukumu LA Prosecutors wote kuanzia ngazi ya wilaya kwa Direct or indirect investigation power vested on them by law

Wakishachunguza suala lolote wanapeleka mahakamani direct bila ksubiri ruhusa na DPP Bali Mkuu Mahalia

Kwa nini waendesha mashtaka

Police wanaofanya uchunguzi hawajasoma hata degree ya sheria Bali basics na experience za mafunzo hivyo weledi unakosa pia wao wataendelea kuchunguza na kisha kupeleka kwa prosecutor wa wilaya ambaye ndiye afisa wa mahakama na hivyo tufute judicial police or Police prosecutor

Pia prosecutors wapewe madaraka ya kukamata kwa msaada wa police isiwe kama Takukuru na wawe na right of detention of a criminal
 
Back
Top Bottom