Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

..sijui kwanini wana-ccm, haswa mashabiki wa Jpm, mnamchukia Rais Samia Hassan.

..Rais Samia Hassan hajatimiza hata siku 100 madarakani, lakini wana-ccm wanamshambulia utadhani ni Raisi asiyetokana na ccm.
 
Lini hakimu alikaa akawahukumu kama magaidi au wachochezi, hiyo ndio haki, wapelekeni kwa majaji wawahukumu au wachiwe. unafunga mtu kama ulimuumba wewe bila aibu. Lets proove they are guilty through proper laws.
 
Mama Samia,ukikabdhiwa tu uenyekiti wa CCM,nakushauri uhutubie Taifa na utumie fursa hiyo kuwaomba radhi watanzania kwa niaba ya chama chako na serikali yako kwa yale yote yaliyotendeka chini ya utawala wa Hayati Raisi Magufuli.

Ni wazi sasa katika utawala wa Magufuli ambapo na nyinyi mlikuwa sehemu ya utawala huo, kulikuwa na uonevu na ukatili mwingi sana kwa watanzania wa makundi mbalimbali.

Haya tunayoaanza kuyasikia sasa ni ushahidi wa hali hii bila kusahau tuhuma za upotevu na matumizi mabaya ya fedha za umma tofauti kabisa na watanzania walivyokuwa wanaaminishwa.

Mheshimiwa Raisi, kitendo cha kuomba radhi kitasaidia kupoza hasira na machungu ya watu kwa marehemu ingawa baadhi wanaweza wasimasamehe.

Na itakuwa bora kama utaomba radhi katika hotuba yako ya kuushukuru kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa(naimani watakuchagua tu) kwani utakuwa umetumia jukwaa sahihi na tukio sahihi kuomba radhi kwa niaba ya chama chako na hata serikali kwani chama chenu ndio kinaunda serikali.

Pia, ili kuponya kabisa majeraha, tumia hotuba hiyo kutangaza adhima ya kufufua mchakato wa Katiba mpya ili tuondokane kabisa na katiba hii inayoweza mtawala kuwa dikteta.

Mama ukifanya hivi kwa vitendo, nakuhakikishia utaacha legacy kubwa sana kwa watanzania na watakukumbuka hata kama hutajenga hata kilomita moja ya lami.

Nawasilisha.
 
Watu wengi hapa wanacomment kwa mihemko na chuki zisizokuwa na sababu,kama mashehe wanna Makosa Basi wahukumiwe ijulikane aduabu yao ni ipi? Hawajawahi kutiwa hatiani na ni miaka zaidi ya nane Sasa.Tuwe waungwana.tuache chuki za kidini.Mimi mambo ya dini sijali Sana ila orientation yangu Ni mkristo lakini naongozwa na kiu ya haki na hivyo nadai haki ya mashehe ipatikane.
 
siku akifungwa pengo au ngwajima wakatolika watalia kila siku watoke
 
Kwanza Madam President mie ni mwananchi wako,nakusalimia kwa salaam za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.#Kazi iendelee.Kwa kifupi nikupe ushauri/ujumbe/maoni ya kuwa uwe unatembelea nchi mbali mbali duniani ukiambatana na wafanyabiashara wa kwetu,pia uwaalike wenzio waje na wafanyabiashara wao ili sote,sisi na wao tunufaike. Uende kwenye mkutano wa uchumi Davos, uhudhurie Mikutano mbali mbali muhimu kama vile kulihutubia Mkutano wa UN,mikutano ya uchumi,uturudishe kwenye ramani ya dunia.

Turudishe uhusiano na nchi jirani,nchi za jumuia ya madola,nchi zilizoendelea,nchi za mashariki ya mbali kama Malaysia,South Korea n.k.Faida zake ni kuwa ushatangaza kuondoa urasimu kwa wawekezaji.hilo limefika na limewafurahisha wengi duniani zikiwemo nchi Tajiri na za Middle East. Tuanzishe Joint commision kwenye sekta mbali mbali na wenzetu.Mfano tembelea nchi ya Qatar ambayo wanazalisha Gesi kwa wingi Duniani.

Tuanzishe joint commision watatusaidia sana katika sekta hiyo.Pia la mwisho umeona ulivyoenda Uganda,wenzetu wamechukua tahadhari zote dhidi ya Covid 19 na ikakulazimu hata wewe, Your Excellency Madam President na Wasaidizi wako mvae Barakoa(Mask).Nasi huku utuundie hiyo tume haraka ili ije na ushauri ambao utaamua na timu yako.

Turudishe uhusiano na mashirika ya kimataifa kama vile Unesco, UNHCR, IMF, World Bank, ILO na hasa WHO. Namalizia kwa #Kazi iendelee.
 
Bwa shehe mbona jazba? Kwani mimi ndo nimewaweka ndani hao watu? Unataka kusema kwamba ,tusitetee mashehe kwakuwa kuna watu wa dini nyingine nao wanateswa? Uzi ulihusu mashehe ,Kama vipi anzisha wa akina Sith na Ruge.
Bwa shehe Ndani hujawaweka wala mwaka 2012 hukuwa/bado hujazaliwa na hilo suala ni la huko Zanzibar na sio kwa awamu hii
tuliijadili tukaona tuwaachie wenyewe mpaka Jaji na Mwakili watajuana
ila kuna wengi tu km kina Ruge na Habinder nao waachiwe kwani Mada ya UAMSHO tumeshaiongelea sana na walitaka kuingilia Mhimili kuchochea kuuvunja Muungano na Kisiwa kiwa na Dini moja
 

Riots, incitement to murder and general criticism[edit]​

Zanzibar and Tanzania government has criticized UAMSHO for failing to stick to its purpose as registered and instead has turned into a political group questioning Zanzibar's place in Tanzania.[3] Uamsho has been accused of no longer being a purely religious movement: Uamsho has called for a referendum on Zanzibar's exit from the United Republic of Tanzania.
 
MSOMI HURU GEREZANI

Tangu rais samia suluhu hassan alipoingia madarakani nimekua nikifuatilia sana hotuba zake pamoja na ripoti anazotoa CAG na nimegundua baadhi ya vitu.

Kwanza namfananisha samia na msomi huru ambaye yupo gerezani kwasababu anajitekenya alafu anacheka mwenyewe. Ripoti zilizoletwa na CAG hivi karibuni zinaonyesha kuwa kuna upotevu mwingi wa pesa na kuna hasara kubwa ilipatikana kwa taifa kwenye miradi mikubwa iliyojengwa na JPM hivyo moja kwa moja kuinyesha kuwa JPM alikua ni fisadi.

Ila ukweli ni kwamba JPM hakua fisadi kwasababu katika uongozi wake kwa muda mfupi tu wa miaka mitano amefanya mengi zaidi ya marais waliokaa madarakani kwa miaka kumi.

Anachokifanya Samia kwasasa ni kuichafua image ya magufuli ili kuonyesha kuwa yeye ni bora ila anasahau kuwa yeye ni rais kwasasa kwasababu ya kura za Magufuli na kama kuna umati ambao unamkubali kwasasa ni kwasababu ya JPM.

Lakini pia Samia anasahau kuwa kama JPM akichafuliwa kwa namna yoyote ile basi ajue nayeye amechafuliwa kwasababu kwenye utawala wa JPM yeye alikuwepo kama makamu wa rais hivyo ni sawa na kujitekenya na kucheka mwenyewe.

"Ukiona umefanya kitu alafu mpinzani wako akashangilia ujue umekosea"JPM. kwasasa naona wale wachumia matumbo na mafisadi wa nchi wanampongeza sana samia kitu ambacho ni hatari sana kwa utawala wake ,bado hajachelewa anaweza kuangalia alipokosea na kujirekebisha mapema.

Rest in peace JPM, SHUJAA WA AFRICA.
 
MSOMI HURU GEREZANI
Tangu rais samia suluhu hassan alipoingia madarakani nimekua nikifuatilia sana hotuba zake pamoja na ripoti anazotoa CAG na nimegundua baadhi ya vitu...
Nafikiri mmekosea kujua kwamba tarehe ya Rais kupokea ripoti ya CAG huwa communicated mwezi mmoja kabla na Rais hupanga mwenyewe. Kwa mantiki hiyo unaweza kuona kabisa hii ripoti ilikuwa ipokelewe na Magu muda tu. Mnalaumu bure tu
 
MSOMI HURU GEREZANI
Tangu rais samia suluhu hassan alipoingia madarakani nimekua nikifuatilia sana hotuba zake pamoja na ripoti anazotoa CAG na nimegundua baadhi ya vitu...
Kwahiyo ukitaka ile ripoti isiwasilishwe? Mbona miaka yote hufanyika vilevile? Utofauti ni kwamba mama samia kasema kichere kuwa huru basi.
 
Naona waimba mampambio bado mnaendelea kuomboleza , Sasa hivi tupo kwenye utawala wenye uwazi kila kitu kinawekwa wazi kama uliiba inajulikana hakuna kuficha kama kipindi cha bwana yule. Muacheni mama Wa watu afanye Kazi kwa weledi wake msimpangie ,
Kuhusu samia kua pamoja na jiwe ,jiwe mwenyewe alikua hashauriki.

Kwa kauli yake mwenyewe alishawahi kusema kua , yeye ukimshauri ndio umehrubu kabisa , Sasa unafikiria huyo mtu Wa namna hiyo unaweza mshauri , mama samia alikua amekaa tu kama kivuli alikua hana lolote chini Ya jiwe.

Kwa taarifa yako huyu mama kuna kipindi alitaka kujiuzuru kautokana na tabia Mbovu za jiwe , šema ndio wakubwa walimsihi ili afiche aibu, Jiwe alikua hashauriki hata kidogo alijawa na kiburi sana.

Mungu amuweke mahali anapostahili huko alipo
 
MSOMI HURU GEREZANI
Tangu rais samia suluhu hassan alipoingia madarakani nimekua nikifuatilia sana hotuba zake pamoja na ripoti anazotoa CAG na nimegundua baadhi ya vitu...
We punguani kweli! Unataka Mama yetu afanye nini wakati uwasilishwaji wa taarifa ya CAG ni taratibu za kawaida?, Tawala zote kwenye ulimwengu hupokea taarifa hizi kwa ajili ya kujipima uwezo wao wa kusimamia mamlaka zao na kuangalia namna ya kujisahihisha, tatizo la " mkono wa chuma" makando kando yaliyomo kwenye taarifa ile yalikuwa yanamuhusu mwenyewe kutokana na kushiriki moja kwa moja kwenye maamuzi kwa maslahi binafsi pasipo kushirikisha Taasisi husika na matokeo yake ndiyo haya.

Ofisi ya CAG imepata tabu sana kipindi cha huyu fedhuli, inanyimwa mpaka fedha za kufanya ukaguzi wa hesabu hasa kwenye miradi anayofanya mpwa wake MAYANGA aliyezoea kutembea na Sanduku lililojaa fedha.

Sasa ujinga huu Bi Mkubwa hataki na utasikia mengi tu. Magufuri alikuwa fisadi na mwizi wa kutupa mpaka kwenye kusambaza nguzo za mradi wa REA ulikuwa wake kwa kumtumia yule jamaa wa pale mafinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…