Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Enyi TISS, sisi raia wema huku mitaani tuna imani Sana na nyinyi,kusema kweli tunawapenda Sana,Sasa Mimi Lee kwa niaba ya Watanzania wema,tunawaomba mumshauri na mhakikishe amepokea ushauri huu mheshimiwa Samiha.
Nawe mama Samiha Rais wetu nakuomba upokee ushauri huu Ili kufanya Tanzania iwe na amani upendo raha furaha na haki,kwani haki huinua Taifa.

Ushauri wangu
Naomba TISS chombo chetu Watanzania,mshaurini Rais Samiha atengeneze taasisi imara ili zilete haki.
Baadhi ya taasisi imara Ni
Mahakama huru,
Bunge huru,
Polisi huru,


TISS huru,
Takukuru huru,
NEC huru,
N.k
Faida ya taassisi huru itamfanya atawale kwa haki,kwa urahisi,kwa raha na bila lawama.
Taasisi huru itawafanya TISS wawe na kazi nyepesi bila lawama kutoka upande wowote.
Polisi hawata onea raia,
Mahakama itaamua kwa Haki,
Bunge litafanya kazi kwa weledi,
Takukuru hawata mwonea mtu,
NEC haitalaumiwa,
TISS haita laumiwa,
Hivyo Mama ataongoza kwa raha bila lawama,yeye atasimamia kuleta maendeleo tu.

Mbali na hayo yote tunaomba Rais Samiha uruhusu katiba pendekezwa ya Jaji Warioba, ambayo wewe Rais ulikua Spika wa Bunge la katiba,tunaomba haya kwa Mustakabali wa Taifa.

Ukiruhusu hayo utatawala ka amani Sana.

Tunaomba Taasisi Imara.
Nchi zote duniani zenye chombo kinacho shugulika na usalama wa taifa lazima kitapata wa kukilaumu kwa muda tofauti tofauti kiutendaji.

Kazi kubwa:

Kukusanya taarifa muhimu za kisiasa za mtu, kundi, jamii au taifa na kuchakata.

kukusanya taarifa muhimu za kijamii za mtu, kundi, Jamii au taifa na kuzichakata.

Kukusanya taarifa muhimu za kiuchumi za mtu, kundi, jamii au taifa ziwe za ndani na nje ya nchi na kuzichakata.

Kukusanya taarifa muhimu za Kiusalama, za mtu, kundi, jamii au taifa na kuzichakata na kuhakikisha zinafanyiwa kazi ki uweledi na wote wenye kuhusika.

Na kukusanya taarifa zozote nyingene zitakazo onekana muhima mahala popote na kwa mtu, kundi au jamii yeyote ile ambazo Zita onekana zinazoweza kulisaidia taifa kwa maamuzi yeyote.

Kuhakikisha maslahi ya kitaifa kiujumla yanalindwa na kuchumgwa, ( to promote, preserve and protect national interests.).

Kuhakikisha kuna utabiri sahihi wa matokeo ya baadae ya Kisiasa, kiuchumi, kijamii, ki usalama na mambo yeyote Yale yatakayo lisaidia taifa.

Kuhakikisha kuna hafidhi ya kutosha ya taarifu zote muhimu na zimechakatwa na kufanyika kazi kiuweledi kwa matumizi ya taifa na zipatikane kiurahisi kila zinapo hitajika.

Wawe na uwezo wa ki ushawishi au nguvu za kisheria kupata msaada wa ki utaalamu wa taaluma yeyote ile kutoka kwa wabobozi ndani au nje ya nchi kwa malipo au ridhaa.

Taarifa yeyote ile ikusanywe, ichakatwe na ihifadhiwe kwa uwezo wa juu kabisa wa usahihi wa akili ya binadamu ikibidi kwa msaada wa vyombo vyote vile. Taarifa zisivuje na kutopungua thamani. Zipate uhifadi na ikibidi kuongezewa thamani kwa miaka isiyo pungua miaka 20.

Kwa hiyo lazima kuna sehemu ukizidi kiasi lazima utawakwaa tuu.
 
Nchi zote duniani zenye chombo kinacho shugulika na usalama wa taifa lazima kitapata wa kukilaumu kwa muda tofauti tofauti kiutendaji.

Kazi kubwa:

Kukusanya taarifa muhimu za kisiasa za mtu, kundi, jamii au taifa na kuchakata.

kukusanya taarifa muhimu za kijamii za mtu, kundi, Jamii au taifa na kuzichakata.

Kukusanya taarifa muhimu za kiuchumi za mtu, kundi, jamii au taifa ziwe za ndani na nje ya nchi na kuzichakata.

Kukusanya taarifa muhimu za Kiusalama, za mtu, kundi, jamii au taifa na kuzichakata na kuhakikisha zinafanyiwa kazi ki uweledi na wote wenye kuhusika.

Na kukusanya taarifa zozote nyingene zitakazo onekana muhima mahala popote na kwa mtu, kundi au jamii yeyote ile ambazo Zita onekana zinazoweza kulisaidia taifa kwa maamuzi yeyote.

Kuhakikisha maslahi ya kitaifa kiujumla yanalindwa na kuchumgwa, ( to promote, preserve and protect national interests.).

Kuhakikisha kuna utabiri sahihi wa matokeo ya baadae ya Kisiasa, kiuchumi, kijamii, ki usalama na mambo yeyote Yale yatakayo lisaidia taifa.

Kuhakikisha kuna hafidhi ya kutosha ya taarifu zote muhimu na zimechakatwa na kufanyika kazi kiuweledi kwa matumizi ya taifa na zipatikane kiurahisi kila zinapo hitajika.

Wawe na uwezo wa ki ushawishi au nguvu za kisheria kupata msaada wa ki utaalamu wa taaluma yeyote ile kutoka kwa wabobozi ndani au nje ya nchi kwa malipo au ridhaa.

Taarifa yeyote ile ikusanywe, ichakatwe na ihifadhiwe kwa uwezo wa juu kabisa wa usahihi wa akili ya binadamu ikibidi kwa msaada wa vyombo vyote vile. Taarifa zisivuje na kutopungua thamani. Zipate uhifadi na ikibidi kuongezewa thamani kwa miaka isiyo pungua miaka 20.

Kwa hiyo lazima kuna sehemu ukizidi kiasi lazima utawakwaa tuu.
..hao jamaa wako kuilinda CCM na siyo kuilinda Tanzania.
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzani haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli kafa, lakini spirit yake haijafa. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu, katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli kafa lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, na kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli haijafa. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60, kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Rekebisha ukali na usahihi wa maneno, mfano Magufuli hajafa ial kafariki dunia, Sio Mzee Magufuli bali Marehemu Dk John Joseph Pombe Magufuli NK
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzani haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli kafa, lakini spirit yake haijafa. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu, katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli kafa lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, na kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli haijafa. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60, kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Awe mazalendo wa kweli kwa kuiheshimu Katiba iliyomweka madarakani na asiwe mtu wa kujimwambafai kama marehemu Magufuli,akumbuke sisi sote tutakufa lakini Tanzania itabaki na Watanzania daima.
 
Kipindi ulichopatia Uongozi ni kigumu sana. Kuna watu walimwelewa JPM katika kujenga Tanzania Mpya na kuna watu hawakumwelewa Kabisa ,kuna watu mpaka sasa wanamakovu ya JPM na kuna watu wana mavuno ya JPM.

Haya ni makundi mawili ambayo yanatakiwa kuunganishwa na si kuyaendeleza kuwepo au kuja na kundi la tatu. Kabla ya Yesu kristo kuja ulimwenguni yalikuwepo makundi mawili Israeli (Wayahudi) taifa teule na mataifa mengine ambayo hayakupata kibali Kwa Mungu.

Bwana Yesu alipokuja aliyaunganisha haya makundi yote na kuja na kundi moja watoto Wa Mungu...(kundi la taifa teule Israeli na kundi la wamataifa ya kazikwa)

"WAEFESO 2:16
Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba."

Wewe ndiye mwili wetu (naongea katika ulimwengu Wa nyama) wakuyapatanisha haya makundi mawili ndipo utakapoweza kuimarisha amani ya Tanzania.

Kipindi hiki kuwa makini na washauri na maneno mengi utakayosikia. Haikuwa kitu chepesi Kwa Wayahudi kuwakubali Wa Maitaifa...na wamataifa kujikubali kuwa wamepatanishwa na Mungu.

Silaha kubwa katika ili ni uvumilivu na kuonesha Upendo hata Kwa wale wasio staili Upendo. Neno la Mungu likae ndani yako Kwa wingi.

(GYS My Swahili is not good , sorry of that )kiswahili changu sikizuri sana.
 
Bila kuchelewa au kupoteza muda tupendekeze miswaada kwa mkutano wa kwanza utakaofanyika Mama Samia akiwa Rais wa JMT

1. Punguzo la makato ya bodi ya mikopo kutoka 15% hadi 5%

2. Kupandisha mishahara kwa wafanyakazi wote wa ngazi za chini serikalini.

3. Ajira kwenye sekta ya Afya na ualimu.

4. Kufuta kodi zote zinazohusu usajili wa online TV

5. Kuruhusu fao la kujitoa kwa wanaoacha kazi.

6. Kurudishwa kwa PPF, PSPF, LAPF na GEPF ili kuongeza ufanisi katika kutoa mafao kwa wastaafu na wanaocha kazi.
 
Maneno yako mazuri, ila mbona kama unamfokea...

Rais hapangiwi...
 
Mh Rais katka mambo ya kufanya hakikisha unafanya yafuatayo:

1.Futa wilaya ya Chato ibaki kata
2.Futa Mpango wa kuipa Chato Mkoa
3.Futa Mpango wa kujenga Daraja la Mwanza la ziwani
4.Ondo miradi ya Maendeleo ya maji chato
5.Ondoa makao makuu Dodoma, na turudi Dar
6. Futa strogiers gourge..tuendeleze gas na tuwape makampuni binadsi kuzalisha umeme ili tupate ajira zaidi
7.Futa SGR ili hera ziendele kwenye maendeleo ya watu na siyo ya vitu
8.Fut mambo ya EFD kwani yanasababisha biashara kusinyaa.
3.afute daraja la kigongo-busisi kwa sababu ya chuki zako zidi ya JPM? hilo halikubaliki kabisa,pesa na muda uliotumika upotee tu hilo daraja Ni la muhimu sana kwa sasa kwani limefuta muda unaopotea hapo feri.mambo yote unayotaka yafutwe nikujitia hasara tu kuyafuta lbd hilo la chato kuwa mkoa.
 
Siyo Mzalendo Wewe Mwenyewe
Miradi Mingi Ipo Kwenye Hatua Nzuri
Unaifutaje. Bwawa La Nyerere Lipo Asilimia Hamsini Unalifutaje? SGR Imefika Morogoro
Unaifutaje. Labda Ambayo Haijaanza
ambayo haijaanza Ni muhimu tu unapakia mzigo wa Uganda kwenye reli ukifika Dom unashuka halafu unapandishwa tena hasara ya handling itakuwaje? au siyo kitu mradi wakome?
 
Mh Rais katka mambo ya kufanya hakikisha unafanya yafuatayo:

1.Futa wilaya ya Chato ibaki kata
2.Futa Mpango wa kuipa Chato Mkoa
3.Futa Mpango wa kujenga Daraja la Mwanza la ziwani
4.Ondo miradi ya Maendeleo ya maji chato
5.Ondoa makao makuu Dodoma, na turudi Dar
6. Futa strogiers gourge..tuendeleze gas na tuwape makampuni binadsi kuzalisha umeme ili tupate ajira zaidi
7.Futa SGR ili hera ziendele kwenye maendeleo ya watu na siyo ya vitu
8.Fut mambo ya EFD kwani yanasababisha biashara kusinyaa.
WEWE unakopo tu akilihuna.
 
Mh Rais katka mambo ya kufanya hakikisha unafanya yafuatayo:

1.Futa wilaya ya Chato ibaki kata
2.Futa Mpango wa kuipa Chato Mkoa
3.Futa Mpango wa kujenga Daraja la Mwanza la ziwani
4.Ondo miradi ya Maendeleo ya maji chato
5.Ondoa makao makuu Dodoma, na turudi Dar
6. Futa strogiers gourge..tuendeleze gas na tuwape makampuni binadsi kuzalisha umeme ili tupate ajira zaidi
7.Futa SGR ili hera ziendele kwenye maendeleo ya watu na siyo ya vitu
8.Fut mambo ya EFD kwani yanasababisha biashara kusinyaa.
Umesahau jambo muhimu sana kwa watumishi wa umma, nalo ni kuongeza mishahara na marupurupu kedekede
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo
Ni mda wa kumuacha, mh rais mpya ,Mambo ya spirit sijui za nani ,tz haijaanza leo, yapo nahitaji mengi ya kitaifa moja ikiwa mshikamano,katiba mpya, mishahara ya watumishi wa uma, Uhuru wa vyombo vya habari, n.k

Mengine yatafuata, na ni kweli miladi lazima kuhisha maana zimetumika pesa za watanzania japo mingi ni maumivu KWA taifa
Vinginevyo msianze mpangia hasa nyie ccm,

Tunataka makamu wa rais mpya sio wa kimtandao, nchi hii yetu sote hata Kama yuko Kijijini analima miogo sawa ila sio hao wakina BASHIRU, full stop,note hata mbatizaji anaweza kua makam wa rais sio kila mda kwamba achaguliwe Alie na mtandao kwani Kati yao na taifa la tz nani katangulia
 
Ni wiki ngumu na yenye majonzi. Wanalia pale uwanja wa Uhuru kuanzia watoto wa shule za msingi mpaka wazee waliostaafu. Nafsi zinalia kwani aliyeondoka alivunja daraja lililokuwepo kati ya Uongozi wa juu na mwananchi wa kawaida.

Kila anayekaribia jeneza unamuona akihuzunika kutoka moyoni kabisa. Ni machozi ya kweli, yenye uhusiano wa moja kwa moja na moyo, haya hayawezi kuwa machozi bandia. Ni huzuni ya kweli itokayo ndani kabisa ya upande wa ubongo ulioumbwa kwa ajili ya shukrani.

Aliimba Patrick Balisidya pale katika uwanja wa Arnatoglu miaka ya nyuma kuhusiana na watu wema. Na naamini wema huwa hauozi siku zote unaishi ndani ya historia za kimaisha.

Winston Churchil aliishi miaka mingi iliyopita lakini ndani ya mioyo ya waingereza mpaka kesho wanaona ufahari kukumbuka kauli na matendo yake.

Pole sana Mama Janeth na familia nzima. Pole nyingine ni maalum kwa mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na hii ni ile inayoenda sambamba na ushauri kwake katika kipindi hiki kigumu kwake, ambapo analo jukumu la kumchagua makamu wake kwa umakini mkubwa.

Akikosea tu katika uteuzi anaweza kukuta ndani ya miaka minne iliyobakia anaweza kujikuta anafanya kazi na mtu ambaye ni adui wa kile ambacho kimejengwa kwa jasho jingi na ujasiri wa kutazama mbele pasipo kuisikiliza miluzi mingi kwa maana ya maneno mengi ya kila aina ya mwenye kujiona anayo haki ya kushauri. Akikosea anaweza kujikuta anafanya kazi na mtu mwenye mipango ya urais wa 2025 hivyo nchi ikashindwa kusonga mbele.

Ipo miradi mingi ambayo imefikia nusu ya safari, hii inabidi imalizwe tena kwa ubora ule ule uliokusudiwa tangu mwanzo. Utekelezaji wa miradi hii unahitaji makamu ambaye kwanza anao mchango mkubwa wa maono ya kiuchumi, mtu ambaye kwenye vikao vya baraza la mawaziri au vile vya kutathmini mafanikio ya taasisi au wizara, anakuwa ni mchangiaji wa mawazo na sio anayekaa tu akisubiri siku ipite.

Mheshimiwa Rais kwepa kabisa hii aina ya watu wenye makundi nyuma yao. Hawa ni wavizia fursa wenye utayari wa kufanyia 'udalali' cheo kikubwa. Ni kipindi chenye kuhitaji sana umakini wa upitiaji wa majina.

Lakini siku zote Mungu amekuwa akiilinda sana Tanzania. Ni nchi iliyopata bahati ya kuwekwa mikononi mwa Mungu tangu wiki ile ya uhuru mwaka 1961.
 
Back
Top Bottom