Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Huyu mama,yaan Rais Samia Suluhu Hassan akija kumaliza kipindi chake kiutawala...watanzania na Rais wetu tumtakae(ajae) tutalia na kusaga meno na hapatakuwepo hata muda wa kumwomba msamaha huyu mama.
Mwenyezi akatufungue akili zetu.Kila aombae kura ataka kura....amani ni kitu cha msingi Sana ndugu zangu.

Mungu ibariki Tanzania.🙏
Nakuhakikishia kuwa hiyo post yako itatafutwa sana na wana JF kukuuliza kuhusu UNABII wako.

Samia yuko kwa mapenzi ya Mungu kwa Taifa letu. Kifo cha Mwendazake kiitokea kwenye kipindi ambacho kama angekuja kiongozi mwingine tofauti na yeye basi utulivu wa Taifa ungekuwa mashakani. Heshima kwako Mkatoliki mwenzangu General Venance Salvarory Mabeyo kwa kuhakikisha peaceful transition
 
Nakuhakikishia kuwa hiyo post yako itatafutwa sana na wana JF kukuuliza kuhusu UNABII wako.

Samia yuko kwa mapenzi ya Mungu kwa Taifa letu. Kifo cha Mwendazake kiitokea kwenye kipindi ambacho kama angekuja kiongozi mwingine tofauti na yeye basi utulivu wa Taifa ungekuwa mashakani. Heshima kwako Mkatoliki mwenzangu General Venance Salvarory Mabeyo kwa kuhakikisha peaceful transition
Ishaunganishwa mkuu
 
Nakuhakikishia kuwa hiyo post yako itatafutwa sana na wana JF kukuuliza kuhusu UNABII wako.

Samia yuko kwa mapenzi ya Mungu kwa Taifa letu. Kifo cha Mwendazake kiitokea kwenye kipindi ambacho kama angekuja kiongozi mwingine tofauti na yeye basi utulivu wa Taifa ungekuwa mashakani. Heshima kwako Mkatoliki mwenzangu General Venance Salvarory Mabeyo kwa kuhakikisha peaceful transition
Huyo mabeyo kwasasa anajutia jambo fulani ambalo hawezi weka wazi!

Samiah katutoa Sana kweli lakini Kuna mambo yatatutafuna na kizazi chetu huko mbeleni!

Itafikia kipindi tutalipa Kodi ya ardhi Kwa wageni ndani ya ardhi yetu wenyewe!!

Ni hilo tu!!Ardhi,ardhi ,ardhi ,ardhi ya Tanganyika eeh Ardhi!
 
Leo morogoro ilikuwa balaa. Hata jpm hajawahi kulakiwa vile na nyomi ile.

Wakuluma wanainjoy sana chini ya utawala huu. Mazo mengi jpm aliua na soko kukosena sasa mama karudisha tabsamu. Kororosho, mbaazi, viazi nk
 
Kazi ipi nzuri unaiongelea ?

Kubinafsisha mali za Tanganyika

Kuchukua mikopo na kuipeleka Zanzibar huku walipaji wakiwa Watanganyika
 
Kazi ipi nzuri unaiongelea ?

Kubinafsisha mali za Tanganyika

Kuchukua mikopo na kuipeleka Zanzibar huku walipaji wakiwa Watanganyika
Kawaulize moro wanavyomshangilia utafikiri masihi. Wakulima wanajua samia anachowafanyia. Jpm aliua mazao yao. Mam karudisha tabasamu kwa masoko ya nje na ndani
 
Leo morogoro ilikuwa balaa. Hata jpm hajawahi kulakiwa vile na nyomi ile.

Wakuluma wanainjoy sana chini ya utawala huu. Mazo mengi jpm aliua na soko kukosena sasa mama karudisha tabsamu. Kororosho, mbaazi, viazi nk
Bado mnaamini kuna watu wanahadaika na hizo nyomi za mchongo? Kama mnajiamini kwa hizo nyomi za mchongo, ruhusuni tume huru ya uchaguzi muone mnavyojidanganya vibaya.
 
Leo morogoro ilikuwa balaa. Hata jpm hajawahi kulakiwa vile na nyomi ile.

Wakuluma wanainjoy sana chini ya utawala huu. Mazo mengi jpm aliua na soko kukosena sasa mama karudisha tabsamu. Kororosho, mbaazi, viazi nk
for sure wakulima wanaenjoy with very long smile na uongozi wa huyu rais kipenzi cha waTanzania Dr Samia Suluhu Hassan...

uwekezaji uliochochea mapinduzi na mageuzi makubwa katika kilimo umeleta mabadiliko makubwa mno kwenye maisha ya waTanzania 🐒
 
Bado mnaamini kuna watu wanahadaika na hizo nyomi za mchongo? Kama mnajiamini kwa hizo nyomi za mchongo, ruhusuni tume huru ya uchaguzi muone mnavyojidanganya vibaya.
Wenzako kenya hawasubili serikali iruhusu tume huru ya uchaguzi bali wanaidai kwa nguvu na kufa wachache. Sasa wewe kama.unasubilia na unaogopa kufa basi endelea kusubili
 
Leo morogoro ilikuwa balaa. Hata jpm hajawahi kulakiwa vile na nyomi ile.

Wakuluma wanainjoy sana chini ya utawala huu. Mazo mengi jpm aliua na soko kukosena sasa mama karudisha tabsamu. Kororosho, mbaazi, viazi nk
Unaonaje umshauri bi mkubwa uchaguzi uwe fair and square kama kweli anapendwa watanzania waamue bila kuchakachua?
 
Hivi kuwa chawa (mpumbavu) inacost kihasi gani? Kuna fungu huwa linatengwa kwa haya mapambio?
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli amefariki, lakini spirit yake inaishi. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi, iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli amefariki lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana, usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili, lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli inaishi. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60 kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Rais Samia Suluhu Hasan(Phd) kaongoza vizuri. Ni muda muafaka akapumzike kizimkazi kazi ya urais ni ngumu sana.
 
Mheshimiwa Rais, Shikamoo

Jukumu namba moja la Serikali yoyote duniani ni kuhakikisha nchi haina vurugu na inaendeshwa kwa utaratibu (Public Order). Serikali zote duniani lazima ziendelee kutekeleza kazi yake hii takatifu ambayo ni msingi wa mambo mengine yoyote yale kwenye nchi. Hata maisha hayatawezekana kama hakuna “public order”. Toka umeingia madararakani umeifanyia kazi hii kwa mafanikio makubwa. Umeliweka taifa letu salama, imara na kwenye njia sahihi.

Naandika ujumbe huu kukuomba na kukusihi kuendelea kutekeleza jukumu hilo kama ambavyo unafanya. Daima dawamu tusiruhusu uvunjifu wa sheria na amani yetu kwa kigezo cha uhuru wa kuzungumza. Tusiruhusu nchi yetu kuingia katika madhila yoyote kwa kigezo cha uhuru wa kukusanyika na kufanya siasa.

Wewe ni mtu mwema sana, mama na muumini wa mazungumzo na upatanishi, sote tunafahamu hilo. Tafadhali endelea kutumia njia zote unazopewa na Katiba, sheria na miongozo ya nchi yetu kuhakikisha kwamba wajasiriamali wa kisiasa ama mtu yoyote, popote ndani ya nchi yetu hapati mwanya wa kuvuruga Taifa hili. Uhuru wa kukusanyika na kufanya siasa lazima ufuate utaratibu na kama usipofuatwa basi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama viingine kazini kuhakikisha public order inaheshimiwa na kudumishwa kwa faida ya kila mwananchi.


Ahsante kwa kusoma. Mungu Akubariki.
 
#MchapakaziSamia katika Sekta ya Maendeleo ya Jamii
 

Attachments

  • IMG-20240818-WA0000.jpg
    IMG-20240818-WA0000.jpg
    146.5 KB · Views: 4
Back
Top Bottom