Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Naunga mkono hii hoja ila tusisahau kumkumbusha mhe. rais kutumbua majipu ktk mikataba iliyojaa harufu mbaya ya ufisadi.hasa TANESCO makampuni yapo pale kuzalisha umeme na hatimaye kuwanyonya watanzania wanaotumia nishati hii.mfano DOWANS,IPTL,AGREKO,PAP,nk
 
Kuna BONGE la jipu kwenye Ruzuku za vyama vya siasa!!!
Ha ha ha!!
 
Wajenge reli na kuimarisha usafiri huo. Huu ujanja wa TRA na makontainer kupotea utapungua kam si kwisha kabisa.
 
Juzi nilienda kununua kifaa flani duka flani maeneo ya samora alikuja jamaa fulani nahisi anafanya kazi serikalini ni mtu mzima sana jamaa aliulizia laptop akaambiwa 960,000 akaulizia na windows 7 genuine pamoja na licence keya zake akaambiwa 420,000 jamaa akamwambia muuza duka hivyo vitu vyote avi double mara mbili mpaka muuzaji akamwambia hapana aiseee hii hio ofisi ukiipeleka watakataa...kwenye manunuzi kuna watu ni wapigaji kweli...
 
Bado nssf makato kutoenda kwa wakati

HATA NSSF nao wawekwe kwenye list ya Majipu Maana najua fika wana madudu ya hali ya juu maana malimbikizo yetu wakubwa wanayafanyia biashara saaana unajikuta una mchango mkubwa kama 50M kwenye mfuko wa NSSF nenda pale waulize mna mikakati gani na sisi wanachama wenu hizo nyumba hatuzioni na sasa wamekuja na saccos unaambiwa uje na vithibitisho vya mali isiyo hamishika mara sijui hiki au kile.

Hili shirika linakosa watu makini wa kuwa wabunifu wa miradi kwa ajiri ya kuwapa mikopo wanachama wao kutokana na michango yao hata nusu ya michango yao ili hata kusimammia hizo fundi. kwa mfano upande wa kilimo NSSF inaweza ikawachukuwa wanachma kadhaa wakajiunga na hizi NGO kama TAHA watu wakalima kilimo cha kisasa kwa Green House hii itawatoa watu kabisa ni swala la vision na utaratibu kufanyiwa kazi. Matokeo yake NSSF imekalia kusema inajenga majengo tena kwenye mikoa michache, ukiangalia wana wanachama nchi nzima

 
Ivi mtumbua majipu hajaliona hili jipu TANESCO? Mbona ngonjera za kukatika katika umeme haziishii yaani kwa kifupi umeme wa kutumainia kuwa utakuwepo 24/7 hakuna kuna maluwe luwe tu. Mbona wakati huu ni wamasika, au kuliko na mabwawa ya kuzalisha umeme mvua hasinyeshi?. TANESCO kuna nini pale?
 

Wewe Dr ndo anajua wapi pa kuanzia maana huu mwili (nchi) una majipu kila kona hadi kwenye nyeti (ile idara muhimu kabisa).
 
mh magufuli umesema we we ni msomi na unapenda kusoma hembu pitia hapa

Tatizo ni mfumo. hata kama utastikuza usiku na mchana haisaidii kitu kwani tunatakiwa ujenzi wa kimfumo wa uongozi.
nitoe mfano kama taasisi ni huru haiwez kuingiliwa na vimemo vya wanasiasa. pia viongozi wake watakuwa vetted na binge.

huwezi kujenga mfumo bila sheria na sheria mama no katiba. kama kweli magufuli hafanyi komedi afute katiba pendekezwa na aitishe binge la katiba huru lisiilotokana na wabunge wa vyama hapo MAGUFULI FOR CHANGE ITAONEKANA.
UTASTUKIZA HADI LINI?

argue, don't shout!.
 
Nimesoma mwishoni nikaona nikuambie jibu lako linapanuka bado tu kupasuliwa na pia nitakusaidia tumuongezee vichwa vinavyojivuta kuwa kila pahala kwa wakati mmoja na hapo pia sheria na katika na kila utakacho WEWE kiwe.
 
Wewe unajuwa huyo anayejiita HAMID-Y kafanya nini? Alitangazia Mh Aboud Jumbe amefariki. Unajuwa usumbufu gani kasababisha kwa watu? Usiwe unatetea watu tu bila ya kujuwa chanzo chake. Hili jamaa thenge sana na kama unamtetea endelea kumtetea.
Haya bana mimi simo kwenye ugomvi wenu
 
Narudia tena, wwe ni jipu ulilotumbuliwa,
kipindi cha kampeni ulimfagilia sana magu na sisiem,
tulia uisome namba mkuu
 
nchi yetu inaajiri zaidi ya 70% ya watu wake ktk secka ya kilimo kwa ajili hiyo wanaajiri wataalam wa kilimo aka maafisa ugani ktk ngazi mbalimbali kwa bahati mbaya sana mm sijaona impact yao kwa wakulima wa kawaida coz licha ya uwepo wao bado wakulima wetu wanalima kilimo cha mazoea chenye tija ndogo na kazi ngumu mbaya zaidi ni kua hata baadhi yao hujiunga na raia wa kawaida kulima na kufuga kwa mtindo ule ule wa mazoea kuna sababu gani ya kuwa na hawa waitwao wataalam wakati kazi yao hatuioni
 
ni ukweli usiofichika, kilio cha wananchi siku zote kimekuwa ufisadi ufisadi ufisadi pamoja na ujenzi wa uchumi ulio imara kwa sababu mali asili zimejaa lukuki. kuna shida moja kwamba kama Magufuli ataendelea hivi kwa speed hiii bila hata kununuliwa , basi wananchi kwa kauli moja tuamue tumpe muda wa zaida kwa kubadilisha katiba ili imruhusu awe rais hata kwa miaka 20. Mungu ampe afya njema. nina uhakika kama akiendelea hivi kwa miaka 20 nchi hii itakuwa imepaa kuwa na uchumi wa juu kabisa na sio wa kati tena.
lakini mambo ya demokrasia demokrasia ndio yanaturudisha nyuma , eti baada ya miaka 10 , basi tena. sasa akija rais bomu si ataturudisha nyuma miaka 10 tuanze upya tena. wananchi tuwe macho.
hii tabia ya upinzani eti kujifanya kungangania kutaka kwenda ikulu ni ya kutulotezea muda kama tunapata watu kama Magufi. imagine leo Lowasa ndie angekuwa rais. haya wengi wa wafanya biashara waliokwepa kodi ni marafiki zake. na wamemchangia kwenye kampeni za urais. angewezaje kuwakamata na kuwaambia walipe kodi ?????? sana sana angewaambia basi wajitahidi wasikwepe tena. lakini wangetafuta tuu mbinu nyingine za maufisadi hiyo ip kwenye damu jamani za hawa watu. wafanya biadhara always hawaridhikagi na mapato na wana hulka ya kutaka kukwepa kodi kwa namna yoyote na ku maximize faida ili wazidi kupanuka.
pia tumejifunza kuwa kumpeleka rais ikulu ambaye ni mfanya biashara au ana chain ya wafanya biashara mzigo mkubwa sana kwa nchi. wanaweza yumbisha nchi kwa kuamua watakavyo wao. wananchi maskini hawawezi pata fursa wala haki yoyote. haya angalia mfano mzuri ule ufukwe wa Coco beach. Manji ndio alishaubeba hivyo huku akinyima fursa na haki za watu wa manzese na tandale kwenda ufukweni walau nao wafurahie maisha yao kama binadamu wengine. lakini mifanya biashara mikubwa haijali hayo ni wabinafsi hawajali binadamu wenzao. Magufuli hapa kaonyesha ujamaa uliotukuka. angekuwa Lowasa walahi angesema mwacheni Manji maadam kashinfa kesi basi apaendeleze pale ili alipe kodi forodhani. pasikae burebure. asingewajali masikini. kwani ni lini alionyesha kuwajali .asikini. kwake Monduli kuna masikini wa kutupwa hawana hata maji mpaka leo hii pamoja na mipesa lukuki aliyonayo. sasa angewezaje kuendeleza taifa kwa mtaji huu. au ulikuwa utapeli wa kisiasa.
anyway nilikuwa najaribu kulinganisha na kupambanua aina ya watu ambao wanaweza kiukweli kupaisha nchi hii kimaendeleo kwa haraka. tusiende na upepo wa kuhongwa na kudhani eti fulani atafaa kuongoza nchi. ni hatari ukishauza utu wako basi ndio umekwisha hivyo. ni sawasawa bwana mwenyekiti wa chadema aalivyohusishwa na kashfa ya kuuza utu kwa kutoa nafasi ya ugombeaji urais kwa Lowasa bila kufuata utaratibu uliokuwa umepangwa awali. na hapo ndipo anguko kuu la chadema na ukawa lilipoanzia. hakuna mchawi mwingine. kwa nini utaratibu uliowekwa na viongozi wa vyama ulipindishwa kiujanjaujanja tuu mpaka kufanya makamanda Slaa na Lipumba kutimka. haikuwa haki lakini maadam uhuru uliuzwa kwa tamaa ya pesa basi matokeo ndio haya sasa. sasa kama ukawa tuliweza kupindisha mfumo mzuri uliowekwa kabla ya kuingia kwa kundi la mafisadi kutoka ccm, tulikuwa na uthubutu gani wa kusema mfumo wa ccm ndio mbaya ??? . ukawa ungewezaje sasa kujenga mfumo uliosimama kama wangechukua madaraka.??? wanasiasa mmetudanganya sana na safari hii ndio tumewafahamu vizuri sana.
mfano wanasiasa wa ukawa wamekuwa wakituaminisha kwa miaka 8 kuwa Lowasa na sumaye ni mafisadi kwa kupitia njia mbalimbali kama magazeti ya Mwanahalisi ya Kubenea, MP Ubungo na mikutano ya hadhara mingiiiii. lakini baada ya kununuliwa na kuuza utu wao waligeuza misemo yao na kusema wamewasafisha, kwa hiyo ajenda ya ufisadi ikawa imefia hapo. na Magufuli kwa sababu ni msafi akaibeba na sasa ajenda hiyo anaendelea kupambana nao mafisadi mpaka kieleweke.
Salam hizi kwa wanasiasa wetu. enzi za kufanyia siasa usanii zimeisha. tunataka tupaishe uchumi wetu sasa.
hongera Magufuli Mungu aendelee kukulinda
 
Kaka Magu kama kuna eneo limeliwa na ushahidi mgumu kupatikana ni kwa wauza mafuta,hamishia nguvu hapo na komaa kila depot wakupe hesabu zao utagundua TRA hatakiwi kubaki MTU,hao wamekula sana kodi zetu na bado mafuta bei juu hata yakipungua huko duniani,ewura pia piga chini wote anza upya
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…