Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
nina swali. kama tanzania tunaweza kuprint pesa feki na kuziweka katika system. bas ushaur wangu wenye technlojia hii ya printing tunge waongezea ujuzi na vifaa wawe wana print kwa ajili ya nchi yetu. na sio kwenda kuprint nje ya nchi na kulipa mabilioni ya hela, kuna watu inawalipa ndio. lakini naomba ufafanuzi juu ya ushauri huu. Ni lazima serikali kuprint fedha nchi za nje.
 
nina swali. kama tanzania tunaweza kuprint pesa feki na kuziweka katika system. bas ushaur wangu wenye technlojia hii ya printing tunge waongezea ujuzi na vifaa wawe wana print kwa ajili ya nchi yetu. na sio kwenda kuprint nje ya nchi na kulipa mabilioni ya hela, kuna watu inawalipa ndio. lakini naomba ufafanuzi juu ya ushauri huu. Ni lazima serikali kuprint fedha nchi za nje.

mkuu hizo noti feki hata kwa macho unaijua kirahisi.....ndio maana amesema mara nyingi wanawapiga wakulima minadani watu ambao mara chache sana wanatumia noti ya 10,000....ila ni feki kabisaa.

ila hao wanaoziingiza BOT au NMB kama anavyosema mleta mada wanaleta janga kwenye uchumi
 
nina swali. kama tanzania tunaweza kuprint pesa feki na kuziweka katika system. bas ushaur wangu wenye technlojia hii ya printing tunge waongezea ujuzi na vifaa wawe wana print kwa ajili ya nchi yetu. na sio kwenda kuprint nje ya nchi na kulipa mabilioni ya hela, kuna watu inawalipa ndio. lakini naomba ufafanuzi juu ya ushauri huu. Ni lazima serikali kuprint fedha nchi za nje.

Hakuna cha mitambo wala nini, wana Scan na kuprint hamna cha ziada
 
Ni jambo zuri sana kwa uchumi wa nchi ila nina wasiwasi endapo tutapiga marufuku uagizaji wa vitu hivyo tutakuwa na uwezo wa kujitosheleza wenyewe...!?isije ikawa ndio tukavipoteza madukani na vikaanza kupatikana kwa magendo.
ni wasiwassi tu.:A S 109::A S 109::A S 109:
 
Ondoa wasiwasi hatuwezi kuvikosa kwakuwa wawekezaji wote wanatafuta nafasi kama hizo ili wazitumie kutanua wigo wa kukuza mitaji yao, ila kile wanachotaka uwahakikishie ni uwepo wa umeme usiokatikakatika ovyo; wakishajilizisha kuwa umeme ni wauhakika, tena kuna amani nchini; watajenga viwanda vingi mno vitakavyo zalisha utoshelevu wa mahitaji ya nchi na kisha kutafuta soko ng' ambo, tena watajitahidi kuzalisha bidhaa za kiwango cha kimataifa. Kwahiyo nchi hatatumia fedha za kigeni kuagiza bidhaa kama zile zilizoorozeshwa hapo juu, na hii ndo itakuwa Tanzania mpya ya Magufuli

Endapo hili halitafanyika, tusiregemee mabadiliko ya uchumi chanya kwakuwa siku zote tutabaki kuwa consumer jambo ambalo siyo zuri kwa nchi inayotaka kuendelea
 
Ondoa wasiwasi hatuwezi kuvikosa kwakuwa wawekezaji wote wanatafuta nafasi kama hizo ili wazitumie kutanua wigo wa kukuza mitaji yao, ila kile wanachotaka uwahakikishie ni uwepo wa umeme usiokatikakatika ovyo; wakishajilizisha kuwa umeme ni wauhakika, tena kuna amani nchini; watajenga viwanda vingi mno vitakavyo zalisha utoshelevu wa mahitaji ya nchi na kisha kutafuta soko ng' ambo, tena watajitahidi kuzalisha bidhaa za kiwango cha kimataifa. Kwahiyo nchi hatatumia fedha za kigeni kuagiza bidhaa kama zile zilizoorozeshwa hapo juu, na hii ndo itakuwa Tanzania mpya ya Magufuli

Endapo hili halitafanyika, tusiregemee mabadiliko ya uchumi chanya kwakuwa siku zote tutabaki kuwa consumer jambo ambalo siyo zuri kwa nchi inayotaka kuendelea

ungebahatika kuishi miaka ya 80-90, ukiwa na utambuzi wa mazingira yanayokuzunguka usingeandika hayo.
 
1. VIATU NA MIKANDA YA NGOZI TOKA NJE YA TZ
2. TOOTHSTICKS TOKA NJE YA TZ
3. JUICE AINA YOTE TOKA NJE
4. BIDHAA ZOTE AINA YA PLASTIC IKIWEMO NA MIFAGIO AINA YOTE PIA PIPE AINA ZOTE ZA BOMBA
5. BIDHAA AINA ZOTE ZA MBAO TOKA NJE YA TZ
6. KOKI AINA ZOTE ZA MABOMBA
7. BIDHAA AINA ZOTE ZA CHOKAA IKIWEMO NA RANGI
8. AINA ZOTE ZA BIDHAA MASHULENI
9. VYOMBO VYOTE VYA MAJUMBANI


Ukishafanya hivyo yaani Tanzania ya Magufuli ya viwanda itawezekana kabla hata haijafika 2017. Kupiga marufuku bidhaa hizo hapo juu toka nje ya TZ kutachochea ujenzi mkubwa sana wa viwanda vya kutengeneza hizo bidhaa mhimu kwa matumizi ya binadam. wawekezaji wataitumia hiyo fursa kukuza wigo wa biadhara zao na kuongeza ajira kwa Watz.

Jambo la mhimu kwako ni kuhakikisha umeme haukatiki kwakuwa tayari gass asilia ipo. Pia uongee na makampuni yanayo jishulisha na utengenezaji wa bidhaa za kielectronic mfano: computer, simu za mkononi, cd, flash, aina yote ya vyombo vya muziki, memory cards e.t.c kuja kujenga viwanda vya kuzalisha bidhaa hizo. Mungu akikupa neema zungumza pia na yale makampuni yanoyotengeneza vipuri vya magari ikiwezekana waje kujenga viwanda vya hiyo shuguli.

Mungu akikuwezesha kuyafanya haya ifikapo 2024 tutaibadilisha katiba yetu ili uendelee kutuongoza kwakuwa utakuwa umeyafanya yale amabayo si marais waliokutangulia tu bali marais wote wa Africa hawajayafanya kuwa wanapoingia madarakani kazi yao hugeuka kujilimbiza mali nying mno ambazo kiukweli hawataweza hata kuzimaliza kwa matumizi yoyote binafis. Kadhia hii imeleta kilio kikubwa mno katika bara zima la Africa, na hii ndiyo imesababisha nchi zote za Afriva kuwa tegemezi kwa weupe huku tukiwazidi kwa utajiri wa vitu vya asili. Ni aibu kubwa imetupata waafrica hata mbele zake YEYE aliyetuumba tumeleta fadhaa kumbwa ya kwamva tumeonekana watu wasiojipenda na wasio na akili hata ya kujua kuwa ni matajiri kuwazidi watu weupe.

Uwepo wa viwanda ktk taifa ni injini ya maendeleo; chonde chonde baba yangu Magufuli wingu la tamaa ya kujilimbikiza mitrilion huk wengi wakifa maskini lisikufunike kabisa bali wewe Rais Magufuli uwe hodari ukafanye yaliyo mema mbele zake aliyekuumba na mbele za watu wako watanzania

Basi, Neema na Amani itokayo kwa Mungu wetu, yaani BABA yetu wa Mbinguni iwe juu yako katika utumishi huu uliokupa Yeye aliyejuu kupita vyote; uwe hodari, ufanye kiume jitie nguvu na wala usiwaonee haya wote wapendao dhuruma na kuhujumu nchi yetu; watu kama ni wabaya si kwa watanzania tu bali hata mbinguni walishakataliwa;

Wewe uwe na moyo wa kuijenga Nchi yetu kwa moyo wa upendo kwa Tanzania na kwa Mungu: Sasa na atukuzwe MUNGU muumba mbingu na nchi yeye aliyetupa kukaa kwenye kiti cha enzi cha Tanzania ili ufanye yaliyo ya akili. Amina na Amina.

Kuzipiga marufuku sio solution, dawa hapa ni kuziongezea kodi maradufu au zaidi kisha kusimamia hizo kodi zilipwe. Maana ukiongeza kodi bila kusimamia ndio unawapa nafasi kina Tiagi Masamaki kuchakachua.

Kodi ikishaongezeka automatically importer atalazimika kuweka bei kubwa ili kufidia kodi kubwa aliyolipa. Bidhaa hizo zikikumbana na bidhaa za hapa zenye bei nafuu automatically zetu zitauzika zaidi.
 
Mtoa mada ni mpuuzi tu, hivi Tanapa wana ufisadi gani/upi? Toa hata mfano wa ufisadi mmoja basi tujue, sio kuunga unga story

Wewe kama hujui kitu kaa kimya wenye akili waweke mambo hadharani! Unatetea ujinga mtupu, Kwa Mtanzania mwenye akili hawezi kusema TANAPA hakuna ufisadi! Tafadhali tupeane muda halafu urudi humu kujitetea, inawezekana kabisa wewe na familia yako ni wanufaika na rasirimali za Taifa na siku zinahesabika wapuuzi nyinyi! Huwezi kusema kusema eti TANAPA hawahusiki na utoroshwaji wa Twiga hai! Wewe unafikiri watu wako kimya hawaelewi?
 
Hakuna ufisadi wala nini, hizo ni hearsay tupu. Kuweka rekodi ebu toa aina moja tu ya ufisadi.

Kukusaidia tu Tanapa, Ncaa, game department na halmashauri za wilaya vina jurisdiction tofauti tofauti ktk uhifadhi wa w/pori Tz.

Like wale twiga wanaoaminika waliosafirishwa tanapa hawakuhusika 100%. Ishu ya Tembo ni cross sectoral thing, sio ishu ya tanapa tu
Unafikiri bado kuna mambo ya kuundiwa tume tena! Siku zenu zinahesabika hata kama nmajiandaa kudanganya.
 
Tunakupongeza na tunakuombea Mungu akulinde katika kazi hii uliyoianza ya kutumbua majipu. Mheshimiwa Rais Pombe John Magufufuli, sisi wananchi wako tuna hamu kubwa sana ya kujua juu ya utajiri wetu mkubwa unaotokana na gesi iliyogunduliwa hivi karibuni.

Pia tunataka mwongozo wako juu ya utaratibu wa kugawana hii keki yetu tamu tuliyopewa na Mungu. Tunajua kuna jambo kubwa lililojificha juu ya hii keki, haswa pale mtawala aliyekutangulia akishirikiana na wale watu wanaokulaga Siku zote bila kushiba, walipoibua hoja Kule bungeni kwa hati ya dharura.

Sisi wananchi wako tunaokupenda na kukuamini, tunataka utufafanulie, ule udharura ulikuwa ni wa nini. Na je? Ni lini haswa sisi wananchi wenye nchi yetu tutanza kuonja hii Keki?.
 
ukiona mtu anazungumzia keki ya nchi ujue ni chadema wanawaza uchumi wa nchi wagawane wao.
na walikataa kuupisha muswada wa sheria ya gass na mafuta wakitegemea wangechukua nchi ili wagawane vitalu bila nyumbu kujua madhara yake
 
ukiona mtu anazungumzia keki ya nchi ujue ni chadema wanawaza uchumi wa nchi wagawane wao.
na walikataa kuupisha muswada wa sheria ya gass na mafuta wakitegemea wangechukua nchi ili wagawane vitalu bila nyumbu kujua madhara yake
inawezekana ww ni mmoja wa wale wanufaikaji wa hati ya dharura. Lakini jua hii nchi ni yetu wote. Kuuliza juu ya mali zetu siyo dhambi!
 
Nani kakwambia kwamba gesi ni yetu?Je Dhahabu ilikuwa yetu?Almasi ya Mwadui ni yetu?
Unajua kuwa tumewapa wageni mali zetu kwa bei ya chee?Juzi kuna Kampuni inaitwa Swala Energy inatafiti mafuta na imepata gesi inakataa kulipa kodi eti sababu itatumia pesa nyingi,je walilazimishwa?Tuache rasilimali zetu zikae kwani haziozi kuliko kutupa kwa bei ya chee,tuangalie mataifa yaliyofanikiwa kama Algeria na wengine katika miradi hiyo.
 
Ingawa watanzania wengi wamefurahia ujio wa Magufuli kama Rais wa Jamhuri yetu tukufu, bado kuna wengi wanaona kama swala la utawala bora na sheria siyo kipaumbele kwa Rais John Pombe. Naomba nitofautiane kidogo.

1 Kwa nchi yetu ilipofika,bila juhudi za makusudi kutafuta na kuimarisha vyanzo vya mapato hatuwezi kutoboa kama taifa. Kama alivyosema Rais Magufuli, Mafisadi wana nguvu sana nchi hii. Inahitaji ujasiri wa kipekee kupambana nao. Kama mnakumbuka Pinda aliwahi kusema kwamba kuna watu ukiwagusa nchi itayumba!Just imagine....the Prime Minister saying that.

2. Wengine wanadiriki kusema kwamba TZ siyo TRA na Bandari tu. Aangalie na kwingine. Sahihi kabisa. Lakini hivi niulize.....hizo program zote alizoahidi atazitekeleza vipi bila kuwa na pesa? Naamini kabisa akisimamia bandari na TRA......tutapata hela ya kupambana na changamoto za taifa letu. Kiukweli Magufuli ameonyesha kwa vitendo kwamba inawezekana. Ofcourse tuna vyanzo vingi vya mapato. Lakini tujue kabisa huu ni mwanzo.

3. Approach ya Magufuli kufukuza hawa watendaji corrupt na wazembe ni swala la kuungwa mkono. Hivi kuna utawala wa sheria unaoruhusu watu kuiba na kuwa wazembe maofisini? Sasa kati ya hao watendaji wabovu na Magufuli nani hafuati utawala wa sheria? Kiuhalisia wengi wanaolilia the so called utawala wa sheria wanafanya hivo kinafiki. Wanajua kabisa kwamba the so called utawala wa sheria wa kuzungusha kesi mahakamani miaka kumi na zaidi ndo umetufikisha hapa. Na wanajua kabisa bila Ujasiri wa Magufuli mafisadi papa watapeta daima.

4. Magufuli has a vision. Tumpe nafasi. Tumuunge mkono.

Masanja
 
Nani kakwambia kwamba gesi ni yetu?Je Dhahabu ilikuwa yetu?Almasi ya Mwadui ni yetu?
Unajua kuwa tumewapa wageni mali zetu kwa bei ya chee?Juzi kuna Kampuni inaitwa Swala Energy inatafiti mafuta na imepata gesi inakataa kulipa kodi eti sababu itatumia pesa nyingi,je walilazimishwa?Tuache rasilimali zetu zikae kwani haziozi kuliko kutupa kwa bei ya chee,tuangalie mataifa yaliyofanikiwa kama Algeria na wengine katika miradi hiyo.
Mkuu uko sawa kabisa. Ila kwa awamu hii ya huyu mtumbua majipu Imani yetu inaanza kurudi, Nina Imani Mali za wananchi zitarudi mikononi mwetu.
 
Ushauri wangu wa sasa kwa Mh. Rais ni kutokuchagua idadi kuubwa ya mawaziri,achague tu mawaziri wachache ila wachapakazi watakaoendana na kasi yake na kumsapoti.
 
Huu uzi ni maalum kwa ajili ya kutazama baadhi ya watanzania ambao sio wabunge ama hawapo kwenye mifumo rasmi ya kisiasa! Lakini sehemu walipo wanatenda kwa uweledi mkubwa sana kujenga taifa lao.

Please kama unamfahamu muandike hapa na sifa zake. Kwa kuanzia tu kuna yule mwanasheria wa NEMC. Sasa, endeleeni. Huu uzi una maana kubwa sana!

Karibuni!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom