Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
aanze kuwatimua kazi wote waliokuwa nje ya ofisi jana huko w.fedha.
 
Furaha yangu sio ushindi wa CCM ... Ni ushindi wa Mgalatia .... Katika vipindi vinne ya taasisi ya uraisi watz tumeshuhudia Wavaa njiwa na wapiga soga mkiharibu nchi yetu, safari hii kaingia tena mwenye UCHUNGU na Tanganyika...... Mtaisoma namba.

Hongera sana.

Huko hunipeleki kwa sasa. Nnaiheshimu sheria ya mtandao ya kutoeneza chuki za kidini kama ufanyavyo.

Hatum-judge mtu kwa dini yake tunam-judge mtu kwa vitendo vyake.
 
Hongera sana.

Huko hunipeleki kwa sasa. Nnaiheshimu sheria ya mtandao ya kutoeneza chuki za kidini kama ufanyavyo.

Hatum-judge mtu kwa dini yake tunam-judge mtu kwa vitendo vyake.

Haaaaaaa unajifanya umekomaaa sasa 👅👅👅👅👅 jinga sana wewe....

Mtaisoma namba toka kwa Mgalatia
 
Ni bora Mh.rais wetu ukafuata ushauri wa rais kagame,na ukautupilia mbali ushauri wa marais wetu wastaafu,kwa tuanaamia tactic zao ni zile-zile.

UFANYAJI KAZI WA BANDARI ZETU NI WA CHINI YA KIWANGO!

MF; Bandari y'a Dar inaoperate kwa only 60% y'a uwezo wake kwa sa sa,ipeleke ifike 100% alkadhalka tanga inaoperate kwa 15% ipelekee ifikie 100%
na Mtwara vilevile ambayo inaoperate kwa 10% y'a uwezo wake!
 
Na ikiwezekana tupilia mbali ile ya kule naniliu,inaongeza tu deni la taifa na itaziua hizi nyingine kwa faida ya wachina
 
Kama kweli huyo mungu wako kakupa ujumbe bs atakuwa amekupa na njia ya kuufikisha. Kama alisahau bs mkumbushe! Ila MUNGU wangu akinipa ujumbe huwa ananipa na njia ya kuufikisha!
 
Ilikuwa Rais kukutana na mgombea urais kuliko Rais...
 
China nao walipata ujumbe kutoka kwa Mungu huyu huyu?
 
Umechelewa jamvini, karamu imeshaliwa.

Magufuli ameshaanza kazi na kishaanza na mengi sana kuliko unavyotarajia.

Dot com wanasubiri eti watangaziwe ndo wataelewa kuwa mh. tayari yuko katikati ya safari yake
 
Rais ndio huyo tena ameshaapishwa, waliomtaka na wasiomtaka ila wote hawa ndio rais wao wa awamu ya tano.

Je, wewe raia ungependa rais aanze na jambo lipi kulitendea kazi au kulisimamia ambalo unaona ni la muhimu na kwa sababu zipi?

Autangazie UMMA wa watanzania kuwa hakushinda kihalali bali Lubuva na Kikwete walimbeba kibabe na kumtangaza mshindi.

Kwa kuwa umetumwa hapa ama umejituma na pengine utapeleka mrejesho, mwambie wazi miongoni mwa Marais walioingia records Za kukosa uhalali wa kuongoza Tanzania na wananchi wake ni yeye POMBE!

Mwambie, taifa hili linaumwa, lina huzuni kubwa na kuomboleza kwaajili ya udhalimu wa kutisha uliofanywa na Tume ya uchaguzi kwa maagizo ya Kikwete na ccm yao.

Mwambie, usione huu ukimya ukadhani sisi watanzania ni mapompompo na mazuzu!

Mwambie, tunakwenda madhabahuni mwa Mungu kumlilia ili kama huyu Mungu tunaemwabudu Yupo, Hakika haitochukua Muda sote tutakuwa mashuhuda!

Mwambie, tunaenda kumuuliza Mungu hivi yeye Ndio Mkuu au Lubuva ama Kikwete hata waweke mteule wao?
 
    1. Usikubali kofia mbili; wewe ni Raisi, uenyekiti wa CCM muachie mwingine ili chama kibaki chama na serikali ibaki serikali.
    2. Washauri Wabunge wa CCM, watangulize maslahi ya taifa mbele ya maslahi ya chama.
    3. Washauri Wabunge wa CCM kama itawezekana wamchague Spika wa Bunge asiyeegemea upande wowote.
    4. Pokea ushauri kutoka kwa vyama vya siasa lakini uwe huru kufanya maamuzi kulingana na matakwa ya Katiba ukizingatia maslahi ya wananchi.
    5. Usiruhusu Ikulu kutumika kwa maslahi ya CCM, vikao vya chama vifanyike nje ya Ikulu.
    6. Washauri CCM waachie mali za wananchi kwa kuzirudisha mikononi mwa wananchi kupitia serikali.
    7. Agiza vyombo vya dola vitoe haki sawa kwa wananchi bila upendeleo.
    8. Futa sheria zote kandamizi zinazozuia uhuru wa kutafuta, kupokea na kutoa habari. Vyombo vyote vya habari viwe huru.
    9. Hakikisha mikataba yote tunayoingia inawekwa wazi ili vijadiliwe na kupitishwa na Bunge.
    10. Vikumbushe vyombo vya dola kwamba jukumu lao la kwanza ni kuwalinda Watanzania na mali zao na si kupambana nao.



Tanzania tunahitaji:
1. Katiba ya Wananchi / Warioba.
2. Tume huru ya Uchaguzi.

Rais atatawala kufuata katiba ya wananchi. Hawezi kutoka nje ya hapo.
Asipofuata hilo tume huru ya uchaguzi itamfutilia mbali.
 
Pamoja na kwamba sina imani na chama chako, ila naomba unishawishi wewe binafsi katika serikali yako.
Kama ulivyojinaji kuwa serikali yako, yani Tanzania ya Magufuli itakuwa KAZI TU, basi naomba udhihirishe hivyo katika baraza lako la mawaziri.

Kabla hata sijataka kujua waziri mkuu ambaye ataendana na sura ya kauli mbiu yako, lakini nataka usituletee watu hawa ambao walikuwa mzigo kwa taifa na waliolifikisha nchi hapa ilipo chini ya aliyekutangulia pamoja na waziri mkuu wake.

1. Sopteter Muhongo.
Huyu pamoja na kwamba tunaambiwa hakuhusika moja kwa moja kwenye kashfa xa escrow lakini alikuwa kinara wa utetezi katika sakata hili. Pia ni miongoni mwa waziri wenye elimu kubwa lkn hakuwa na mkakati bunifu wa kutatua tatizo la umeme nchini zaidi ya kuiacha tanesco kwenye deni kubwa. Pia ni miongoni mwa viongozi ambao hawathamini wawekezaji wa ndani, anaamini nchi itajengwa na wazungu au wachina.

2. Lazaro Nyalandu.
Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao tumeshuhudia tembo wakiuliwa kwa wingi, na twiga wetu wakisafirishwa kwenda nje, hafai katika serikali yako, kwani atafanya kazi ya mazoeaa ya serikali ya awamu ya 4.

3. Mwigulu Nchemba.
Pamoja na kwamba hakukaa kwenye wizara ya fedha kwa mda mrefu, lkn ni miongoni mwa vijana ambao hawana adabu katika taifa hili. Ni mmoja wa wanasiasa wachanga ambao hajali matamshi yake mbele ya umma, haangalii baada ya hapa athari zake zitanipeleka wapi, sio mstaarabu.

4. Willium Lukuvi.
Huyu kwa mwendo wa kasi inayohitajika nchini hatufai, utendaji wake hauto tofautiana na wa awamu ya 4, hana jipya ndani ya serikali yako.

5. Shukuru Kawambwa
Huyu ni moja ya mawaziri walioshusha thamani ya elimu yetu. Sio mbunifu. Fedha za fidia za rada mpaka leo hatujui matumizi yake yalienda wapi, hatufai kabisaa.

6.Hawa Ghasia.
Huyu mama bado uchama umemkaa kichwani kuliko maslai ya taifa. Hayupo active katika utendaji wake.

7. Jumanne Maghembe.
Huyu ni moja ya mawaziri ambao ndio chanzo cha huduma mbovu za elimu na maji. Elimu yake ni kubwa lkn haina msaada kwetu.

8.Harrison Mwakyembe.
Huyu kinachompa sifa ni lile sakata la richmond ambalo tunamwona kama shujaa. Lakini kiukweli hafai hata kuwa mwenyekiti wa kijiji. Sijaona mafanikio yake katika wizara alizozisimamia, ni mzigo ana asili ya mtandao ambao ni chanzo cha utendaji mbovu nchini. Ni mafya wa kisiasa

9. Magreth Sitta
Mama huyu tangu zama ni outdated, haendani na kasi ya dunia, yupo nyuma na mda, hafai katika serikali yako.

10. Sofia Simba
Hana tofauti na Mama sitta, tena huyu uchama na mtandao wa uongozi umemjaa kichwani, hafai katika serikali yako.

11. Andwer Chenge
Najua huyu unamfahamu vema

12. Anna Tibaijuka
Najua unamfahamu vizur

13. Willium Ngeleja
Najua wamfahamu vzr

NB.
1. Mheshimiwa Rais kuna vijana wengi ambao naamini katika utendaji wao lkn siamini kundi lake, na mmoja wao ni Januari Makamba. Huyu binafsi namwamini kiutendaji, ubunifu lakini kinachomsumbua ni kutaka madaraka makubwa, kundi lake lililo nyuma yake, Huyu badala ya kuchapa kazi atakuwa anawaza urais baada yako kustaafu. Kwa mtazamo wangu ungemweka kando kwa mda baada ya miaka miwili ndo uumpe majukumu.

2. Kwa kukusaidia mh Rais ni vema ukachagua mawaziri wachache ambao wengi wao hawakuwa mawaziri, sio viongozi katika chama, vijana, wenye elimu isiyo na shaka. Hawa ndio wataileta tanzania mpya ya HAPA KAZI TU.

Mh Rais ukikosea kwenye baraza la mawaziri basi jua umeuwa nchi, na hapo tutadhibitisha kuwa hakuna cha Magufuli 4 change itakuwa ccm ni ile ile.

Asantee.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom