Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Kwenye kusema ukweli. Ni moto au baridi?

Mzee Tupatupa
Unashindwa kujielewa kuwa upinzani unaoutetea hauna dira na umepotea.

Kamwambie Mbowe aache utemi aliojipatichika na hataki agushwe.

Magu hajakuja kubadili kawaida ya chama ila taifa. Akipewa utapoteza nini? maana inajulikana hivyo. Kwa Mbowe katiba inaruhusu ila yeye harusu.
 
Wewe VUTA-NKUVUTE tatizo lako ni nini? Unaogopa nini Magu akikabidhiwa chama? Ni vyema kuendeleza BAVICHA kuliko kurukia mambo ya CCM ambayo CDM wameyashindwa. Ngoja tuweke kwa ufupi hapa uozo wa katiba ya chama kinachojinadi cha demokrasia.
Mosi, ukomo wa madaraka, nafasi ya uenyekiti CDM ni nafasi ya kifalme, unaruhusiwa kuishika hadi uchoke mwenyewe, ingekuwa hii kitu ipo kwenye katiba ya CCM au ya Tz kuna nyumbu wangejidai wanaipenda sana demokrasia ila kwa kuwa ipo CDM, nyumbu wote wapo kimya.

Pili, sheria kandamizi dhidi ya uhuru wa mwanachama wa CDM kwenda mahakamani, katiba ya CDM inawakandamizi wanachama wake, ukienda mahakamani kuishtaki CDM, na ukashindwa kesi ni umejifukuzisha uanachama, hii ni sheria kandamizi tena kwa chama kinachojinasibu katika demokrasia ya kweli, ndio kitanzi hichi hichi walikitumia kumuondoa ndugu Zitto, he CDM ni chama cha demokrasia?

Tatu, tumeshuhudia CDM wakitumia muda mwingi wakituhumu watu kutofuata sheria au katiba, je CDM wanafuata na kuheshimu katiba yao? Kutokuwepo kwa watu wanaowazonga zonga CDM haimaniishi ni wasafi, ila bado hawajapata umuhimu wa kukosolewa katika mizania sawa na CCM, mfano mdogo tu ni katiba ya CDM inasema wazi Nafasi ya katibu mkuu lazima ijazwe ndani ya miezi mitatu baada ya kuachwa wazi, je kwa nini hii sheria haikufuatwa au kina Lisu wanajua kunyoosha kidole kimoja kwa CCM tu?
 
mzee Tupatupa wa Lumumba, unataka kutueleza kwamba huko nyuma walikosea walivyokuwa wanapeana au unatuposha hapa. Na pele mwenyekiti aliyekuwepo anataka kuachia madaraka mapema , si uchanguzi lazima ufanyike ili kuziba pengo lange? Kwa hiyo bado JPM anaweza kuwa mwenyekiti June. Naona mzee mwenzangu ngojea utumbuliwe tu JMP anakuwa mwenyekiti anza kufanya mazungumzo na chadema wakupe hifathi kama mzee L.
 
R
mzee Tupatupa wa Lumumba, unataka kutueleza kwamba huko nyuma walikosea walivyokuwa wanapeana au unatuposha hapa. Na pele mwenyekiti aliyekuwepo anataka kuachia madaraka mapema , si uchanguzi lazima ufanyike ili kuziba pengo lange? Kwa hiyo bado JPM anaweza kuwa mwenyekiti June. Naona mzee mwenzangu ngojea utumbuliwe tu JMP anakuwa mwenyekiti anza kufanya mazungumzo na chadema wakupe hifathi kama mzee L.

Sawa kabisa. Huyu hatakubali kukabidhiwa. Atagombea na makada wengine.

Mzee Tupatupa
 
umeshindwa kumshauri mbowe na lowasa ndio utaweza kumshauri magu?
 
Kama Rais wetu JPM atapita kwenye uzi huu namuomba atafute vitabu vya historia vinavyoeleza historia ya viongozi waadilifu duniani waliowahi kutokea kipindi hicho, ninaimani atajifunza mengi kutoka kwao na kwakua lengo lake ni KUMTANGULIZA MUNGU mbele katika kutetea maslahi ya wale anaowaongoza basi ausome utawala wa Umar bunil khatwaab. Nahisi Mheshimiwa anataka kuelekea huko. Nimekupa ramani ya safari yako. Mungu akusaidie ufike salama safari hiyo, wewe ni kiongozi na si mtawala. japo umar R.A alikuwa ni kiongozi wa waislam, jikaze uyasome mambo yake aliyowafanyia raia wake katika uadilifu utajifunza. au kama hutapata muda wa kumsoma basi msikilize Shk. Othman Maalim katika mawaidha yake ameilezea kinagaubaga historia y umar Al faarouk. Wale waumini wa dini zingine nanyi mko huru kumsaidia Rais kwa kumpa reference zingine kulingana na sampuli ya utawala wake.
 
Ungetuelezea angalao kwa kifupi hicho kitabu kinazungumza mambo gani ungekuwa umetusaidia sana pamoja na Raisi
 
Kwa wale wajuvi wa mambo ya Imani wanajua kuwa Mungu ana namna mbalimbali za kutenda kazi zake.

Imeshathibitishwa kuwa Mh Rais wetu Ni Mpango wa Mungu kwa sababu amekuja wakati mwafaka ili kuwatia matumaini watanzania waliokwisha kukata tama....Amekuja ili kuwapa matumaini makubwa kwama siku Moja Hali ya Umasikini,Mateso,Ukosefu wa Demokrasia ,Wizi,Ufisadi na Rushwa zilizojaa katika taifa zikiongozwa na Chama aachokiongoza cha CCM zitaenda kwisha siku moja

Hivyo ni wajibu wetu kuendelea kumwombea sana katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa Sababu yeye ni yule anayekuja kama Nabii wa Mwisho kabla nchi yetu haijaingia katika neema ya milele.

Utawala wake ndio utakuwa wa mwisho katika tawala zile kubwa zilizodumu kwa muda mrefu wa karibu Nusu Karne.Hii ndio Itakuwa Turning Point ya Watanzania.

Naam ujumbe huu ni kwa wale waliojazwa na akili na maono ndio wanaoweza kuuvumbua
 
Labda mungu ila si Mungu
Huyu anaetaka watu waishi kama mashetani atakuwaje mpango wa Mungu?
 
ushawanasa sasa wazee wa kusifia wanaanza kumwagika usiku wa leo watalala vizur sna hizi ndo habar wanazozipenda.

mkuu umewazunguka wenzio hapa najua sio lengo lako unawapima kwa ulichokiandika.
 
naunga mkono acha mifisadi haikomeshe na kuishikisha adabu, magu oyeeeeeeeeee
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom