Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Kabla ya kilio cha kuadimika kwa madawa katika mahospitali yetu hakijaisha, sasa kimeibuka kilio kingine cha wanafunzi wengi wa vyuo vikuu kukosa mikopo na hivyo kuendelea kuongeza lawama kwa serikali.

Mh.Raisi,lawama hizi kwa mtazamo wangu si za lazima kabisa bali ni za kujitakia tu kwa nyinyi kushindwa kuwa na vipaumbele na zaidi watu kutaka kuishi maisha ya anasa kwa gharama ya serikali,serikali ambayo teyari ina mzigo mkubwa wa kuhudumia wananchi wake.

Mh.Raisi,mimi nina ushauri mmoja tu kwako juu ya namna bora na ya haraka ya kumaliza tatizo hili bila hata kuathiri bajeti ya serikali wala kuhamisha mafungu na mambo mengine ya aina hiyo.

Mh.Raisi,unachotakiwa ni kufanya maamuzi magumu ya kufuta sitting allowance za wabunge na kuondoa magari ya anasa maarufu kama mashangingi serikalini.

Unachotakiwa ni kupeleka muswaada /mapendekezo Bungeni katika Bunge lijalo la November au January mwakani ya kuwataka wabunge waachane na malipo haya ya sitting allowance ili fedha zitakazookolewa zikahudumie watoto wa masikini pamoja na kuboresha huduma za jamii.

Malipo haya jamani ni ya aibu kwa wanasiasa waliotuomba kura kwa lengo la kutetea masikini na wanyonge wa nchi hii.Hivi nyinyi watu hata nafsi zenu haziwasuti kuendelea kulipwa fedha hizi?Mbona mwalimu au Police traffick hana kitu kinachoitwa standing standing allowance?Nyie huu uhalali wa kujilipa fedha hizi mnaupata wapi?!

Mh.Raisi,nina hakika hakuna atakaepinga hadharani pendekezo hili kwani hata wao nafsi zao zinawasuta kupokea fedha hizi ila tu imekosekana nguvu ya kupendekeza jambo hili lifike mwisho.

Mh.Raisi,eneo lingine ni hili la matumizo ya magari ya anasa maarufu kama mashangingi kwa mawaziri na viongozi wengine waandamizi serikalini.

Magari haya mbali na kuwa yananunuliwa kwa gharama kubwa,lakini hata gharama ya kuyahudumia ni kubwa mno kuanzia mafuta,vipuri,service,n.k.

Hivi kuna ulazima gani wa waziri,naibu waziri,makatibu wakuu,wakurugenzi wa taasisi na mashirika ya umma, wakuu wa mikoa,wilaya,vigogo wa polisi,magereza, na jeshi wote kutumia magari haya?

Hivi Land Cruiser Mkonge New Model haziwatoshi?Anasa za aina hii katika ya umasikini huu kwa faida ya nani?Nani atakaethubutu kupinga hili?Atakaekupinga kwanini usimfukuze?

Mh.Raisi,kaa na watendaji wako kisha mfanye tathimini juu ya kutekeleza uamuzi huu na zaidi muweke timeframe ya kutekeleza mpango huu.

Mh.Raisi,maamuzi ya aina hii ndio tunayoyata.Huu ndio udikteta tunaouhitaji na sio ule wa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na mambo mengineyo yanayafanana na hayo.

Fedha zitakazopatikana zilelekeza kwenye huduma za jamii kama vile kununulia madawa na vifaa tiba,ujenzi wa madarasa,kukopesha wanafunzi wa elimu ya juu,n.k.

Mh.Raisi,hebu jiulize bei ya shangingi moja ingesomesha watoto wangapi wa masikini vyuo vikuu?

Mh.Raisi,kama mliona kuhudumia nyumba za serikali ilikuwa ni gharama mpaka mkaamuza kuziuza, kinawashinda nini kwenye mashangingi haya?

Hivi katika mataifa tajiri na yaliyoendelea,viongozi waandamizi serikalini wanatumia magari haya haya ya gharama?

Naamini hata UkAWA waliposema elimu bure mpaka chuo kikuu,vichwani mwao walikuwa na policy za aina hii sera ambazo nyinyi zimewashinda kwa kukosa dhamira na uthubutu tu.
Hivi unajua muda unaotumia shangingi from dar to dom au maeneo mengine??? Kinachomatter ni comfort na muda wa kufika kwenye ziara zao... hivi umtoe wazir dodoma to mtwara kwenye mkonga??? Hahaha sasa atakuwa ana tofauti gani na mkuu wa kitengo??? Acha wale maisha ili na wewe ufight uje uyakute hayo mambo... imagine ungekuwa wewe waziri je ungeshauri hivyo?? Suala la sitting allowance kikwazo ni wabunge wa ccm kwani wao kwa wingi wao ndio wenye nguvu ya kujenga hoja ya kuindoa hiyo kitu. But kumbuka ndio mshahara wao na perdiem hiyo...
 
Mbunge anapokea 12 milioni kwa mwezi. ..hivi iyo pesa wanaweza kukopeshwa wanafunzi zaidi ya watatu kwa mwaka
 
Hivi unajua muda unaotumia shangingi from dar to dom au maendeo mengine??? Kinachomatter ni comfort na muda wa kufika kwenye ziara zao... hivi umtoe wazir dodoma to mtwara kwenye mkonga??? Hahaha sasa atakuwa ana tofauti gani na mkuu wa kitengo??? Acha wale maisha ili na wewe ufight uje uyakute hayo mambo... imagine ungekuwa wewe waziri je ungeshauri hivyo?? Suala la sitting allowance kikwazo ni wabunge wa ccm kwani wao kwa wingi wao ndio wenye nguvu ya kujenga hoja ya kuindoa hiyo kitu. But kumbuka ndio mshahara wao na perdiem hiyo...
Ndio maana huwa sitoi michango ya madawati ma vitu vingine vya aina hiyo.
 
Kabla ya kilio cha kuadimika kwa madawa katika mahospitali yetu hakijaisha, sasa kimeibuka kilio kingine cha wanafunzi wengi wa vyuo vikuu kukosa mikopo na hivyo kuendelea kuongeza lawama kwa serikali.

Mh.Raisi,lawama hizi kwa mtazamo wangu si za lazima kabisa bali ni za kujitakia tu kwa nyinyi kushindwa kuwa na vipaumbele na zaidi watu kutaka kuishi maisha ya anasa kwa gharama ya serikali,serikali ambayo teyari ina mzigo mkubwa wa kuhudumia wananchi wake.

Mh.Raisi,mimi nina ushauri mmoja tu kwako juu ya namna bora na ya haraka ya kumaliza tatizo hili bila hata kuathiri bajeti ya serikali wala kuhamisha mafungu na mambo mengine ya aina hiyo.

Mh.Raisi,unachotakiwa ni kufanya maamuzi magumu ya kufuta sitting allowance za wabunge na kuondoa magari ya anasa maarufu kama mashangingi serikalini.

Unachotakiwa ni kupeleka muswaada /mapendekezo Bungeni katika Bunge lijalo la November au January mwakani ya kuwataka wabunge waachane na malipo haya ya sitting allowance ili fedha zitakazookolewa zikahudumie watoto wa masikini pamoja na kuboresha huduma za jamii.

Malipo haya jamani ni ya aibu kwa wanasiasa waliotuomba kura kwa lengo la kutetea masikini na wanyonge wa nchi hii.Hivi nyinyi watu hata nafsi zenu haziwasuti kuendelea kulipwa fedha hizi?Mbona mwalimu au Police traffick hana kitu kinachoitwa standing standing allowance?Nyie huu uhalali wa kujilipa fedha hizi mnaupata wapi?!

Mh.Raisi,nina hakika hakuna atakaepinga hadharani pendekezo hili kwani hata wao nafsi zao zinawasuta kupokea fedha hizi ila tu imekosekana nguvu ya kupendekeza jambo hili lifike mwisho.

Mh.Raisi,eneo lingine ni hili la matumizo ya magari ya anasa maarufu kama mashangingi kwa mawaziri na viongozi wengine waandamizi serikalini.

Magari haya mbali na kuwa yananunuliwa kwa gharama kubwa,lakini hata gharama ya kuyahudumia ni kubwa mno kuanzia mafuta,vipuri,service,n.k.

Hivi kuna ulazima gani wa waziri,naibu waziri,makatibu wakuu,wakurugenzi wa taasisi na mashirika ya umma, wakuu wa mikoa,wilaya,vigogo wa polisi,magereza, na jeshi wote kutumia magari haya?

Hivi Land Cruiser Mkonge New Model haziwatoshi?Anasa za aina hii katika ya umasikini huu kwa faida ya nani?Nani atakaethubutu kupinga hili?Atakaekupinga kwanini usimfukuze?

Mh.Raisi,kaa na watendaji wako kisha mfanye tathimini juu ya kutekeleza uamuzi huu na zaidi muweke timeframe ya kutekeleza mpango huu.

Mh.Raisi,maamuzi ya aina hii ndio tunayoyata.Huu ndio udikteta tunaouhitaji na sio ule wa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na mambo mengineyo yanayafanana na hayo.

Fedha zitakazopatikana zilelekeza kwenye huduma za jamii kama vile kununulia madawa na vifaa tiba,ujenzi wa madarasa,kukopesha wanafunzi wa elimu ya juu,n.k.

Mh.Raisi,hebu jiulize bei ya shangingi moja ingesomesha watoto wangapi wa masikini vyuo vikuu?

Mh.Raisi,kama mliona kuhudumia nyumba za serikali ilikuwa ni gharama mpaka mkaamuza kuziuza, kinawashinda nini kwenye mashangingi haya?

Hivi katika mataifa tajiri na yaliyoendelea,viongozi waandamizi serikalini wanatumia magari haya haya ya gharama?

Naamini hata UkAWA waliposema elimu bure mpaka chuo kikuu,vichwani mwao walikuwa na policy za aina hii sera ambazo nyinyi zimewashinda kwa kukosa dhamira na uthubutu tu.
Sasa kama pesa hakuna wauze shangingi wamuuzie nani sasa kama baba analalamika njaa watoto jee ...
 
Kwaio unataka magufuli ageuke bunge maana hio sheria si itabidi iridhiww na hao wabunge? ambao wataikataa, mkulu atageuka legislature n executive....
 
dah.. mkuu ungepata kachanc ka sekta ya kumshauri na kumshawishi ili akubali nazan tungekua mbali kidogo... ila tuishi kwa matumaini kwamba ujumbe utafika
 
Mh Rais nimejiuliza maswali mengi magumu juu ya hatma ya Tanzania chini ya utawala wako. Ni ukweli usiopingika kuwa Wasukuma wana uzoefu mkubwa wa utawala kutokana na mfumo tulilipitia wa Kitemi.

Kwa upande wangu toka moyoni mwangu kwa mfumo unaotumia kiutawala una matokeo hasi zaidi kuliko chanya. Kwanza mipango ulinayo ni mizuri kwa taifa hili lakini Urais una ukomo, ungekuwa ni utawala wa kifalme matunda yako tungeyafurahia.

Pili impact ya maendeleo kwa wananchi wa kawaida ni ndogo sana. Kulalia huko ni sawa na Herode alichofanya kwa kumwadhibu Yesu ili awafurahishe Wayahudi.

Tatu kutrain wasomi sana katika siasa ni kazi.Uhalisia unaonyesha wengi wao si wa kweli.

Nne walio upande wako ni wachache.Namanisha wapo hapo kwa ajili ya mishahara.

Tano washauri wako wameufanya uongozi wako kuwa mgumu. Hapa pana changamoto kubwa.

Sita nakushauri huu ni wakati wako wa kutekeleza kauli mbiu yako ya Hapa Kazi tu kwa vitendo.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Sisi wanaume wa kiafrika kuwa na wanawake watatu, wanne au watano ni jambo la kawaida Sana....
 
Nature ya mtu ni vigumu kuibadilisha kwa muda mfupi but as time goes watu watajifunza kitu na Ku shape their mind baada ya kuona output waliyoitarajia ni tofauti na kama jinsi walivyofikiri hivyo kuwa na subira muda ni mwalimu mzuri
 
Leo tarehe 19 Oktoba 2016; hapa jamii forum pekee zaidi ya post 5 plus hii yangu nimeziona zikiongelea chuki ya wananchi dhidi ya utawala serikali.

Potelea mbali waweza kusema ni propaganda za wapinzani na mafisadi kama ilivyoada kutoa majibu mepesi kwa maswali na mambo mhimu yanayohitaji uangalizi mkubwa, ila kuna jambo mh. Rais kama uko makini bila shaka ulitakiwa kuwa umeligundua, fuatilia matukio ya na mlio wa ngoma (maoni ya wananchi utaelewa).

Zilianza tetesi za mizigo bandarini likapita.

Ikaja mtikisiko wa uchumi BOT wakakanusha.

likaja issue ya deni la taifa BOT watakakanusha,

likaja issue ya maisha magumu na kupotea kwa pesa ukasema mafisadi wameficha pesa,

likaja ukosefu wa dawa mkasema hakuna tatizo,

likaja tatizo la mikopo ya wanafunzi bado galina majibu ya kutosha,

Walimu wametoa siku 15 unaona km mzaha tu, kuna issues ya watu kushushwa madaraja kiukweli linamkera kila mtumishi.

Chukizo la kila kijana ni AJIRA KUSITISHWA LINAMPA KICHEFUCHEFU na HASIRA kila kijana maana ni muda ambao vijana wengi hawajui mstakabali wa maisha yao.

Serikali tutasema mengi na kujitahidi kujivua majukumu mengi ila twende turudi bado serikali inalo jukumu la kupanga msitakabali wa wananchi (vijana) wake. Huwezi kusema tukalime pasipo kujua tukalime wapi? Tulime nini? na kulime kupeleka wapi? Juzi kati mwezi wa 8 na 9 tumeshuhudia nyanya zikioza, hapa naongea ila walima tikitiki wanajua machungu waliyonayo moyoni.

Mh. Rais ebu sumbua kichwa kubuni mikakati ya ajira URAIS si rahisi kuna kichwa majibu rahisi hayawezi kutufanya tukuone kama baba. Kutana na vijana na watu wakushauri binafsi siamini kama wewe pekee unaakili ya kutatua matatizo yote ya nchi hii.

Narudia kutana na vijana tukupe mawazo yetu ujue wapi tumekwama na wapi usaidie tusonge mbele.
 
Leo tarehe 19 Oktoba 2016; hapa jamii forum pekee zaidi ya post 5 plus hii yangu nimeziona zikiongelea chuki ya wananchi dhidi ya utawala serikali.

Potelea mbali waweza kusema ni propaganda za wapinzani na mafisadi kama ilivyoada kutoa majibu mepesi kwa maswali na mambo mhimu yanayohitaji uangalizi mkubwa, ila kuna jambo mh. Rais kama uko makini bila shaka ulitakiwa kuwa umeligundua, fuatilia matukio ya na mlio wa ngoma (maoni ya wananchi utaelewa).

Zilianza tetesi za mizigo bandarini likapita.

Ikaja mtikisiko wa uchumi BOT wakakanusha.

likaja issue ya deni la taifa BOT watakakanusha,

likaja issue ya maisha magumu na kupotea kwa pesa ukasema mafisadi wameficha pesa,

likaja ukosefu wa dawa mkasema hakuna tatizo,

likaja tatizo la mikopo ya wanafunzi bado galina majibu ya kutosha,

Walimu wametoa siku 15 unaona km mzaha tu, kuna issues ya watu kushushwa madaraja kiukweli linamkera kila mtumishi.

Chukizo la kila kijana ni AJIRA KUSITISHWA LINAMPA KICHEFUCHEFU na HASIRA kila kijana maana ni muda ambao vijana wengi hawajui mstakabali wa maisha yao.

Serikali tutasema mengi na kujitahidi kujivua majukumu mengi ila twende turudi bado serikali inalo jukumu la kupanga msitakabali wa wananchi (vijana) wake. Huwezi kusema tukalime pasipo kujua tukalime wapi? Tulime nini? na kulime kupeleka wapi? Juzi kati mwezi wa 8 na 9 tumeshuhudia nyanya zikioza, hapa naongea ila walima tikitiki wanajua machungu waliyonayo moyoni.

Mh. Rais ebu sumbua kichwa kubuni mikakati ya ajira URAIS si rahisi kuna kichwa majibu rahisi hayawezi kutufanya tukuone kama baba. Kutana na vijana na watu wakushauri binafsi siamini kama wewe pekee unaakili ya kutatua matatizo yote ya nchi hii.

Narudia kutana na vijana tukupe mawazo yetu ujue wapi tumekwama na wapi usaidie tusonge mbele.
Nimekuelewa sana mkuu
 
Rais pitia hapa uone vijana wako tulivyo makini nawe!

umetuliza vijana kwa mengi ,ajira na,mikopo kwa wanavyuo ,
 
Kuna vijana wapo wamemzunguka Kama vile makonda, hapi na gumbo wanatosha
 
Hakika umenena mkuu, JPM ausome huu uzi na kuufanyia kazi, asiwaletee watu maisha ya kikoloni hii nchi ni ya watanzania wote, wote tuna hati miliki halali.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom