Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Hao misukule wa lumumba hawana uwezo wa kutoa hoja hizo zaidi kuishia kusifia kila kitu.

Mikataba yote ya madini,gesi na mafuta iwekwe wazi na ijadiliwe live bungeni
 
Unafikiri hapo Rais angepata shida ya kujisubua na watu walioweka matumbo yao mbele kuliko ubinadamu. Hawa vijana wapo mazoezini, mwenye uwezo wa fitna, uwongo, mpiga blabla, anaeweza kumzibiti anasema ukweli ndio wenye uwezo na anaaminiwa kwelikweli.

Sio hao vijana tu hata wabunge wa ssm aijui wanajisikiaje jinzi Lissu anavyowashushia nondo. Inawezekana ndio ajira ngosha kauli mbiu yake fukuza kazi tukanunue ndege za kwamda chato.

Baba yao si aliona watu wengine ni vilaza. Sasa mungu karudisha kinyume chake. Nasikia hata wale sijui wa nyumba kumi kauli zao zinapingana na za baba yao.
 
Hii thread iwe Maalum kwa Maoni, Ushauri na Mapendekezo mbalimbali kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Mimi namuomba, Mheshimiwa Rais mteuliwa, kwa heshima na taadhima hili ni ombi binafsi kwako.

Nnaomba uhakikishe huyu mrembo wa ACT Bi Anna Mghwira unamuingiza bungeni na unampa wadhifa anaostahiki, huyu mama ni kichwa adhyim na adim kabisa.

Nimemfatilia mikutano yake mingi sana ya kampeni, anatoa vitu kichwani utafikiri ana word processor inayopanga na kuchuja anachokizungumza kutoka kichwani bila kusoma.

Halikadhalika leo kanifurahisha sana alipostukizwa na kutoa hotuba pale Diamond, ilikuwa fupi na imelenga points zote nzuri na ameeleweka vyema kabisa.

Anna heko sana na nitakuunga mkono katika siasa zako.
























Faizafoxy wewe umezawadiwa cheo gani?
 
Kufuatia nchi kupata misuko suko ya aina mbali mbali kwa zaidi ya miongo 3 , kama ukwepaji wa kodi, uhujumu wa mali za taifa kama mkataba kia aka kadco, loliondo gate n.k pamoja na mikataba ya madini na mengineyo , hata ktk mambo ya import and export ni vizuri nchi ikaanzisha kitengo kama hicho chenye watu wenye ueledi ktk nyanja za biashara, uchumi,kodi , uhasibu, elimu, science , na hata mipango miji ilituweze kupanga nchi kuwa na uchumi na maendeleo endelevu
 
Heko nyingi kwako mh.Raisi kwa kupambana na wahujumu.

Bila maneno mengi yakupoteza muda ninashauritu kwamba kwenye baraza la mawaziri usimsahau Bashe maana huyo mheshimiwa anaonekana kuwa na uchungu na rasilimali zetu

Pia kwa uongozi mzuri wa mh.Zungu,hekima na aina ya kumaliza hata mivutano ndani ya mhimili naomba umuone

Inawezekana kunamakosa wamefanya kama binadamu yakiwemo ya kukikosoa chama dola bali ninaona wanastahili kupewa nafasi kwasasa ilinao wawatumikie watanzania.
 
Awali ya yote niungane na wote wanaomuombea kamanda Lissu Mungu ampe afya na apone haraka na kurudi kwenye uwanja wa mapambano. Kwa mara ya kwanza, mara nilipopata taarifa hizi, nilikuwa na wanangu wawili, niliwataka tumwombee Lissu, na mwanangu mmoja aliongoza sala hiyo. Sijawahi kufanya kitu kama hicho kwa kweli, ila kwa Tundu Lissu, niliona kuna haja ya kufanya hivyo, na hata Zaidi.

Sasa tuje kwenye mada. Rais wetu, JP Magufuli, pamoja na nia nzuri aliyo nayo ya kuondoa maovu katika nchi hii na kuiwezesha kufaidi rasilimali zake, kuna huu utaratibu wa kutumia nguvu nyingi, kuwabana wengine wasifanye siasa abaki peke yake, kuendesha utawala ambao yeye mwenyewe aliwahi kukiri kwamba anapenda "kutumia rungu". aliyasema haya alipokuwa akiongea mbele ya Rais wa Zambia, ambaye ana jina la "Lungu". alimwomba wabadilishane jina, ampe jina lake la "Pombe" kwa sababu yeye Magufuli hapendi na hatumii Pombe, lakini achukue jina la "Lungu" kwa sababu yeye Magufuli anapenda "kutumia rungu".

Huu utaratibu wa kuongoza nchi namna hii, unafanya upinzani uchukue hatua za kiharakati Zaidi, na ndio maana akina Tundu Lissu wamejitokeza sana. uwanja wa siasa umefungwa, na kwa hiyo kumbi za mahakama na vituo vya Polisi ndio vimegeuzwa kuwa viwanja vya siasa. siyo kwa kupenda, lakini kwa sababu "Nature Abhorrs vacuum". Siyo lazima nchi iwe katika hali ya taharuki namna hii. kwa kuwa "antagonize" wapinzani, yamejengwa mazingira ambapo sasa hivi siasa za vyama vingi ni uadui, badala ya kuwa ni utani, na kusaidiana kujenga nchi. inafikia hatua mpaka tukio kama hili la kupigwa risasi Tundu Lissu, inakuwa vigumu kuamini kwamba serikali haihusiki, kutokana na aina ya mahusiano yaliyopo baina ya upinzani na serikali na CCM yake.

Hata katika maisha ya kawaida, kama mtu anashambuliwa na risasi namna hii, watuhumiwa wa kwanza Polisi inaoanza nao ni wale ambao ni "maadui" za huyu mhanga. wote waliowahi kutoa kauli za vitisho kwake, wanakuwa watuhumiwa. hiyo ni kadiri ya utaratibu wa kawaida kabisa wa kipolisi. na inaleta ukakasi kusikia vyombo vya dola, viongozi wa serikali, pamoja na Rais mwenyewe, spika Ndugai na wengine kama hao, wakitoa kauli za "pole" na kulaani tukio. wanaonekana kama wanafanya kejeli tu. kauli kama hizi zinatakiwa ziungwe mkono na aina ya mahusiano ya kila siku yaliyopo kati ya serikali na upinzani. ndio maana napendekeza kwa dhati kabisa, Rais Magufuli ajitafakari. CCM ijitafakari. namna nyingine itabidi serikali ifanye jitihada kubwa kumlinda Tundu Lissu, maana akipata tatizo lolote, itakuwa vigumu sana kwa serikali kukwepa lawama
 
Hauna mamlaka ya kumtaka raisi abadirishe system ya uongozi....

Wewe usiyeendana na hii system ndio ubadirike.... cheza kulingana na ngoma inavyopigwa... mbona ngoma ni zile zile tu... mpigaji ndio tofauti.

Tatizo letu wabongo... tuliishi kwa kukariri saaana... tukaamini katika tuliyokaririshwa ingawaje hayakuwa saaawa..... now mambo yamebadirika tumepoteana....

Kaza tu.. ukizoea mlio.. utaenda step sahihi

Sent from "La -Vista"
 
Amani iwe nanyi wadau.
Natumaini mu wazima na mnaendelea vizuri na majukumu yenu Ni vizuri pia kabla ya yote nikatoa pole kwa watanzania wote walioguswa na tukio la kinyama dhidi ya kiongozi wa upinzani Bw Tundu Lissu.

Nikiwa sijaonekana kitambo sana kwenye jukwaa hili leo napenda kusema kuwa kwa yanayoendelea nchini Tanzania kwa sasa, imebidi niamue kujitokeza tu na labda niamue kutoa mchango wangu wa mawazo hata kama hayatasikilzwa lakini nikiwa na Imani kuwa haya mawazo kwa kuwa ni mazuri na yanajenga basi yatasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Sipendi kwenda kwenye hili la Lissu ila kwa kuwa nia yangu ni ya kumsaidia Mh Raisi naona kwa hili la Lissu linaweza kupata utatuzi wake humuhumu.

Kwanza nianze na maana halisi ya wasaidizi wa Mh. Raisi ni kina nani hasa- Kama hamjui kwa Tanzania hawa wanaanzia na baraza la mawaziri ambalo kisheria na kikatiba ndicho chombo kilichopewa mamlaka ya kumshauri Mh. Raisi juu ya mambo yote ya nchi. Kwa hapa Tanzania washauri wengine ni mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na wasaidizi wengine wa Mh Raisi.Wengine ni viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Kwa nini leo nimeamua kuwaelezea hawa watu na kuongea na hawa watu????

Hawa ndo watu wa kumsaidia kumwambia ukweli Mh.Raisi, ukweli wa kiuchumi, ukweli wa kisiasa hata kijamii. Bila shaka kwa hali ilivyo sasa napenda kusema kuwa wasaidizi wa raisi hamfanyi wajibu wenu ipasavyo na inapoelekea nchi itaenda kuanguka chini ya raisi Magufuli. Naomba nielezee kwa mifano hili suala.

KIUCHUMI.

Pamoja na Mh Magufuli kuwa na nia njema kwa nchi hii kiuchumi napenda kusema kuwa mmekuwa mnapotosha vibaya sana Mh. Raisi kiuchumi kiasi kwamba nchi imekuwa ikipata matokeo hasi zaidi kiuchumi zaidi ya chanya.Swali langu kwenu ni kwa nini mmeshindwa kumshauri Mh Raisi juu ya kuanza na njia ya kupiga marufuku vitu wakati mlishaona hili lilianza kuleta matokeo hasi???

Kwenye sukari wasaidizi wa raisi mlipaswa kujifunza sana kwenye suala hili kwa sababu tangu Mh.Raisi apige marufuku uingizaji wa sukari bei ya sukari haijaweza kushuka kuwa kawaida hadi leo hii. Swali langu kwenu hamkujifunza kitu kwenye suala hili???? Hamjui kuwa bei ya sukari hadi leo haijawa kawaida na hili limepelekea nia nzuri ya Mh Raisi ishindwe kuonekana hapa???

Sio tu kwenye sukari, mlishindwa kumshauri Mh Raisi vizuri kwenye pesa kuondolewa kwenye benki za biashara na hadi leo hali ya kifedha imekuwa mbaya sana nchini hasa kwenye mzunguko na upatikanaji wa mikopo.

Kubwa zaidi mliloshindwa kumshauri Mh. Raisi ni hili la Acasia. Hivi ni nani aliwaambia kuwa wazungu unapambana nao kwa mabavu na sio akili? Hamjaona hili suala la Acasia linamuweka Raisi na nchi sehemu mbaya sana kiuchumi? Hivi hamkuona haja ya kumshauri Mh Raisi angeanza na kubadili sheria tena at least kwa kujifanya anawashirikisha hao wawekezaji wa madini alafu badae kunatokea maoni ya wadau ndo tunafikia kurekebisha sheria kwa muktadha tunaoona sie??? Hamkuona hi indo ilikuwa njia sahihi ya kudeal na suala la madini bila kucreate tension kwa dunia juu ya hali ya uwekezaji Tanzania???

Mmemuacha Mh Raisi ametumia nguvu kubwa kudeal na issue ya madini kwa kuzuia usafirishwaji wa makinikia kiasi ambacho kimeleta picha mbaya sana kiuwekezaji hapa kwetu. Kusema kweli mmeiweka Tanzania sehemu mbaya sana kiuwekezaji na pia hata hifadhi yetu ya pesa za kigeni itaathilika sana kwa kuwa kuondoka kwa Acasia msidhani itakuwa raisi kwa muwekezaji mwingine kuja Tanzania kama amefikiria vizuri kwenye kucalculate risk za kuinvest Tanzania. Kwa nchi yenye miaka mingi ya uhuru hii haikuwa approach tuliyotakiwa kuitumia kwenye kudeal na hawa ngozi nyeupe.

Mnamuacha raisi atamke juu ya vita vya uchumi hadharani. Hivi mmeshindwa kumshauri Mh Raisi juu ya madhara ya nchi kutangaza hadharani vita dhidi ya maslahi yao kiuchumi?? Au mnataka siku ya mwisho nchi itapata nini??? Mnadhani kama nchi itafaidika chochote kwenye vita dhidi ya maslahi ya kiuchumi ya wanamagharibi au wanamashariki??? Hamuoni Zimbabwe?? Hamuoni Venezuela??? Hamuoni Libya na Syria???? Mnataka Magufuli aje kukumbukwa kwa sifa mbaya zaidi????

KISIASA.

Mmeshindwa kumshauri Mh Raisi vizuri kiuchumi na mbaya zaidi hadi kisiasa mnaharibu kwenye kumshauri Mh. Raisi vizuri kiasi ambacho leo adui akitumia siasa kutuvuruga anatumaliza kesho asubuhi tu. Hivi kulikuwa na haja gani ya kumshauri raisi kuwafungulia mashtaka wapinzani kila wanapomsema??? Hamuoni hili linawatengenezea huruma kwa wananchi na siku ya mwisho wananchi kuwasikiliza na kuwaamini wao zaidi kuliko wanavyoiamini serikali au Raisi wao???? Mmeshindwa nini kumshauri Mh. Raisi kuimalisha kitengo cha propaganda na uenezi cha chama chake ili kiweze kujibu kila shutuma dhidi ya Mh.Raisi na siku ya mwisho kuanzia wananchi hadi wageni waone kuwa ni game za kisiasa tu????? Hamuoni kutumia vyombo vya dola kujibu hoja za kisiasa zinamuharibia raisi kimataifa n ahata kuharibu taswira ya nchi kimataifa????

Kwako Mh. Raisi, bado nakuamini sana, kama nilivokupigania kwenye uchaguzi sitaacha kukuigania kwa nia ya kutaka uongoze vizuri. Ila naomba uchague wasaidizi wa uhakika wanaojua dunia inavyoenda na figisu zake na mwisho wape uhuru wa kukushauri kwa weredi.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Kuna uwezekano wa 99% kwamba waliovamia clouds ndio waliofanya jaribio la kumuua Lissu. Siro alipewa u-IGP ili kikosi cha bashite kiweze kutekeleza matendo yake bila bugudha popote nchini. Amani ya nchi hii inaondolewa na bashite.
 
Wapo wapuuzi wata kukebei..... RAIS angewaacha wapinzani wabwabwaje tuuu wangechoka na wangepata relief wapinzani na wananch, lakini kulazimisha watu waweke vinyongo moyoni na wakose pa kusemea siku Rais akipata tatizo itakuwa ni sherehe na nderemo kwa wananch na wapinzani. Rais awaache waseme vinyongo viishe.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom