Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Serikali ya Tanzania inaweza kuongeza kipato kutoka kwenye mitandao ya kijamii ikiwa tu itaanzisha utaratibu wa kuwakata kodi watumiaji wote wa mitandao hiyo kila siku. Inaaminika hapa Tanzania kuna watumiaji wa mitandao ya kijamii milioni 14 kwa siku(14,000,000), hizi takwimu sio, rasmi lakini ikiwa zitafanyika takwimu rasmi idadi hii inaweza kuwa kubwa zaidi.

Ikiwa Serikali yako itaamua kuanza kukata kodi ya sh. 200 tu kwa kila mtumiaji wa mitandao ya kijamii kwa siku, TRA itakusanya sh. 84,000,000,000 (Bilioni 84) kwa mwezi, na kwa mwaka itakuwa sh. 1008,000,000,000 (Trilioni 1 na bilioni 1). Hii ni pesa mingi sana ambayo kama ikikusanywa itaweza kuisaidia Serikali katika kupata pesa za kujenga nyumba za waalimu nchi nzima. Kwa mahesabu haya ya haraka haraka, utaona kuwa hii mitandao ya kijamii ni "migodi" iliyolala.

Mfano ikiwa kila nyumba moja itajengwa kwa sh. 50,000,000 (Milioni 50) basi kwa mwaka zitajengwa nyumba 20,160 nchi nzima na baada ya miaka 5 zitakuwa zimejengwa nyumba 100,800 na hapa tutakuwa tumeondoa tatizo la nyumba sio tu kwa waalimu, bali pia kwa askari polisi, askari magareza, madaktari na wanajeshi wetu. Tena tenda hii ya ujenzi wa nyumba hizi wapewe wanajeshi kama walivyopewa ile tenda ya kujenga ukuta wa Mererani. Na uzuri ni kwamba watumiaji wa mitandao ya kijamii wanaongezeka kila mwaka na hawapungui.

Mheshimiwa Rais Magufuli, nakuomba ulichukue hili wazo na ulifanyie kazi haraka iwezekanavyo kwani huku kwenye mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter, Youtube, Instagram, JamiiForum, snapchat, n.k watumiaji wake, wengi wao wanapesa za kuchezea tu na hazina kazi maalumu. Kuna watu wanashinda kwenye mitandao ya kijamii siku nzima wakipost "ujinga" tu na kutukana wenzao, hivyo itakuwa bora sana kama wakianza kulipia "kodi" maalumu ya kutumia mtandao hiyo kwa siku. Sidhani kama Sh. 200 itakuwa nyingi sana kwa mtu kushindwa kulipia. Mimi binafsi nipo tayari kulipia hiyo Sh. 200 kwa siku.

Mheshimiwa Rais, nchi hii itajengwa na Watanzania wenyewe na hii ni mbinu mojawapo ya Watanzania kuchangia katika ujenzi wa nchi yao. Mitandao ya kijamii siyo chakula wala siyo maji, hivyo atakayeshindwa kulipa hiyo kodi hawezi kufa wala kudhurika kwa namna yoyote ile.

By Son of Gamba.
Kwa nyongeza tu uwekwe ushuru kwa kila mtu atakayepita kwenye barabara kuu alipe sh.100/ mfano Dar ya Kilwa, Bagamoyo, Pugu na Morogoro na zikusanywe kwa kutumia mfumo mpya. Itapatikana pesa ya kutosha kuboresha magereza na nyumba za askari, Tanzania tumejaliwa pesa ipo nyingi sana.
 
Kwa nyongeza tu uwekwe ushuru kwa kila MTU atakayepita kwenye barabara kuu alipe sh.100/ mfano Dar ya Kilwa, Bagamoyo, Pugu na Morogoro na zikusanywe kwa kutumia mfumo mpya. Itapatikana pesa ya kutosha kuboresha magereza na nyumba za askari, Tanzania tumejaliwa pesa ipo nyingi sana.
Tuanze na huku kwenye mitandao ya kijamii kwanza. Huku watu wanachezea pesa tu, bora tuweke kodi hiyo ndogo ili isaidie kujenga taifa kuliko kuziachia hizo pesa zipotee bure tu kwa watu kutukanana na kuandika ujinga siku nzima.
 
siungi hoja mkono naogopa kupelekewa matamuzi mengne yasiyo na tija km kina molel na mtulia.napendekeza kodi ya kichwa ili watanzania wote tuwe na uchungu na nch yetu.tupo zaidi ya 55milion wenye kulipa kodi ya kichwa tupo km 35mil*20,000=750Bilion nipato kubwa sna kwa mwaka nakila mtu atakuwa na uchungu sbb anajua kodi yake ndyo inayojenga bara2 inamlipa police mwalimu mbunge kuliko shv weng wanaona nikm serikali inatoa tu kma zawadi fulani kwao bila kujua ni kodi yao
 
Ng'ombe humlishi unachofikiria ni kumkamua maziwa tu, mwishowe utakamua damu! Mawazo ya kipumbavu kabisa!
 
Lengo la mtoa mada ni kutaka tukaishi shimoni...na we we utakuwa umetumwa kuja kututesti tutalipokeaje tens mshindweeee.. kwa unyonyaji huo pamoja na kutufanya tuishi kama mashetani bado mnaona haitoshi hebu tupumzisheni kidogo sasa khaaaa.
 
Sina shida kama nikikatwa hiyo 200 halafu ikaenda kufanyia mambo yatakayoboresha maisha ya Mtanzania, na sio viini macho tunavyoviona sasa.
 
Wazee wa kutest mitambo! Omba sasa wachangiaji waongezeke then "conclude"
 
Hii imegandamiziwa kwa majirani zetu,mwisho watatuona mazuzu Ku copy kila kitu kutoka kwao,nyie ubunifu umewashinda mpaka kila kitu mgandamizie?
 
Ng'ombe humlishi unachofikiria ni kumkamua maziwa tu, mwishowe utakamua damu! Mawazo ya kipumbavu kabisa!
Watanzania hawapendi kulipa kodi, lakini wengi wao utawaona siku nzima wanashinda kwenye mitandao ya kijamii wanapost ujinga na kuangalia uchafu. Sasa bora hiyo pesa wanayopoteza kununu bando, waanze kuipia zaidi ili itumike kulinufaisha taifa kwa ujumla.

Waalimu wetu wanateseka kukosa nyumba za kuishi wakati huku kwenye mitandao ya kijamii watu wanachezea pesa tu.
 
Mitandao ni kama bia kwa sasa, kila mwaka kodi ya bia inaongezeka na kusababisha ongezeko la bei ila wanywaji hawajawahi kuacha kunywa, pia unaposema tutasevu kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu ni mawazo dhahania sana, kwa sasa serikali (inadai) inasevu sana mfano kuzuia safari za nje, kuunganisha wizara, kuondoa watumishi hewa lkn hujaambiwa hicho kiasi kimefanyiwa nini! Vile vile sio wote katika mitandao wanatukana, kwani wewe ulichoandika umetukana? Jifunze kusikia hata yale ambayo huyataki, taifa hili ni kama limekengeuka hatuwezi kuwa na watu wa mtazamo mmoja tu yaaani KUSIFIA tu, huo ni ujinga kuwaza hivyo kwa sababu binadamu tuko tofauti katika nyanja nyingi
Sasa kama mitandao ya kijamii ni kama bia, kwanini unalalamika? Wewe tulia tu, kodi ikianzishwa na wewe uwe mlipaji basi.
 
Sipati picha watu wanavyoomba kupangiwa kazi ya ofisi ya makamu wa rais
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom