Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Sipati picha watu wanavyoomba kupangiwa kazi ya ofisi ya makamu wa rais
Usishangae kwa sababu sasa ni ofisi ya Mkm/Rais ndo iliyo TOO ACTIVE na ina overshadow ofisi ya rais Magufuli.
Najua hili hatapenda kulisikia lakini huo ndo ukweli wa mambo.
 
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Rais wetu Dr. John Joseph Pombe Magufuli ni Rais sahihi kwa Tanzania yetu. Magufuli ana faa sn kuwa Rais wa Tz. Tz ilipokuwa imefiki, Rais kama JPM alihitajika sana. Watu karibia wauze nchi yote!!!! Kila sehemu wizi!! Kila sehemu pa mtu!!



Binafsi nampenda sn JPM ila afanyie maboresho mapungufu yafuatayo:

1. Udikteta. Yaani yy ndie anafahamu kila kitu nchini, wengine wote hatujui kitu. Na kwame naomba asiige Utawala wa Rwanda. Rwanda ni ndogo sn, kueneza hiyo style ya Utawala Tz itamchukua si chini ya miaka 10-15 na muda wake utakuwa umeisha. Hivyo raia hatuta ambulia kitu isipokuwa manung’uniko. Amekaribia kutupangia muda wa kulala mwisho saa 4 usiku.


2. Akubali kushaulika na kukosolewa. Hii ni sifa nzr kwa Mwanasiasa.

3. Akomeshe mauawaji. Mauwaji siyo hulka ya Watanzania. Watanzania wana hulka ya kupendana sana. Kama kuna genge la chama au chombo chochote linafanya ukatili huu alishughulikie, awakataze, na kulivunja kama KIBITI.


4. Democracy/Multipartism. Aruhusu uhuru wa Habari na kujieleza. Pia mfumo wa vyama vingi Tz siyo wa bahati mbaya bali ni wa makusudi na una manufaa yake. Siasa ni ajira. Unapo zuia siasa unakosesha watu kazi. Pia kupitia Demokrasia na mfumo wa vyama vingi Rais hukosolewa na kujifunza na kufanya vyema zaidi.


5. Nyumba alizo uza azirudishe. Uwezo anao iwapo atakuwa na dhamira na nia hiyo. Kwani nyumba zile nyingi zipo City Centers na Strategic Places mfano, karibu na Mahakama, Office za Mikoa, nk. Atenge Budget ya fidia. Naamini fidia yake ni ndogo sn ukilinganisha na hasara za kupangisha watumishi au kuishi hotelini. Hii itamuondolea doa na kupunguza Criticism za Wapinzani wake.


6. Aboreshe sera zake za uchumi. Hakuna Private kompany kwa miaka 2 itakayo ripoti ongezeko la mauzo au faida. Nyingi zimepenguza uzalishaji, Redundacy, na zingine kuuzwa (TBL, ACACIA), zingine kusimamisha uzalishaji (DANGOTE) na nyingi zimeshindwa hata kulipa mishahara (Wana madeni hadi miezi 6). Tutarajie MASS UNEMPLOYMENT akiendelea na sera zake hizi!!! Vyuo vikuu vingi vimekufa!! Na vingi vimeshindwa hata kulipa mishahara (un employment soon). Uchumi kiwe kipa umbele ya sera zako mwaka 2018. Angalia Rais wa Russia Putin anachofanya, ni ujasusi wa kiuchumi siyo wa MAUAWAJI!!


7. Hotuba: Nampenda sn JMP. Anaongea kitu toka rohoni. Ana nia njema kabisaa na Tz. Japo jazba humuzidi na kushindwa kujizuia na kujikuta ameongea lugha/maneno ya kutisha (Singida speech), kuogofya, au kutukana (Bukoba-tetemeko speech). Hii si sifa nzr kwa Rais kwa wananchi wake!! Kauli zake zimefanya watu wamchukie hata walio mpenda!! Kwa sasa yy ni Rais wa wote, uwe CHADEMA, ACT, CCM, CUF, TADEA, NLD, nk.

Kurugenzi ya Ikulu-Ndg Geryson Msigwa na Mkurugenzi wa TISS- Mlazimisheni Rais kusoma Hotuba. Apende asipende. Nchi si mali ya Rais. Ni mali ya Raia wake. Rais ni mtu tu, atapita ila amani na umoja wa Watanzania ni mhimu mno kuliko CCM nzima!! Nakuombea Mungu akusaidie ulimudu hili Rais wangu.


8. Tenganisha kofia ya CHAMA na U RAIS. Muda wako wa kutajataja CCM umeisha!! Huwa unasababisha vijana nyuma ya mikutano yako kukuzomea au kuguna. Hii haina mantiki kwako. CCM ni chama kubwa huna haja ya kuanza kampeni kwa sasa, utashinda tu hata 2020. Jikite katika utendaji uliotukuka. Uliosababisha upendwe na kila Mtanzania ukiwa Wizara ya Ujenzi. Toa msamaha kwa wafungwa wote na walio CELLO POLISI kwa Makosa ya kisiasa, uchochezi, kukosoa, na viongozi wote wa vyama pinzani na ww. Kujisahihisha ni jambo jema, hakuna aliye mkamilifu chini ya Jua. Naamini hata Mungu atakupunguzia dhambi zako.

Nadhani hata huyo Mange Kimambi, hakuchambi kwa mazuri ila kwa Mabaya yako!! Yaani Rais hujawahi hata siku 1 kukemea haya mauaji , utekaji na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaoendelea nchini? Rais gani ww?


9. KUWA NA JOPO LA USHAURI. Usitoe kauli yoyote bila kulishirikisha hili japo. Kamwe usikubali kushauriwa na hawa VILAZA wa DAR. Wengi wana utoto, mihemko na ufinyu wa Maono kama viongozi. Iwe ni timu ya (TISS, WACHUMI, JWTZ, WAHADHIRI, WATAFITI, WANASAYANSI, nk).

Ukifanaya hayo 2020 huitaji kampeni kuingia IKULU. Ila ukiendelea na siasa zako za sasa 2019/2020 hadi mnyakue masanduku ya kura vituoni ndio mshinde!!

WAVIVU, MAFISADI NA WEZI WOOOOOTE LALA NAO MBELEMBELE KWA MBELE.

MUNGU AZIDI KUKUONGOZA RAIS WANGU. NAKUPENDA SANA.
Huyu hana tofauti na kakamega sory kagame .
alishasema hapangiwi au umesahau hii kauli yake[emoji61]
 
Kwa Mhe Rais wetu, Rais Mtukufu na wa wanyonge wote Tanzania.
Salaam.
Jana nilikuangalia na kukusikiliza kwa makini ulipokuwa wanatoa neno baada ya kuwaapisha Majaji uliowateua wiki hii. Niliona pia ulipomsimamisha CAG na kumuuliza kama kuna pesa trillioni 1.5 alizogundua kwamba zimeibiwa na akakujibu hakuna.
Pia nilikusikia ukisema umeisoma taarifa ya CAG mwanzo hadi mwisho.
Haraka nilikimbilia kitabu changu ambacho nami nimekisoma mwanzo mpaka mwisho.
Nilipofungua ukurasa wa 34 niligundua haya:-

1. CAG Anasema, kwa mwaka wa fedha 2016/17 Serikali ilipanga kukusanya mapato yenye dhamani ya Shilingi Trillioni 29.5

2. Mapato halisi yaliyokusanywa ni Shilingi Trillioni 25.3

3. Serikali ilitumia shilingi Trillion 23.8

4. Trillioni 25.3 ukitoa Trillion 23.8 ni Trillion 1.5 ambazo ndizo anazotaka apewe maelezo.

Mtukufu Rais CAG hajasema pesa zimeibiwa. Wala ktk hatua hii hawezi kusema hivyo. Anachosema fedha hizo, matumizi yake hayaonekani na hazipo popote. Inawezekana kweli zimeibiwa, zimetumika kwa uzembe bila kufuata sheria au zipo mahali fulani.

Kwa taratibu za kibunge Maafisa Masuuli(accounting officers) wanatakiwa wampelekee ushahidi wa matumizi yake au ziliko ktk Kamati ya bunge ya Hesabu za Serikali yaani PAC mbele ya CAG ili hoja hii ifungwe. Kama wakishindwa kuifunga PAC na CAG sasa wanaweza kuomba msaada wa Polisi na au Takukuru kutafuta wezi au wabadhirifu.

Mhe Rais bila shaka umesoma pia ktk ripoti kwamba Serikali ktk ujumla wake imepata HATI CHAFU.
Wakati ukipokea taarifa hii Ikulu uliagiza Mkurugenzi wa Mji wa Kigoma Ujiji na wa Pangani watumbuliwe kutokana na maeneo yao kupata hati chafu.

Mhe unasubiri nini kumtumbua Katibu Mkuu hazina kwa kuisababishia Serikali yako kupata Hati chafu? Mbona kila mara unaapa kuwa mtu wa haki na jana uliwaagiza Majaji wakatende haki kwa Watanzania hasa wanyonge?

Mheshimiwa Serikali yako imepata doa kubwa. Vyombo vya dola haviwezi kulizuia kwa kuwatisha wanaoandika. Hizi ni fedha za maskini wote unaowatetea wauza maandazi, mitumba, mchicha na wengine wakubwa.

Ninakushauri baadala ya kuwatisha wanaohoji, waagize watendaji wa Serikali yako, wapeleke maelezo ya kutosha yenye ushahidi kwa CAG. Vinginevyo hatutaacha kukuuliza kila mara ZIKO WAPI PESA ZETU SHILINGI TRILLION 1.5

Jana Naibu waziri wa fedha alisema uongo Bungeni akidai sehemu ya fedha hizo Billioni 200 Serikali ya Muungano iliisaidia Serikali ya Zanzibar kukusanya mapato yake huku Bara.

Wote tunajiuliza vyanzo vya mapato ya ZNZ huku bara ni vipi? Hebu atutajie tuvijue na je! utaratibu huo ulikuwa wa 2016/17 peke yake tangu uhuru au ulikuwepo Taifa lisijue?
Mheshimiwa naona nakuchosha lakini nataka kusema neno la mwisho.
Inawezekana unadanganywa sana na waliokuzunguka na kwamba hawakuambii mambo mengi kwa faida yao. Wanapenda tu kukuambia yale wanayogundua unapenda kuyasikia na wanaogipa kukukosoa kutokana na ukali wako. Panua wigo wasikilize hata wale ambao hupendi kuwasikia hutakosa jambo lenye faida. Asante.
 
Kwa Mhe Rais wetu, Rais Mtukufu na wa wanyonge wote Tanzania.
Salaam.
Jana nilikuangalia na kukusikiliza kwa makini ulipokuwa wanatoa neno baada ya kuwaapisha Majaji uliowateua wiki hii. Niliona pia ulipomsimamisha CAG na kumuuliza kama kuna pesa trillioni 1.5 alizogundua kwamba zimeibiwa na akakujibu hakuna.
Pia nilikusikia ukisema umeisoma taarifa ya CAG mwanzo hadi mwisho.
Haraka nilikimbilia kitabu changu ambacho nami nimekisoma mwanzo mpaka mwisho.
Nilipofungua ukurasa wa 34 niligundua haya:-

1. CAG Anasema, kwa mwaka wa fedha 2016/17 Serikali ilipanga kukusanya mapato yenye dhamani ya Shilingi Trillioni 29.5

2. Mapato halisi yaliyokusanywa ni Shilingi Trillioni 25.3

3. Serikali ilitumia shilingi Trillion 23.8

4. Trillioni 25.3 ukitoa Trillion 23.8 ni Trillion 1.5 ambazo ndizo anazotaka apewe maelezo.

Mtukufu Rais CAG hajasema pesa zimeibiwa. Wala ktk hatua hii hawezi kusema hivyo. Anachosema fedha hizo, matumizi yake hayaonekani na hazipo popote. Inawezekana kweli zimeibiwa, zimetumika kwa uzembe bila kufuata sheria au zipo mahali fulani.

Kwa taratibu za kibunge Maafisa Masuuli(accounting officers) wanatakiwa wampelekee ushahidi wa matumizi yake au ziliko ktk Kamati ya bunge ya Hesabu za Serikali yaani PAC mbele ya CAG ili hoja hii ifungwe. Kama wakishindwa kuifunga PAC na CAG sasa wanaweza kuomba msaada wa Polisi na au Takukuru kutafuta wezi au wabadhirifu.

Mhe Rais bila shaka umesoma pia ktk ripoti kwamba Serikali ktk ujumla wake imepata HATI CHAFU.
Wakati ukipokea taarifa hii Ikulu uliagiza Mkurugenzi wa Mji wa Kigoma Ujiji na wa Pangani watumbuliwe kutokana na maeneo yao kupata hati chafu.

Mhe unasubiri nini kumtumbua Katibu Mkuu hazina kwa kuisababishia Serikali yako kupata Hati chafu? Mbona kila mara unaapa kuwa mtu wa haki na jana uliwaagiza Majaji wakatende haki kwa Watanzania hasa wanyonge?

Mheshimiwa Serikali yako imepata doa kubwa. Vyombo vya dola haviwezi kulizuia kwa kuwatisha wanaoandika. Hizi ni fedha za maskini wote unaowatetea wauza maandazi, mitumba, mchicha na wengine wakubwa.

Ninakushauri baadala ya kuwatisha wanaohoji, waagize watendaji wa Serikali yako, wapeleke maelezo ya kutosha yenye ushahidi kwa CAG. Vinginevyo hatutaacha kukuuliza kila mara ZIKO WAPI PESA ZETU SHILINGI TRILLION 1.5

Jana Naibu waziri wa fedha alisema uongo Bungeni akidai sehemu ya fedha hizo Billioni 200 Serikali ya Muungano iliisaidia Serikali ya Zanzibar kukusanya mapato yake huku Bara.

Wote tunajiuliza vyanzo vya mapato ya ZNZ huku bara ni vipi? Hebu atutajie tuvijue na je! utaratibu huo ulikuwa wa 2016/17 peke yake tangu uhuru au ulikuwepo Taifa lisijue?
Mheshimiwa naona nakuchosha lakini nataka kusema neno la mwisho.
Inawezekana unadanganywa sana na waliokuzunguka na kwamba hawakuambii mambo mengi kwa faida yao. Wanapenda tu kukuambia yale wanayogundua unapenda kuyasikia na wanaogipa kukukosoa kutokana na ukali wako. Panua wigo wasikilize hata wale ambao hupendi kuwasikia hutakosa jambo lenye faida. Asante.
Pesa Trillion 1.5 imetumika kununua ndege, kukomboa ndege Canada, kuwanunua wabunge, madiwani wa chadema, kurudia chaguzi, uchakachuaji, kuwabambikia kesi, kuwapiga Risasi, kuwafunga jela Wapinzani nk pesa nyingi ya Nchi imetumika kwa mambo ya hovyo hovyo ikiwemo kumlipa Cyprian msiba na kafulila kutengeneza Uzushi na Propaganda za kishamba na kijinga jinga kuwahadaa watanzania.
 
Nchi inaongozwa na wasukuma wawili washamba toka kolomije na chato wanatumia Katiba ya kuanzia 1971- 1979 ya uganda ni katiba ya marehemu idd Amin dada, wake-copy Tabia zote za marehemu idd Amin Dada na msaidizi wake marehemu colonel Maliyamungu, ambao walikuwa watu Hatari na wakatili hakuna mfano, walichukua pesa Hazina ya uganda hata usiku na Gavana alipokataa aliawa na Tanzania ya sasa Gavana aliyepita alikuwa akigoma kutoa pesa kienyeji ndipo wakamtoa na kumpachika wao ambaye huwapa pesa mda wowote hata saa nane usiku , utawala huu wa Awamu ya Tano unaendesha Nchi kienyeji sana, Maliyamungu Bashite Naibu Rais ana nguvu kuliko waziri mkuu na makamu wa Rais hata Bunge, kwa bahati kipindi hiki watanzania wameamka hawataki kusikia Propaganda za polepole wala ujinga wa akina kafulila na Cyprian msiba.
 
Nafasi ya mshauri wa Rais inatendewa haki?
Mh.Rais kujibizana na wanamitandao/wanasiasa kwenye majukwaa yenye maudhui tofauti ni sahihi?
Je,kuna haja ya kuhutubia taifa kila mwezi?
Je,hotuba ya mh.Rais inatakiwa kuandaliwa jitaalamu zaidi?
Je,ni muhimu mh.Rais kufuata yale tu yaliyoandaliwa kwenye hotuba bila kuathiri maudhui yaliyokuudiwa?

Ushauri wa CAG usichukuliwe juu juu alimaanisha kwa kutumia lugha ya kisomi mtu mwingine angechafua hali ya hewa.
 
Nafasi ya mshauri wa Rais inatendewa haki?
Mh.Rais kujibizana na wanamitandao/wanasiasa kwenye majukwaa yenye maudhui tofauti ni sahihi?
Je,kuna haja ya kuhutubia taifa kila mwezi?
Je,hotuba ya mh.Rais inatakiwa kuandaliwa jitaalamu zaidi?
Je,ni muhimu mh.Rais kufuata yale tu yaliyoandaliwa kwenye hotuba bila kuathiri maudhui yaliyokuudiwa?

Ushauri wa CAG usichukuliwe juu juu alimaanisha kwa kutumia lugha ya kisomi mtu mwingine angechafua hali ya hewa.
Kwa sasa ni zidumu fikra za Mwenyekiti wa CCM pekee, mshauri mkuu hana vyeti na ni Naibu Rais unategemea nini?
 
Ni heri ashauriwe na bashite atamuelewa mara moja sio wewe! Ndivyo alivyo.
Maliyamungu idd Amin Bashite ndiyo mshauri mkuu wa Mtukufu malaika toka. Kwani ulidhani kuna mshauri mwingine mkuu? wapo washauri wengine lakini ni waoga wa kumkosoa humshauri kile anachopenda kukisikia ikiwemo kudhoofisha upinzani na kurejesha mfumo wa chama kimoja kama Cuba na China .
 
Mimi nashindwa kuelewa kabisa, inaonekana hawa viongozi kwanza hawana maelewano wenyew kwa wenyew. Anachoongea Pole pole ni tofuti na Mkuru na naibu wa fedha.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom