Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Mleta thread umetumwa. Lengo lenu ni namba 1,Prof Muhongo. Mzee wa Machame,Baba wawili,akisikia hilo jina,mhhh!! Kitu kigonga nguo ya ndani. Wauza juice,biashara ya nishati hamwezi
 
Mnamfichia aibu siyo? Juzi anaapishwa niliona aibu alishindwa kusalimia hata wageni kwa Kiinglish! Wengine wanajitoa akili eti tunatukuza lugha za Wageni wakati mwanao anasoma English Medium, Wadanganye hao siyo Mimi.

Kwenye kampeini alisifiwa sana kwamba anajua vilugha vyoote kumbe mweupe Kimataifa.

Hapana hizi ni chuki binafsi sasa mtu ana PhD ashindwe just kusalimia tu?
 
Kwani Maalim Seif anatekeleza ilani ipi kama Makamu wa Rais wa Zanzibar?

ile ipo kwenye katiba ya Zanzibar, je hii ya kwako ipo kwenye katiba ya muungano?hau ni maaba tu. labda ungemuombea viti maalum tu ili apeleke mchango wake bungeni na kumpa tafu kiongozi mkuu.
 
Msifananishe China na Tanzania kwa kigezo cha lugha wachina wanajiweza sisi walala hoi tu

Mkuu, kwa nini unajivunjia heshima kwa kudharau chako? Kwa tabia za namna hii mtu utajikuta unamkana mzazi wako alikuja kukutembelea kutoka kijijini. Kiswahili ni chetu tukupende, tukikuze mpaka kifike huko unakotaka wewe. Mbona mtoto wa malkia Elizabeti wa Uingereza anajifunza kiswahili na anakipenda? Heshimuni vyenu mheshimiwe...
 
Hapana hizi ni chuki binafsi sasa mtu ana PhD ashindwe just kusalimia tu?

PhD alisoma kwa ujaja ujanja wa kitanzania. Waziri Si ana mchuzi anaandikiwa na wasomi walala wima. Kiukweli tuliaminishwa kuwa anajua lugha nyingi sana kumbe anajua Kisukuma, Kizinza, Kiha, Kijita, Kikerwe,Kisubi etc. Kimataifa bado sana wote tulijionea uwanja wa Taifa. Amesoma Kemia. H20+Mg0=
 
Katika nchi yenye wanasheria waliobobea kashindwa kumpata hata mmoja kamrudisha yule yule aliyekua anashindwa kujibu maswali bungeni atawezaje kuchagua sura mpya kwenye baraza la mawaziri, ccm ni ileile.
 
Mheshimiwa Rais mteuliwa, kwa heshima na taadhima hili ni ombi binafsi kwako.

Nnaomba uhakikishe huyu mrembo wa ACT Bi Anna Mughwira unamuingiza bungeni na unampa wadhifa anaostahiki, huyu mama ni kichwa adhyim na adim kabisa.

Nimemfatilia mikutano yake mingi sana ya kampeni, anatoa vitu kichwani utafikiri ana word processor inayopanga na kuchuja anachokizungumza kutoka kichwani bila kusoma.

Halikadhalika leo kanifurahisha sana alipostukizwa na kutoa hotuba pale Diamond, ilikuwa fupi na imelenga points zote nzuri na ameeleweka vyema kabisa.

Anna heko sana na nitakuunga mkono katika siasa zako.

Naunga mkono Hoja.
 
Ni wazo zuri,nadhani kuna haja ya kulifanyia kazi.Wenzetu katika kututawala wanatumia mbinu mbili soft power na hard power.Hard inatumika kama soft imeshindwa.Language ni soft power na imefanikiwa sana.
Ili kuipa hadhi na kuitangaza lugha yetu ya taifa, nashauri rais wetu mpya atumie Kiswahili katika shughuli zote rasmi za kitaifa na kimataifa. Cha msingi ni kuwa na wakalimani mahiri katika shughuli za kimataifa. Hii itainua hadhi na heshima ya nchi yetu badala ya kuendelea kuthamini lugha za kigeni. Tumekuwa watumwa mno wa lugha ya kiingereza mpaka kufikia hatua kudhani kuwa mtu anayeongea kiingereza vizuri ndiye aliye elimika wakati si kweli. Elimu ni uwezo siyo kuongea kiingereza. Hiki kiingereza cha "izi, wozi, wea, kongrugesheni, ameizingi, wati?, yu no, no problemu hakitusaidii kitu. Na kwa ujinga wetu tunafundishana kwa lugha tusiyoijua vizuri matokeo yake watoto wanafeli halafu tunawaona wajinga kumbe sera zetu ndio mbovu. Wachina, wakorea, wajerumani, wareno, wafaransa mbona wanatumia lugha zao na wanapiga hatua kubwa sana katika uchumi na sayansi. Sisi na kiingereza chetu cha kuombea maji tumefika wapi zaidi ya kutudhalilisha?

Maoni yangu haya hayana maana kuwa sitambui uwezo mkubwa wa kiingereza alio nao dr. Nataka aendeleze pale mwenzake alipoachia mwenzake, kwani alianza kwa kuhutubia kwa kiswahili kwenye mkutano wa AU lakini baadaye akaacha. Mimi nashauri Dr. sasa ajikite pamoja na mambo mengi kuitangaza lugha ya kiswahili kimataifa kwa yeye mwenyewe kuitumia badala ya kiingereza. Huwa naona viongozi wa nchi nyingine kama za kiarabu pamoja na kuwa wanajua kiingereza lakini utakuta wanazaunguza kiarabu na kisha wasiojua kutafsiriwa. Wakalimani sasa hivi tunao wengi, ni vizuri wakatumika vizuri kuikuza lugha yetu ya taifa. Ukweli ni kuwa unapotumia lugha mama au lugha ya taifa una kuwa na uhuru na uwezo mkubwa sana wa kujieleza na kuelezea kuliko unapotumia lugha za kigeni. Kwa watanzania wengi lugha yetu ya mama ni kiswahili.
 
Ha ha ha! apewe nafasi kwa kipi kwa kwenda kuhudhuria jpm anapewa cheti? hana lolote! labda kama mnatafuta huruma kwa wanaccm mpate kubebwa!
 
Hii ni chuki binafsi.Ni mbaya, kwa kuwa you can never be objective..
Mnamfichia aibu siyo? Juzi anaapishwa niliona aibu alishindwa kusalimia hata wageni kwa Kiinglish! Wengine wanajitoa akili eti tunatukuza lugha za Wageni wakati mwanao anasoma English Medium, Wadanganye hao siyo Mimi.

Kwenye kampeini alisifiwa sana kwamba anajua vilugha vyoote kumbe mweupe Kimataifa.
 
Kweli kunabaadhi ya uliyo wataja hawastahili hata kidogo kuwemo ila kuna majembe hayata kosa mwakyembe mwigulu lukuvi muhongo Hawa ntasikitika sana wakikosa hapa kazi tu
 
Tanzania ya Magufuli ni ya viwanda ili vijana wengi wapate ajira, wakati ile Tanzania ya Mkapa ilikuwa ya kuviuza viwanda na kuwakosesha vijana wengi ajira. Kila nikimuangalia usoni mzee Mkapa anaonekana kama vile mwenye furaha sana kuliko zile zama za Kikwete. Wasiwasi yangu mimi asije akapeleka mkono wake kwa Rais Magufuli kwa kutumia njia ya uzoefu wake na ugeni wa Rais Magufuli kumshawishi mambo mabaya kama vile kumalizia kuyauza yale mashirika aliyoyabakiza enzi zake kama vile posta, simu, reli, umeme, ndege na DAWASA, na kuzirudisha kwa wenyewe shule za umma zilizokuwa zimetaifishwa na Nyerere kama vile Mkapa alivyofanya kwenye shule za Magamba, Mazengo, Forodhani, n.k ambazo hivi sasa zimegeuka kuwa shule za watoto wa matajiri tu wenye fedha. Kama haitoshi, Mkapa enzi zake alipunguza wafanyakazi wengi sana na kusitisha ajira mpya kiasi cha kusababisha hali ngumu sana katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Kwake mzee Mkapa "paka ni paka" bila kujali rangi yake, alithamini zaidi wageni wenye fedha kuliko wazawa wakati wa zoezi lake la ubinafsishaji wa viwanda, majengo, mahoteli, migodi, n.k. Wazawa tuliachwa tumeduwaa tunangalia mashamba yetu makubwa na viwanda vikigawiwa kwa wageni ambao walishindwa kuviendeleza na kufa hadi leo. Wageni hawa walitumia rasilimali zetu hizo kuombea mikopo mikubwa nje ya nchi ambayo hawakuiwekeza kuendeleza zile mali walizoziweka rehani ili kupata mikopo hiyo.

Dr. Magufuli akili za kuambiwa tafadhali sana uchanganye na PhD yako.
 
Pamoja na kwamba sina imani na chama chako, ila naomba unishawishi wewe binafsi katika serikali yako.
Kama ulivyojinaji kuwa serikali yako, yani Tanzania ya Magufuli itakuwa KAZI TU, basi naomba udhihirishe hivyo katika baraza lako la mawaziri.

Kabla hata sijataka kujua waziri mkuu ambaye ataendana na sura ya kauli mbiu yako, lakini nataka usituletee watu hawa ambao walikuwa mzigo kwa taifa na waliolifikisha nchi hapa ilipo chini ya aliyekutangulia pamoja na waziri mkuu wake.

1. Sopteter Muhongo.
Huyu pamoja na kwamba tunaambiwa hakuhusika moja kwa moja kwenye kashfa xa escrow lakini alikuwa kinara wa utetezi katika sakata hili. Pia ni miongoni mwa waziri wenye elimu kubwa lkn hakuwa na mkakati bunifu wa kutatua tatizo la umeme nchini zaidi ya kuiacha tanesco kwenye deni kubwa. Pia ni miongoni mwa viongozi ambao hawathamini wawekezaji wa ndani, anaamini nchi itajengwa na wazungu au wachina.

2. Lazaro Nyalandu.
Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao tumeshuhudia tembo wakiuliwa kwa wingi, na twiga wetu wakisafirishwa kwenda nje, hafai katika serikali yako, kwani atafanya kazi ya mazoeaa ya serikali ya awamu ya 4.

3. Mwigulu Nchemba.
Pamoja na kwamba hakukaa kwenye wizara ya fedha kwa mda mrefu, lkn ni miongoni mwa vijana ambao hawana adabu katika taifa hili. Ni mmoja wa wanasiasa wachanga ambao hajali matamshi yake mbele ya umma, haangalii baada ya hapa athari zake zitanipeleka wapi, sio mstaarabu.

4. Willium Lukuvi.
Huyu kwa mwendo wa kasi inayohitajika nchini hatufai, utendaji wake hauto tofautiana na wa awamu ya 4, hana jipya ndani ya serikali yako.

5. Shukuru Kawambwa
Huyu ni moja ya mawaziri walioshusha thamani ya elimu yetu. Sio mbunifu. Fedha za fidia za rada mpaka leo hatujui matumizi yake yalienda wapi, hatufai kabisaa.

6.Hawa Ghasia.
Huyu mama bado uchama umemkaa kichwani kuliko maslai ya taifa. Hayupo active katika utendaji wake.

7. Jumanne Maghembe.
Huyu ni moja ya mawaziri ambao ndio chanzo cha huduma mbovu za elimu na maji. Elimu yake ni kubwa lkn haina msaada kwetu.

8.Harrison Mwakyembe.
Huyu kinachompa sifa ni lile sakata la richmond ambalo tunamwona kama shujaa. Lakini kiukweli hafai hata kuwa mwenyekiti wa kijiji. Sijaona mafanikio yake katika wizara alizozisimamia, ni mzigo ana asili ya mtandao ambao ni chanzo cha utendaji mbovu nchini. Ni mafya wa kisiasa

9. Magreth Sitta
Mama huyu tangu zama ni outdated, haendani na kasi ya dunia, yupo nyuma na mda, hafai katika serikali yako.

10. Sofia Simba
Hana tofauti na Mama sitta, tena huyu uchama na mtandao wa uongozi umemjaa kichwani, hafai katika serikali yako.

11. Andwer Chenge
Najua huyu unamfahamu vema

12. Anna Tibaijuka
Najua unamfahamu vizur

13. Willium Ngeleja
Najua wamfahamu vzr

NB.
1. Mheshimiwa Rais kuna vijana wengi ambao naamini katika utendaji wao lkn siamini kundi lake, na mmoja wao ni Januari Makamba. Huyu binafsi namwamini kiutendaji, ubunifu lakini kinachomsumbua ni kutaka madaraka makubwa, kundi lake lililo nyuma yake, Huyu badala ya kuchapa kazi atakuwa anawaza urais baada yako kustaafu. Kwa mtazamo wangu ungemweka kando kwa mda baada ya miaka miwili ndo uumpe majukumu.

2. Kwa kukusaidia mh Rais ni vema ukachagua mawaziri wachache ambao wengi wao hawakuwa mawaziri, sio viongozi katika chama, vijana, wenye elimu isiyo na shaka. Hawa ndio wataileta tanzania mpya ya HAPA KAZI TU.

Mh Rais ukikosea kwenye baraza la mawaziri basi jua umeuwa nchi, na hapo tutadhibitisha kuwa hakuna cha Magufuli 4 change itakuwa ccm ni ile ile.

Asantee.

Hivi nani aliwapigia kura yani wasingestahili hata kurudii bungeni. Sana sana Mwingulu Nchemba .
 
Kweli kunabaadhi ya uliyo wataja hawastahili hata kidogo kuwemo ila kuna majembe hayata kosa mwakyembe mwigulu lukuvi muhongo Hawa ntasikitika sana wakikosa hapa kazi tu

tatizo nchi hii kuwa kiongozi mbovu ni mpaka uwe fisadi, kuna mengi ya kuangalia, sio uadilifu pekee
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom