Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Watu hawapindishwi vyeo,hela za matibabu mfanyakazi wa chini mpaka anyenyekee na madudu mengine mengi ili hali vibosile kila siku safari na vikao.
Vikao Na safari za nje Na ndani wao tu kila siku Na wafunga kamba za viatu vyao
 
Mh. Magufuli kama unataka kufanikiwa kujua madudu yaliko katika Taasisi na mashirika ya umma nchini,lenga kukutana na watumishi wa ngazi za chini na sio vibosile tu na utoe fursa kwa kila mtumishi kuandika kikaratasi cha matatizo yaliyoko katika Taasisi husika bila kuweka jina lake na kisha karatasi hizo zikafanyiwe kazi na tuhuma/matatizo yatakayokuwa yamejitokeza yachunguzwe na hatua zichukuliwe kwa watakaobainika kuwa wazembe na kusababisha mateso kwa wafanyakazi au ubadhirifu n.k.


Mh.Raisi,Watumishi wa ngazi za chini ndio wanaoweza kukueleza ukweli na si vigogo au watumishi wandamizi katika Idara,Wizara na Taasisi mbalimbali za umma.

Tunaomba juhudi hizi zisiwe za muda tu bali zidume kwa miaka yote 5.
Hii ni mbaya kama nina bifu na boss si namlipua tu
Magufuli anajua wizi wote.
Bandari stay tuned..
 
Hii ni mbaya kama nina bifu na boss si namlipua tu
Magufuli anajua wizi wote.
Bandari stay tuned..
Ndio maana nasema tuhuma zichunguzwe kwanza na haiwezekani watumishi kadhaa wote wakulalamikie mtu mmoja tu tena kwa tuhuma zinazofanana.
 
Ushauri mzuri sana. Akiufuata huu ndio utakuwa mwanzo wa kutatua kero za watu wa chini ambao ndio wanakandamizwa.
 
Umenena. lakini kuna angalizo: wafanyakazi wa chini sio mesaja na wafagiaji tu. Hata wa kada za kati nao wananyanyaswa.
 
Mh. Magufuli, kama unataka kufanikiwa kujua madudu yaliko katika Taasisi na mashirika ya umma nchini,lenga kukutana na watumishi wa ngazi za chini na sio vibosile tu na utoe fursa kwa kila mtumishi kuandika kikaratasi cha matatizo yaliyoko katika Taasisi husika bila kuweka jina lake na kisha karatasi hizo zikafanyiwe kazi na tuhuma/matatizo yatakayokuwa yamejitokeza yachunguzwe na hatua zichukuliwe kwa watakaobainika kuwa wazembe na kusababisha mateso kwa wafanyakazi au ubadhirifu n.k.


Mh. Rais,Watumishi wa ngazi za chini ndio wanaoweza kukueleza ukweli na si vigogo au watumishi wandamizi katika Idara,Wizara na Taasisi mbalimbali za umma.

Tunaomba juhudi hizi zisiwe za muda tu bali zidume kwa miaka yote 5.

Pia ili kuwatendea haki wakurugenzi, hakikisha bajaeti wanazaomba na kutengewa wanazipata kwa wakati na zinazotosheleza mahitaji yao ili kama ni uzembe basi uwe ni uzembe wao wenyewe wa kushindwa kusimamia utekelezaji wa mipango waliojiwekea.

Matatizo ya nchi hii yote yanafahamika.ni ya kimfumo tu.pindua mfumo basi mambo yataenda
 
Nafarijika kuona watu walokuwa na mihemuko wa lile kapi kama salary slip, mmawia, shost na matola wakirudi kundini kwa kasi, karibuni sana CCM bado niffah peke yake
 
Salary slip hapa naungana na wewe!
Umekuwa tofauti na wenzako ambao hadi sasa hawakubaliani na ukweli kwamba Raisi ni Magufuli!
Kinachotakiwa kwa sasa ni ushauri kama huu wako wa kusaidia kuijenga Tanzania!
 
Hatupokei ushauri wa chadema.asante

Samahani kwa hili ila nna mashaka kama umekamilika kichwani.... Tanzania yetu sote na ni jukumu la kila mtanzania bila kujali itikadi yake kuhakikisha tunapata Tanzania iliyo bora...tatizo wanaccm mmejimilikisha nchi shame on you!
 
Huo ni ukweli na ushauri mzuri pia nashauri awe akipanga mwenyewe ni lini na kero gani anataka kwenda kuishughulikia, ili kuepuka wapambe kumharibia kwa kuwatonya walengwa mapema

Urais ni Taasisi inayotakiwa kuwa na Ulinzi wa kiitifaki a.k.a Presidential Security Protocol, ili kumuwezesha anayekishika cheo hicho cha juu kabisa katika nchi awe salama na aongoze kwa muda mrefu akiwa salama.

Kuna faida kubwa Katika ziara za kushtukiza, kwamba unajionea hali halisi na kuchukua hatua Madhubuti. Hilo ni jambo jema, lakini ikumbukwe kuwa wakati unafanya hivyo, unazidi kujijengea marafiki wengi ambao ni wananchi, na wakati huo huo unajitengenezea maadui wachache waliokuwa na maslahi binafsi hapo mwanzo.

Hawa maadui wachache ndio wa hatari zaidi kwa mustakabali wa Ulinzi wa Kiongozi.

Sasa ili kuwa na Ulinzi thabiti dhidi ya hawa wachache wa hatari, inabidi ziara za Rais zile very secured kwa kuzingatia Presidential Security Protocol zote muhimu ili Kiongozi huyo wa nchi awe salama katika Uongozi wake.

HIVYO ZIARA ZA KUSHTUKIZA ZINA FAIDA KWA WANANCHI LAKINI ZINA HATARI KWA USALAMA WA KIONGOZI MKUU WA NCHI KAMA NILIVYOELEZA HAPO JUU.

NI MATUMAINI YANGU WAHUSIKA WATAUCHUKUA USHAURI HUU NA KUJIPANGA VIZURI KWA USALAMA ZAIDI.
 
Ushauri mzuri sana huu mkuu, bila shaka wana watu wake wa karibu watampelekea
 
Urais ni Taasisi inayotakiwa kuwa na Ulinzi wa kiitifaki a.k.a Presidential Security Protocol, ili kumuwezesha anayekishika cheo hicho cha juu kabisa katika nchi awe salama na aongoze kwa muda mrefu akiwa salama.

Kuna faida kubwa Katika ziara za kushtukiza, kwamba unajionea hali halisi na kuchukua hatua Madhubuti. Hilo ni jambo jema, lakini ikumbukwe kuwa wakati unafanya hivyo, unazidi kujijengea marafiki wengi ambao ni wananchi, na wakati huo huo unajitengenezea maadui wachache waliokuwa na maslahi binafsi hapo mwanzo.

Hawa maadui wachache ndio wa hatari zaidi kwa mustakabali wa Ulinzi wa Kiongozi.

Sasa ili kuwa na Ulinzi thabiti dhidi ya hawa wachache wa hatari, inabidi ziara za Rais zile very secured kwa kuzingatia Presidential Security Protocol zote muhimu ili Kiongozi huyo wa nchi awe salama katika Uongozi wake.

HIVYO ZIARA ZA KUSHTUKIZA ZINA FAIDA KWA WANANCHI LAKINI ZINA HATARI KWA USALAMA WA KIONGOZI MKUU WA NCHI KAMA NILIVYOELEZA HAPO JUU.

NI MATUMAINI YANGU WAHUSIKA WATAUCHUKUA USHAURI HUU NA KUJIPANGA VIZURI KWA USALAMA ZAIDI.

Yule mwanadada mwenye rasta yuko makini sana, anahakikisha rais yuko safe, na hapo kwenye msafara TISS ni wa kumwaga, wengine wanakuwa wameshatangulia eneo la tukio
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom