Wana JF,
Habaru zenu
Nianze kwa kumpongeza Rais Magufuli kwa uzalendo alionao!
Tumo katika zama za kutumbua majipu. Tumemulika sana upande Wa uchumi au mapato ya serikali. Utumbuaji Wa majipu TRA, TPA, PCCB nk.... ni jambo linalotupa faraja.
Japo tumeangalia uchumi, lakini kuna jipu LA AJIRA KATIKA OFISI ZA UMMA. Naamini ni kubwa kuliko yote.
Watanzania tuna haki ya kupata ajira serikalini kwa misingi ya uadilifu. Zisiangaliwe dini, kabila, koo, eneo tunakotoka na jinsia. Cha kuangaliwa uwe uwezo Wa MTU kufanya kazi husika.
Kwa masikitiko makubwa, ajira serikalini zinazingatia dini, kabila na kanda katika wizara na mashirika mengi. Ukuu wa idara unazingatia dini, kabila na kanda. Huu mdudu umeanza kututafuna na utatupeleka pabaya sana.
Tutajikuta tuna dini fulani au kabila fulani ndiyo limeendelea kiuchumi sana kuliko dini au makabila mengine.
Kuna baadhi ya mashirika kama TRA, TPA, NSSF, baadhi ya mabenki nk...., yamelalamikiwa kuwa na ukabila na udini.
Tumefika mahali tumeanza kusema, kwa mfano, kupata kazi maliasili lazima uwe kabila fulani. Kupata kazi Tra lazima uwe kabila fulani, kupata kazi nssf lazima uwe dini fulani.....
Hii nchi ni yetu sote. Tuna haki ya kupata ajira kwa usawa bila upendeleo.
Namuomba Muh. Rais aunde tume ya kuchunguza jambo hili. Kwa mfano, Je TRA kuna zaidi ya nusu ya wafanyakazi kabila moja au dini moja! Kama ni hivyo kwa nini? Tuendelee na uchunguzi katika mashirika na wizara zote. Penye mapungufu ajira ziitishwe upya na uwiano uzingatiwe.
Bila kufanya hivi, watu wataendelea kuvutana na baadhi ya kabila, dini na kanda zitaendelea kuwa za wasindikizaji. Watoto wao hata wakisoma haitokua rahisi kupenya katika ajira serikalini. Barua za kazi lazima zitaendelea kuwekwa kapuni.
TANBIHI
Tuache mtindo Wa kukwepa kuzungumzia udini na ukabila. Tunazidi kulifanya jipu hili liwe kubwa zaidi na sugu. Kadri linavyozidi ukubwa watu wanazidi kuumia. Rais Magufuli tafadhali Pasua jipu hili.