Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Mkuu upo sober kweli au unaongea under the influence of kinda kitu cha Arusha? Hata kama ulikua unakaa nae nyumba moja sasa hivi huyo sio mwenzako, status yake imebadiika so have some respect unapo mu address
Status ya magufuli haijabadilika ofisi ndio imembadilisha . Magufuli hata ukiomba kumuona kwa kibali Cha kutress pass unaingia ikulu sema watu wanaogopa protocol yake.
 
Kiukweli ukitoa protokali za urais za mh Magufuli yeye binafsi ni mwana Sana Tena msela kabisa ila sijui atajinasua vipi na kifungo Cha Ben sanane na Azory Gwanda ila jpm ni mwana Sana Tena msela Sana Mungu amlinde!
Alianza vibaya sana, kwa kutaka watu wote wamuogope yeye.

Unakumbuka akina Lema walivyowekwa mahabusu miezi kadhaa?

Na "Dikteta Uchwara" ilivyomtia ukichaa, huku makesi yote Lissu akiyapangua?

Alipotoka huko, akaona atengeneze masheria ya kikandamizi, ya kunyima watu uhuru na haki zao; na kama hiyo haikutosha akaona kwamba wapinzani kuendelea kufanya siasa kutamnyima alichokitamani sana...'sifa' .

Akapiga marufuku mikutano ya siasa ili abaki yeye peke yake akitamba na kufanya kampeni miaka minne yote. Kabinafsisha TBC, kila akigeuka huku anasikika yeye pekee.

Kaweka magenge kila sehemu waimbe nyimbo zake tu, lakini wapi, bado haridhiki na haoni kama waTanzania wamekogwa roho zao.
Kaanza kujitangaza mwenyewe, kwamba hakuna aliyefanya kazi kubwa kama yeye, waTanzania wanamsikiliza tu hawasemi kitu.

Kwa hiyo ana hofu kubwa hapo alipo. Anajua akiruhusu uchaguzi ulio huru kabisa, ataangukia mchanga licha ya kufanya mambo mengi ambayo waTanzania wengi wanayaona kuwa ni mambo mazuri kwa taifa. Lakini wengi hawaoni maana ya kuuza haki zao kwa gharama ya miradi hiyo inayofanyika, pamoja na uzuri wake.

Aliponyakua Mahakama na Bunge, vyote viwe mfukoni mwake, hapo katimiza kabisa kuwakatisha tamaa waliokuwa wakisubiri kwamba atarekebisha aliyokwisha haribu.

Rekodi yake imekwishaganda. Watu hawatekwi na hawapotei ovyo tena, lakini kumbukumbu zipo na hofu zinaendelea kwamba huenda ni mapumziko tu ya muda.

Mengi ya haya asingeruhusu yamchafue, kwa hakika msimamo wake wa kulinda mali za taifa hili na hii miradi mikubwa ingemfanya awe kiongozi wa kuheshimiwa na kukumbukwa. Kwa hakika, asingehangaika kamwe kupiga kampeni kwenye chaguzi zinazokuja..

Sasa hivi ni lazima awategemee polisi na wasimamizi wa uchaguzi kuwa na hakika ya kuchaguliwa ngwe nyingine.
 
Magufuli ni msela Sana ila protocol yake imemharibia japo Ana nafasi ya kurekebisha
Hakuwahi kukwambia yeye "hajaribiwi"; au "sijibiwi hivyo"? Basi huyo atakuwa ni mwingine siye huyu unayemwandika habari zake
Kajaribu kumtafuta huyo rafiki yako huko mlikokuwa mnakutana.
 
Umeanzisha uzi na kuujaza mwenyewe kwa comments zako...hongera...ila ngoja nimuite huyu jamaa aje angalau atoe neno Kawe Alumni hebu njoo umsikilize kijana simuelewi
 
Najua hakuna Mwana CCM anaweza. Kwa hilo tu, basi Lazima Rais aone Ikulu ni kiti cha moto.
Sasa basi afanye nini ili kazi iwe nyepesi. Abadili style yake ya uongozi.

Hakuna Rais anasifiwa duniani kama Magufuli. Je sifa hizo sio stahili yake!? Kama kweli anazistahili kwanini aseme kazi ni ngumu.

Nafikiri kwa sifa ambazo mnampa Magufuli ilibidi awe Rais Mwenye furaha duniani.
Je! CCM Mnamsifu Rais kinafiki!? Ili tu muendelee neemeka na keki ya Taifa!?
Jitafakarini.

Mtajijua wenyewe.. Ila mimi binafsi ninavyomuona Rais , licha ya nia yake njema kabisa iliyothabiti kuibadilisha nchi. Kuna nafsi inamsuta. Ni ipi hiyo..!? Mnajua.

Bado ana nafasi ya kujirekebisha. Kuteleza Si kuanguaka. Anaweza kuanza upya. Kuijenga nchi katika uwazi na DEMOKRASIA ya kweli.
 
Rais Magufuli anafanya kila jitihada kuwatumikia Watanzania

Tuendelee kumuombea
 
Sijawahi kuona awamu yenye uwoga kama hii, unajisifu unafanya kazi nzuri na unasema unapendwa na wananchi alafu mpinzani wako unatumia dola kumziba mdomo

Ningekuwa JPM ningeachana na harakati za kupambana na upinzani, kwa sababu nafanya kazi nzuri na wananchi wananipenda ningewaachia wananchi wenyewe waumalize upinzani kwenye sanduku la kura na sio kutumia nguvu ya dola kuwanyanyasa na kuuwa upinzani.

Kitendo cha jpm kutesa wapinzani kinamshushia heshima sana , huko nchi za wenzetu wanatuona kituko, ajifunze kwa watangulizi wake waliishi na upinzani kwa akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
....waliishi na wapinzani wake kwa akili..... hii sentensi inaibua masaaki mengine kuntu kama ifuatavyo;
i. Ni kama unasema awamu ya tano nawatumii iyo unayoiita 'akili' kuishi na hao mbadala wao?
ii. Hivi ni nani anamuhitaji mwenzake mtawala au mpinzani?
iii. Kama unaona rais anatosha tuondoke wote upinzani, bunge ma mihimili yote matumizi yatapungua na
tutapata Maendeleo kwa haraka
 
Hivi kuna gazeti au media yeyote inayoratibu maagizo anayotoa JPM na kuyaweka wazi ili wananchi tujue kama yametekelezeka na kutoa mawazo yet kama Ni kweli au wanamdang'anya.
Magazeti zetu yatoe ukrasa maalum juu ya maelekezo ya rahisi na jinsi yalivyo fanyiwa kazi yaone yatakavyo uza


Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Futa uchaguzi wa 2020 ngazi zote waliopo waendelee kwa miaka mingine mitano. Hela ya uchaguzi ikatumike kwa shughuli nyingine za maendeleo kama barabara. Tunahitaji barabara zaidi kuliko tunavyohitaji uchaguzi au madiwani wabunge au hata raisi. Hakuna sababu ya kufanya uchaguzi kwa sababu Magufuli ameshapita na wengine hawana chochote wanachofanya kwa maslahi ya wananchi. Ikikupendeza futa hata bunge hatulihitaji kwa sasa, utakuwa unateua wabunge panapokuwa na sababu ya msingi.
2. Ongeza wigo wa kodi kwa kuanza kukusanya mapato kutoka maneo mengine mfano michango ya harusi,sherehe, sadaka na zaka kwenye nyumba za ibada. Nafikiri tukiangalia huko kuna mapato ya kutosha tu yatasaidia maendeleo. Hili ni muhimu sana kwa waziri wa fedha kuliangali
kwaleo haya yanatosha yafanyieni kazi
 
Mkuu mleta uzi hakuna kilevi chochote ulichotumia kabla ya kuandika uzi huu? Au chanzo chochote cha moshi hujatumia?
 
Jamani watanzania tumuunge mkono raisi wetu ametupa heshima Kubwa sana ndani Na nje ya nchi , binafsi nasafiri sana nje ya nchi kila mahali nikienda naambiwa you have a good president .


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Jamani watanzania tumuunge mkono raisi wetu ametupa heshima Kubwa sana ndani Na nje ya nchi , binafsi nasafiri sana nje ya nchi kila mahali nikienda naambiwa you have a good president .


Sent from my iPhone using JamiiForums
kumuunga mkono rais, si suala la matakwa ya mtu ni suala la kikatiba na kisheria. kwa hiyo wote tunamuunga mkono ndio maana tunatekeleza maagizo yake yote kwa utimilifu.
wasi wasi wetu ni kununua ndege hali ya kuwa barabara zetu zinazounganisha wilaya ni mbaya mno, kutokuajiri, kuwanyima watoto wetu mikopo, kutumia fedha za dawa kununua wapinzani? kupotea kwa watu nk, nk.
bado tunamuunga mkono, tutamlinda, tutamtunza lakini na yeye afikirie haya malalamiko.
 
Kiukweli nchi ilihitaji raisi kam Mh John Pombe, nimuombe raisi asikize maoni ya wapinzani kwani nao wanamaono ambayo yanaweza kuwa na mchango chanya kwa nchi yetu. Sema wapinzani wawe wastarabu kwani raisi ni zaidi ya mwenye nyumba!!! Viva President tuongoze

Sijaona mtu muoga kama yeye maana akiona wapinzani wanampa changamoto anawaka sana kwenye uongoZi ni bora aache upinzani washike madaraka
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom