Maoni ya Baba wa taifa kuhusu uwekezaji

Maoni ya Baba wa taifa kuhusu uwekezaji

The Burning Spear

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
4,118
Reaction score
9,864
Mheshimu sana kiongozi anayeongea bila kusoma mahali...
Baba wa Taifa alikuwa na maono ya Mbali sana.

Nafikiri tutazidi kujifunza kutoka kwake for years. Utafakiri alikuwa analijua hili la DPW Pamoja na kubadili Sheria zetu.
 
Duuh,mwabukuzi anongea Leo kumbe Nyerere alishaongea. Tunakwama wapi kutumia maliasili asilia kuwaajiri hata hao wanaotaka kutununua. Kwani ile mkataba hawezi ukabadilika wakawa watumwa wetu.
 
Duuh,mwabukuzi anongea Leo kumbe Nyerere alishaongea. Tunakwama wapi kutumia maliasili asilia kuwaajiri hata hao wanaotaka kutununua. Kwani ile mkataba hawezi ukabadilika wakawa watumwa wetu.
Ndiyo Mwalimu aliyaongea hayo.

Hili litukumbushe sisi sote kuwa, tunahitaji kuwa na 'AKILI' na 'ROHO MPYA' ili tuwe na uelewa uliobora na basi utashi bora.

Kiufundi, nasibu ya haya yote si 'mambo ya maoni'--ni mambo ya kiufundi kuhusu 'Matukio-Wakati-Machaguo ya Kitaasisi-Jamii'.

Ukimsikiliza Mwalimu kwenye hiyo video, unaweza 'trizanisha' nasibu ya 'Machaguo ya Kitaasisi' na basi 'unabaki na majibu yako' kuhusu lolote lile linalohusiana na sura na mwenendo wa nchi. Kwa mfano 'maneno ufunguo' kwenye hiyo video ni 'Imani' na 'Uwezo'; kisha tafakuri ya masuala ili kukadirisha pembetatu ya 'Uono Mifumo'--mambo ya 'dhamira' na 'vina vya tafsiri' vyenye kuakisikia kwenye 'miongozo/sera ama sheria...

Ukiwa na uono na ufikirifu mifumo ilivyo ni Elimu 2.0, mambo ya sura na mienendo ya jamii si 'Sayansi ya Roketi'...

Hapa ndipo 'shida' iliko -- kwenye 'vina vya tafsiri' juu ya 'Akili' na 'Utashi'.

Hauhitaji kusema 'mimi ninatambua...' kama vile haya ni mambo ya hoja ya ubishani--kama vile 'maoni'; Maoni si 'Maarifa'--vivyo hivyo sayansi si 'maoni'. Kadiri yoyote ya hata sayansi kuwa ni 'Maoni' ni nyumba iliyojengwa kwenye mchanga ama tuseme jumba la makuti kwenye nyika; huweza kusambaratikia mbali pepo kali za kuvuma wakati mmoja hata mwingine...

Haya ni mambo ya kiufundi kabisa... Hayana cha 'Unafsi' labda tu 'Mazoea' ya tabia ya utu wa kujitafsiri hivi ama vile kwa kuwa 'unapenda'--ama kufikiria kama wengine wengi. Nasibu ya kujua ilivyobora huhitaji nidhamu ya kuwa tayari kuikana nafsi na basi 'uono wako uwe fasaha' na wenye kujitegemea wenyewe.

...

Tazama hiyo picha ya 'Trizania'--ruhusu 'akili yako ya ndani itafsiri'; achana na akili ya nyama kwenye hiyo itakutoa kapa!

Hizo alama nne zina ufunguo kwa ajili ya 'ufunuo' kuhusiana 'Utashi' wa 'ndani na nje' ya mtu.

Alama ya juu ni alama ya 'Mboni ya Jicho', ni hiyo mboni ya jicho ipo kwenye fraktali tunayoweza kuiita 'Mpango Mzima'. Kwa kuwa hiyo ndiyo fraktali ya 'Uono'--uono ulio ni hatma ya kubangua utatusho wa 'Mtenda-Kitendo-Matokeo'.

Fraktali ya Kushoto-chini, hiyo unayoiona ni picha-gramu ya 'Utaasisi' ambavyo kiufundi ni alama mbili katika moja; MSALABA na MKASI. Alama hizi mbili ni akitipu ya 'Imani' na 'NIa' katika moja. Msalaba ni alama ya 'Imani' inayoshikilia 'Mbingu na Nchi'. Kwa hivyo pande nne za msalaba huwakilisha 'Ardhi', 'Maji', 'Upepo' na 'Moto'. Mkasi ni alama ya 'Ulinzi wa Malango'--ni alama ya uaminifu kwa ajili ya 'Shika Neno, Tenda Neno'. Kwa hivyo zao la Msalaba na Mkasi kiufundi ni 'UTASHI'.
 
Back
Top Bottom