Maoni ya Mwanasheria kuhusu kufungiwa kwa Diamond Platnumz na Rayvanny

Yajayo yanafurahisha kuchoshana tu ivi wasanii wengine hawawaoni kutwa kumkalia kooni mondi nimeamini mti wenye matunda ndio hupigwa mawe, hayo matusi ni gani mbona hawaja yataja nadhani wakate rufaa tu.
 
Akina diamond walifanya makosa lakini kutokuwapa haki ya kusikilizwa kunafanya haki iwe upande wao. Wakienda mahakamani maana yake malalamiko yao watakuwa hatukupewa haki ya kusikilizwa. Hivyo BASATA hawawezi kutumia akina mond kutokata rufaa na kukaidi adhabu kama defense hata kidogo.
 
Niwie radhi kama nimekukwaza lakini nilidhani nawe unalitetea hilo linalojifanya liko juu ya sheria nakati sheria ilimtangulia hata Baba na Babu zake.

Na bado atakuja ataipita hii dunia kwa mauti lakini sheria zitabaki pale pale katika weledi wake, maana kila mamlaka iliyopo duniani imetoka kwa Mungu.

Ndiyomaana huwa tunaaswa tuwatii sana wenye mamlaka(Serikali na viongozi wake kiujumla).
Mkuu, umekosea kuniquote.
 
Sizani kama maamuzi ya BASATA yanakatiwa rufaa, kama kukata ninamini wangefanya hivyo.
 
Mapato kupitia upumbavu na matusi ambayo hayaleti maana wala maadili yoyote kwa kizazi cha sasa na kijacho?

Ama kweli duniani wajinga tuko wengi sana kuliko wale waliojaliwa hekima na utashi wa utu.
 
Kwa dharau alizoonyesha kwa taasisi alafu sheria im'bebe ndio pale nnapokua upande wa rais hata akikandamiza sheria maana haina faida yoyote kwa baadhi ya jamii,

Sioni tofauti ya mtu kuiba au kuua alafu sheria inam'beba kisa kuna kifungu cha sheria kinakinzana na jambo flani.
 
Mbele ya sheria hata muuaji ana haki ya kusikilizwa na ndio maana Kuna rufaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…