Mwigulu Nchemba alitumia muda mwingi kutamba yeye na Rais walivyoboresha utendaji wa ofisi ya CAG hadi ikaibua yale madudu yaliyoibuliwa lakini hakuwa na mkakati wowote ule wa jinsi atakavyomsaidia Rais kuthibiti wizi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kama taarifa ya CAG ilivyobainisha.