Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

Ninaamini
 

Attachments

  • 1699161101226.png
    1699161101226.png
    1.4 MB · Views: 1
Jana wabunge walionyesha kukosa imani na baraza la mawaziri
 
Ni dhahiri wabunge hawana imani madudu yaliyoibuliwa na taarifa ya CAG baraza la mawaziri wana dhamira, upeo au hata ukereketwa wa kuyashughulikia
 
Sisi leo tutajikita kwa mchango wa mawaziri 3 tu ambao michango yao imethibitisha hawana sifa ya kuendelea kwenye baraza la mawaziri.

Hatuafiki ni baraza lote limeoza ila hawa 3 ni bure kabisa
 
Katika hawa mawaziri watatu Profesa Kitilya Mkumbo ndiye aliyetia fora kwa kukosa upeo, kujitutumua kama ni mjuaji na kukosoa maeneo aliyopaswa kuufyata
 
Mbunge Salome Makamba aliibua hoja nzito ya kuonyesha taarifa za CAG zinaonyesha maovu yanaongezeka na hivyo kuonyesha watendaji waandamizi wameshindwa kuthibiti hali hiyo

Watendaji wamekuwa magwiji wa kufuata taratibu za kiuhasibu ili kulinda wizi na ubadhirifu wa mali ya umma!
 
Profesa Kitilya Mkumbo katika harakati zisizo na mashiko akainua mkono na kudai Salome alisema uongo maana yeye aliisoma taarifa yote ya CAG yenye kurasa 800+ hajaona tuhuma zilizoibuliwa na Salome Makamba
 
Mdee alimpeleka puta Profesa Kitilya Mkumbo kwa kufanya kazi ambayo Kitilya hakuifanya
 
Nayo ilikuwa kuutaja ukurasa ambao taarifa ya CAG imeonyesha hati safi kupungua huku zenye utata zikipaa na hivyo kuthibitisha mtazamo ya kuwa profesa Kitilya Mkumbo aidha hajaisoma taarifa ya CAG au hata kama aliisoma hakuielewa
 
Alipoombwa na spika aipokee taarifa ya Salome Makamba Nape Nnauye aliyekuwa akitetea utendaji wa serikali na kuibeza taarifa ya CAG Nape Nnauye kwa kiburi alikataa kuikubali na hakutaja sababu ya maana kwanini haikubali zaidi ya kuwakumbusha wabunge muda wa utumishi wake bungeni ni wa kitambo hoja ambayo haikuwa na uhusiano na sababu alizotakiwa kutoa kuelezea kinagaubaga kwanini ameikataa taarifa ya Salome
 
Mwigulu Nchemba alitumia muda mwingi kutamba yeye na Rais walivyoboresha utendaji wa ofisi ya CAG hadi ikaibua yale madudu yaliyoibuliwa lakini hakuwa na mkakati wowote ule wa jinsi atakavyomsaidia Rais kuthibiti wizi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kama taarifa ya CAG ilivyobainisha.
 
Mwigulu Nchemba alilitumia jina na cheo cha urais kama kinga ya yeye asiadhibiwe kwa kushindwa kuthibiti hasara kubwa nchi inapata kwa yeye kuendelea kuwa waziri wa fedha mzigo
 
Tulichojifunza Nape Nnauye, Profesa Kitilya Mkumbo na Mwigulu Nchemba wamepoteza imani ya wabunge na vyema bunge likatoa azimio la kuwapigia kura ya kukosa imani nao
 
Back
Top Bottom