Jaji mkuu ndiye mwenyekiti wa kamati ya uteuzi wa makamishina wa Tume ya uchaguzi sasa ikija kesi ya kupinga zoezi zima la uteuzi wa hao makamishina atatoa wapi uhalali wa kuunda jopo la majaji wamchunguze yeye mwenyewe kama hakuhongwa wakati alipokuwa akiyatelekeza majukumu yake.
Atajifunga kengele mwenyewe au atateua jopo analojua litamsafisha.
Swali la msingi kuliko yote ni sahihi kwa majaji kuwa mahakimu kwenye kesi yao yenyewe?
Pia, je ni sahihi kwa wateule wa Rais kuwa wajumbe wa Tume ya uchaguzi kama lengo siyo kuijaza Tume ya uchaguzi na makada wa CCM ili watangaze matokeo ya uchaguzi bila kuhesabu kura?
Ieleweke tuliyoyashuhudia kwa macho yetu wenyewe uchaguzi wa 2020 ndiyo yanatusukuma tuoni kama tunavyooni.
Hatuna imani na wateule wote wa Rais kujihusisha na Tume ya Uchaguzi kwa sababu wanayo masilahi binafsi ya kuhakikisha CCM inaendelea kutawala hata kama wapigakura wameikataa kwenye masanduku ya kura
Si sahihi kwa Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi kuwa jaji kwani kuhesabu kura tuna kesi ya kuamua? Jaji na kuhesabu kura wapi na wapi?
Sifa ya ujaji ni unafiki mtupu wa kuipa Tume ya uchaguzi sifa ya haki wakati haina bali ni kijiwe na kichinjio dhidi wa wagombea wa vyama vya siasa vya upinzani
Halafu bado tunajigamba tuna Mwanasheria Mkuu mbavu zangu hoi